Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Hatua Tatu za Kazi | Dondoo 33

26/10/2020

Katika hatua hii ya mwisho ya kazi, matokeo yanapatikana kupitia kwa neno. Kupitia kwa neno, mwanadamu anaelewa mafumbo mengi na kazi ya Mungu katika vizazi vilivyopita; kupitia kwa neno, mwanadamu anapewa nuru na Roho Mtakatifu; kupitia kwa neno, mwanadamu anapata kuelewa mafumbo ambayo hayajawahi kuelezwa na vizazi vilivyopita, na pia kazi za manabii na, mitume wa enzi zilizopita, na kanuni ambazo walitumia kufanya kazi; kupitia kwa neno, mwanadamu anatambua tabia ya Mungu Mwenyewe, na pia uasi na pingamizi ya mwanadamu, na anakuja kujua dutu yake mwenyewe. Kupitia kwa hatua hizi za kazi na maneno yote yaliyonenwa, mwanadamu anatambua kazi ya Roho Mtakatifu, kazi ya mwili wa Mungu, na zaidi ya hayo, tabia Yake yote. Maarifa yako ya kazi ya usimamizi wa Mungu wa kupita miaka elfu sita ulitwaliwa kupitia kwa neno. Je, maarifa yako hayakuwa ya fikira zako za awali na mafanikio kwa kuyaweka kando pia yalipatikana kupitia neno? Katika hatua ya awali, Yesu Alifanya ishara na maajabu, lakini sio hivyo katika hatua hii. Je si kuelewa kwako kwa nini Mungu hafanyi ishara na maajabu pia kulipatikana kupitia neno? Kwa hivyo, maneno yanenwayo katika hatua hii, yanashinda kazi iliyofanywa na mitume na manabii wa vizazi vilivyopita. Hata unabii uliotabiriwa na manabii haungeweza kupata matokeo haya. Manabii waliongelea unabii pekee, ya kile kitakachotendeka hapo baadaye, lakini sio kazi ambayo Mungu angefanya katika wakati huo. Hawakuongea kuwaongoza wanadamu katika maisha yao, kuwapa wanadamu ukweli ama kumfichulia mwanadamu mafumbo, ama hata kutawaza maisha. Kwa maneno yaliyonenwa katika hatua hii, kuna unabii na ukweli, lakini hasa yanafanya kazi ya kutawaza maisha juu ya mwanadamu. Maneno ya wakati huu sio kama unabii wa manabii. Hii ni hatua ya kazi isiyo ya unabii ila ya maisha ya mwanadamu, kubadili tabia ya maisha ya mwanadamu. Hatua ya kwanza ilikuwa kazi ya Yehova kutengeneza njia ya mwanadamu kuabudu Mungu duniani. Ilikuwa kazi ya kuanzisha kutafuta chanzo cha kazi duniani. Wakati huo, Yehova aliwafunza Waisraeli kuiheshimu Sabato, wawaheshimu wazazi wao na kuishi kwa amani na wengine. Hii ilikuwa kwa sababu watu wa wakati huo hawakuwa ni nini kilichukuliwa kuwa mwanadamu, wala hawakuelewa walivyopaswa kuishi duniani. Ilikuwa lazima Kwake katika hatua ya kwanza ya kazi kuwaongoza wanadamu katika maisha yao. Yote yale Yehova aliwazungumzia hayakuwa yamewahi kujulikana kwa binadamu ama kuwa katika umiliki wao. Wakati huo, Mungu aliwainua manabii wengi kunena unabii, yote kutengenezwa chini ya uongozi wa Yehova. Hii ilikuwa sehemu moja ya kazi ya Mungu. Katika hatua ya kwanza, Mungu hakuwa mwili, hivyo Alizungumza na makabila yote na mataifa kupitia kwa manabii. Yesu alipofanya kazi Yake katika huo wakati, Hakuzungumza sana kama wakati huu wa leo. Kazi hii ya neno katika siku za mwisho haijafanyika katika enzi na vizazi vilivyopita. Ingawa Isaya, Danieli na Yohana walitabiri utabiri mwingi, unabii huo ulikuwa tofauti kabisa na maneno yazungumzwayo sasa. Walichoongelea ulikuwa unabii pekee, lakini maneno ya sasa sio unabii. Iwapo Ningebadilisha Ninayoongea sasa yawe unabii, je mngeweza kuyaelewa? Iwapo yale niliyozungumzia yangehusu mambo baada ya Mimi kuondoka, ungewezaje basi kupata kuelewa? Kazi ya neno haikuwahi kufanyika wakati wa Yesu ama Enzi ya Sheria. Labda wengine wanaweza kusema, “Je Yehova hakuzungumza maneno pia katika wakati wa kazi Yake? Juu yaa kuponya magonjwa, kukemea mapepo na kufanya ishara na maajabu, je Yesu hakuzungumza katika wakati huo?” Kuna tofauti katika vile maneno yananenwa. Ni nini ndiyo ilikuwa dutu ya maneno yaliyonenwa na Yehova? Alikuwa tu Akiwaongoza wanadamu katika maisha yao duniani, ambayo hayakuwa yanahusiana na mambo ya kiroho katika maisha. Ni kwa nini inasemekana kuwa maneno ya Yehova yalitangazwa katika sehemu zote? Neno “kufundisha” linamaanisha kuwaambia waziwazi na kuamrisha moja kwa moja. Hakupa mwanadamu maisha; ila, Alimchukua mwanadamu kwa mkono na kumfunza jinsi ya kumheshimu sana. Hakukuwa na mafumbo. Kazi ya Yehova katika Israeli haikuwa kushughulika na ama kumwadhibu mwanadamu ama kutoa hukumu na kuadibu, ilikuwa kuongoza. Yehova alimwambia Musa awaeleze watu Wake wakusanye mana jangwani. Kila asubuhi kabla ya jua kuchomoza, walikuwa wakusanye mana, iliyotosha tu kuliwa siku hiyo. Mana haingewekwa hadi siku inayofuata, kwani ingeoza. Hakuwakaripia wanadamu au kufichua asili zao, wa Hakufichua mawazo yao na fikira. Hakuwabadilisha watu ila tu aliwaongoza katika maisha yao. Katika wakati huo, watu walikuwa kama watoto; mwanadamu hakuelewa chochote na angefanya hatua za kuelekezwa, na hivyo, Yehova aliamuru tu sheria kuongoza watu.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

The Last Days’ Work Is Mainly to Give Man Life

I

The results of God’s work in the last days are achieved through the word, through the word. The word helps man understand mysteries and God’s work throughout history. It brings man enlightenment of the Holy Spirit, and knowledge of mysteries sealed for centuries. It explains the work of prophets and apostles and the rules when they carried it out. The word makes man know God’s disposition, as well as his own rebelliousness and substance.

II

Through these steps of work and all words spoken, man comes to know the work of the Spirit, and know the work of God’s incarnate flesh, moreover the entirety of His disposition. Your knowledge of God’s 6,000-year work was also attained through the word. Know your old notions and put them aside— was not it too attained through the word?

III

In the previous stage Jesus displayed miracles, but it’s not so in this last stage. Wasn’t it through the word that you finally understood why you don’t see any signs now? The words spoken in this stage surpass work done by apostles and the prophets of the past. Even for prophecies made by the prophets, such results could not have come to pass.

IV

The prophets only prophesied what would happen in the future, but not of the work God was to do at the time. They didn’t speak to lead man, bestow truth, reveal mysteries, and much less did they speak, and much less did they speak to bestow life. Words spoken in this stage contain prophecy and truth, but mainly serve to bestow life upon man. Unlike the prophecies of the prophets, the words at present are a stage of work for man’s life, to change his disposition.

from Follow the Lamb and Sing New Songs

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp