Tenzi ya Rohoni | Unapoufungua Moyo Wako kwa Mungu

17/04/2020

Wakati hamumwelewi Mungu na hamjui asili Yake,

mioyo yenu haiwezi kamwe kufunguka, kufungukia Mungu.

Mara utakapomwelewa Mungu wako, utaelewa kilicho moyoni Mwake,

na kufurahia kilicho ndani Yake kwa imani na usikivu wako wote.

Unapofurahia kile kilicho ndani ya moyo wa Mungu, kidogo kidogo, siku baada ya siku,

unapofurahia kile kilicho ndani ya moyo wa Mungu, moyo wako utakuwa wazi Kwake.

Moyo wako unapokuwa wazi kweli, moyo wako unapokuwa wazi kweli,

utaiona dharau, utaiona aibu

ya maombi yako ya kupita kiasi na yenye ubinafsi.

Moyo wako unapokuwa wazi kweli,

moyo wako unapokuwa wazi kweli,

utaona dunia isiyo na mwisho moyoni mwa Mungu,

na kuwa katika ulimwengu wa maajabu yasiyosimuliwa.

Hakuna giza mabaya au uongo,

Unapoufungua Moyo wako kwa Mungu.

Ni ukweli tu, imani tu mwanga tu haki kote.

Unapoufungua Moyo wako kwa Mungu.

Yeye ni upendo, Yeye anajali, ana huruma isiyo na mwisho.

Maishani mwako, unahisi furaha,

Unapoufungua moyo wako kwa Mungu.

Hekima na nguvu Zake zinajaza ulimwengu huu,

vile vile mamlaka na upendo Wake.

Unaweza kuona kile Mungu anacho na Alicho

Kinachomletea furaha, na kinachomletea matatizo,

kinachomletea huzuni na hasira, vyote viko wazi kwa wote kuona,

unapoufungua moyo wako kwa Mungu na kumwalika aingie ndani.

kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp