Mazingira ya Msingi ya Uzima Ambayo Mungu Anawaumbia Wanadamu: Sauti

08/09/2019

Kitu cha tatu ni nini? Pia ni kitu ambacho mazingira ya kuishi ya kawaida ya wanadamu yanatakiwa kuwa nacho. Ni kitu ambacho Mungu alishughulikia alipoumba vitu vyote. Hiki ni kitu muhimu sana kwa Mungu na pia kwa kila mtu. Kama Mungu hakushughulikia suala hilo, ingekuwa kizuizi kikubwa kwa kuendelea kuishi kwa wanadamu. Hiyo ni kusema kwamba ingekuwa na athari yenye maana sana kwa mwili na maisha ya mwanadamu, kiasi kwamba wanadamu hawangeweza kuendelea kuishi katika mazingira kama hayo. Pia inaweza kusemwa kwamba viumbe vyote vyenye uhai haviwezi kuendelea kuishi katika mazingira kama hayo. Hivyo hiki ni kitu gani? Ni sauti. Mungu aliumba kila kitu, na kila kitu kinaishi mikononi mwa Mungu. Machoni pa Mungu, vitu vyote vinasonga na vinaishi. Yaani kuwepo kwa kila mojawapo ya vitu vilivyoumbwa na Mungu kuna thamani na maana. Yaani, vyote vina umuhimu katika kuwepo kwao. Kila kitu kina uhai machoni pa Mungu; kwa kuwa vyote viko hai, vitatoa sauti. Kwa mfano, dunia daima inazunguka, jua daima linazunguka, na mwezi daima unazunguka pia. Sauti daima zinatolewa katika uzalishaji na kuendelea na miendo ya vitu vyote. Vitu juu ya dunia daima vinazaa, kukua na kusonga. Kwa mfano, misingi ya milima inasonga na kubadilisha nafasi, na vitu vyote vyenye uhai katika kina cha bahari vinasonga na kuogelea na kwenda hapa na pale. Hii inamaanisha kwamba vitu hivi vyenye uhai, vitu vyote anavyoviona Mungu, vyote viko mara kwa mara, kwa mwendo wa kawaida, kulingana na mifumo iliyoanzishwa. Kwa hivyo, ni nini kinaletwa na uzalishaji wa siri na maendeleo na miendo ya vitu hivyo? Sauti za nguvu. Mbali na dunia, kila aina ya sayari daima ziko katika mwendo, na viumbe vyenye uhai na viumbe hai juu ya sayari hizo pia daima vinazaa, vinakua na viko katika mwendo. Yaani, vitu vyote vilivyo na uhai na visivyo na uhai daima vinasonga mbele machoni pa Mungu, na pia vinatoa sauti wakati huo huo. Mungu pia ameshughulikia sauti hizi. Mnapaswa kujua sababu ya mbona sauti hizi zinashughulikiwa, sivyo? Unaposonga karibu na ndege, sauti ya kunguruma ya ndege itakufanyia nini? Masikio yako yatazibwa muda unavyozidi kusonga. Je, mioyo yenu itaweza kuistahimili? Wengine wenye mioyo hafifu hawataweza kuistahimili. Bila shaka, hata wale wenye mioyo yenye nguvu hawataweza kuistahimili ikiendelea kwa muda mrefu. Hiyo ni kusema, athari ya sauti kwa mwili wa mwanadamu, kama ni kwa masikio au moyo, ni yenye maana kabisa kwa kila mtu, na sauti ambazo ni za juu sana zitaleta madhara kwa watu. Kwa hiyo, Mungu alipoumba vitu vyote na baada ya hivyo kuanza kufanya kazi kwa kawaida, Mungu pia aliweka sauti hizi—sauti za vitu vyote vilivyo katika mwendo—kupitia kwa utendeaji wa kufaa. Hii pia ni mojawapo ya fikira muhimu alizokuwa nazo Mungu alipoumbia wanadamu mazingira.

Kwanza kabisa, kimo cha angahewa kutoka kwa uso wa dunia kitaathiri sauti. Pia, ukubwa wa utupu ndani ya mchanga, pia utaendesha na kuathiri sauti. Kisha kuna mahali mito miwili inapoungana pa mazingira mbalimbali ya kijiografia, ambapo pia pataathiri sauti. Hiyo ni kusema, Mungu hutumia mbinu fulani kuondoa sauti zingine, ili wanadamu waweze kuendelea kuishi katika mazingira ambayo masikio na mioyo yao vinaweza kustahimili. La sivyo sauti zitaleta kizuizi kikubwa kwa kuendelea kuishi kwa wanadamu; zitaleta matatizo makubwa kwa maisha yao. Hili litakuwa tatizo kubwa kwao. Hiyo ni kusema, Mungu alikuwa mwenye kujali sana katika uumbaji Wake wa nchi, angahewa, na aina mbalimbali za mazingira ya kijiografia. Hekima ya Mungu iko ndani ya haya yote. Ufahamu wa wanadamu kuhusu haya hauhitaji kuwa kinaganaga sana. Kila wanachohitaji kujua ni kwamba kitendo cha Mungu kimo humo. Sasa Niambieni, hii kazi ambayo Mungu alifanya ilikuwa muhimu? Yaani, uendeshaji wa taratibu sana wa sauti ili kudumisha mazingira ya kuishi ya wanadamu na maisha yao ya kawaida. (Ndiyo.) Ikiwa kazi hii ilikuwa muhimu, basi kutokana na mtazamo huu, je, inaweza kusemwa kwamba Mungu alitumia mbinu kama hii kupeana vitu vyote? Mungu aliwapa wanadamu na kuumba mazingira haya tulivu, ili kwamba mwili wa mwanadamu uweze kuishi kwa kawaida kabisa katika mazingira haya bila vizuizi vyovyote, na ili kwamba mwanadamu ataweza kuwepo na kuishi kwa kawaida. Je, hii si njia mojawapo ambayo kwayo Mungu huwapa wanadamu? Je, jambo hili alilofanya Mungu lilikuwa muhimu sana? (Ndiyo.) Lilikuwa muhimu sana. Je, ni vipi ambavyo mnashukuru hili? Hata kama hamwezi kuhisi kwamba hiki kilikuwa kitendo cha Mungu, wala hamjui vile Mungu alikifanya wakati huo, je, bado mnaweza kuhisi umuhimu wa Mungu kufanya hilo? Je, mnaweza kuhisi hekima ya Mungu au umakini na wazo Aliyoweka katika jambo hili? (Ndiyo.) Kuweza tu kuhisi hili ni sawa. Yatosha. Kuna vitu vingi ambavyo Mungu amefanya miongoni mwa vitu vyote ambavyo watu hawawezi kuhisi na kuona. Lengo la Mimi kukitaja hapa ni kuwapa tu habari kiasi kuhusu matendo ya Mungu ili muweze kuanza kumjua Mungu. Vidokezo hivi vinaweza kuwafanya mjue na kumwelewa Mungu vizuri zaidi.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VIII

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp