Kama Imani Yako kwa Mungu ni ya Kweli, Utapokea Utunzaji Wake Mara Nyingi

07/09/2019

Mungu kubadilisha nia Zake kwa watu wa Ninawi hakukuhusisha kusitasita au kutoeleweka kokote. Badala yake kulikuwa ni mabadiliko kutoka kwa hasira tupu hadi uvumilivu mtupu. Huu ni ufunuo wa kweli wa kiini cha Mungu. Mungu kamwe si wa kusitasita au asiye na uamuzi katika vitendo Vyake; kanuni na makusudio yaliyo katika matendo Yake yote ni wazi na dhahiri, yasiyo na dosari wala doa, yasiyo kabisa na hila ama njama zozote zilizochanganywa ndani. Kwa maneno mengine, kiini cha Mungu hakina giza wala maovu. Mungu alikasirikia Waninawi kwa sababu vitendo vyao viovu vilikuwa vimefikia macho Yake; wakati ule hasira Yake ilitokana na kiini Chake. Hata hivyo, wakati hasira ya Mungu ilitoweka na akatoa uvumilivu Wake kwa watu wa Ninawi kwa mara nyingine tena, kila kitu Alichofichua kilikuwa bado ni kiini Chake. Uzima wa badiliko hili ulitokana na badiliko katika mtazamo wa mwanadamu kwa Mungu. Katika kipindi hiki chote cha muda, tabia ya Mungu isiyokosewa haikubadilika; kiini cha Mungu cha uvumilivu hakikubadilika; kiini cha Mungu cha upendo na huruma hakikubadilika. Wakati watu wanapotekeleza vitendo viovu na kumkosea Mungu atawashushia ghadhabu Yake. Wakati watu wanatubu kwa kweli, moyo wa Mungu utabadilika, na hasira Yake itakoma. Wakati watu wanapoendelea kumpinga Mungu kwa ukaidi, hasira Yake kali haitakoma; hasira Yake itawalemea hatua kwa hatua mpaka watakapoangamizwa. Hiki ndicho kiini cha tabia ya Mungu. Haijalishi kama Mungu anaonyesha hasira au huruma na wema, mwenendo wa binadamu, tabia na mtazamo wake kwa Mungu ndani ya kina cha moyo wake vinaamrisha kile ambacho kinaonyeshwa kupitia kwa ufunuo wa tabia ya Mungu. Kama Mungu anaendelea kumfanya mtu apitie hasira Yake, moyo wa mtu huyu bila shaka humpinga Mungu. Kwa sababu hajawahi kutubu kwa kweli, kuinamisha kichwa chake mbele ya Mungu au kumiliki imani ya kweli kwa Mungu, hajawahi kupata huruma na uvumilivu wa Mungu. Kama mtu hupokea utunzaji wa Mungu mara nyingi na hupokea huruma na uvumilivu Wake mara nyingi, basi mtu huyo bila shaka anaamini Mungu kwa kweli ndani ya moyo wake, na moyo wake haumpingi Mungu. Yeye kwa mara nyingi anatubu kwa kweli mbele ya Mungu; kwa hivyo, hata kama nidhamu ya Mungu mara nyingi humshukia mtu huyu, hasira Yake haitamshukia.

Maelezo haya mafupi yanaruhusu watu kuuona moyo wa Mungu, kuona uhalisi wa kiini Chake, kuona kwamba ghadhabu ya Mungu na mabadiliko katika moyo Wake yana sababu. Licha ya utofautishaji mkavu ambao Mungu alionyesha Alipoghadhabishwa na wakati Alipobadilisha moyo Wake, jambo ambalo linafanya watu kusadiki kwamba utofautishaji mkavu au nafasi kubwa yaonekana kuwepo kati ya vipengele hivi viwili vya kiini cha Mungu—ghadhabu Yake na uvumilivu Wake—mtazamo wa Mungu kwa kule kutubu kwa Waninawi kwa mara nyingine kunaruhusu watu kuweza kuona ule upande mwingine wa tabia halisi ya Mungu. Mabadiliko katika moyo wa Mungu yanaruhusu kwa kweli binadamu kwa mara nyingine kuuona ukweli wa huruma na wema wa Mungu na kuona ufunuo wa kweli wa kiini cha Mungu. Binadamu hawana budi kutambua kwamba rehema ya Mungu na wema si hadithi za uwongo tu, wala si ughushi. Hii ni kwa sababu hisia za Mungu kwa wakati huo zilikuwa kweli; Mabadiliko ya moyo wa Mungu yalikuwa kweli; Mungu kwa kweli aliwapa binadamu kwa mara nyingine tena rehema na uvumilivu Wake.

Kama Imani Yako kwa Mungu ni ya Kweli, Utapokea Utunzaji Wake Mara Nyingi

Toba ya Kweli Ndani ya Mioyo ya Waninawi Inawapa Rehema ya Mungu na Kubadilisha Hatima Zao Wenyewe

Je, kulikuwa na ukinzani wowote kati ya mabadiliko ya moyo wa Mungu na hasira Yake? Bila shaka la! Hii ni kwa sababu uvumilivu wa Mungu wakati ule maalum ulikuwa na sababu yake. Je, sababu yake yaweza kuwa nini? Ni ile iliyotolewa katika Biblia: “Kila mtu aligeuka kutoka kwenye njia yake ovu” na “kuacha vurugu iliyokuwa mikononi mwake.”

Hii “njia ovu” hairejelei kiasi kidogo cha vitendo viovu, lakini inarejelea chanzo cha maovu katika tabia ya watu. “Kugeuka kutoka njia yake ovu” kunamaanisha kwamba wale wanaozungumziwa hawatawahi kutekeleza vitendo hivi tena. Kwa maneno mengine, hawatawahi kutenda kwa njia hii ovu tena; mbinu, chanzo, kusudio, nia na kanuni za vitendo vyao vyote vimebadilika; hawatawahi tena kutumia mbinu na kanuni hizi kuleta nafuu na furaha mioyoni mwao. Kule “kuacha” katika “kuacha vurugu iliyo mikononi mwake” kunamaanisha kuweka chini au kuweka pembeni, kujitenga kabisa na mambo ya kale na kutorudi nyuma tena. Wakati watu wa Ninawi walipoacha vurugu iliyokuwa mikononi mwao, hii ilithibitisha na vilevile iliwakilisha toba yao ya kweli. Mungu huangalia kwa makini sehemu ya nje ya watu na vilevile mioyo yao. Wakati Mungu alipoangalia kwa makini toba ya kweli katika mioyo ya Waninawi bila kuuliza swali na pia kutambua kwamba walikuwa wameacha njia zao ovu na kuacha vurugu iliyokuwa mikononi mwao, Alibadilisha moyo Wake. Hivi ni kusema kwamba mwenendo na tabia ya watu hawa na njia mbalimbali za kufanya mambo, pamoja na ungamo na toba ya dhambi ya kweli zilizokuwa mioyoni mwao, kulisababisha Mungu kubadilisha moyo Wake, kubadilisha nia Zake, kufuta uamuzi Wake na kutowaadhibu wala kuwaangamiza. Kwa hivyo, watu wa Ninawi waliweza kufikia hatima tofauti. Waliyakomboa maisha yao binafsi na wakati uo huo wakapata huruma na uvumilivu wa Mungu, na wakati huo Mungu pia alifuta hasira Yake.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp