Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kazi na Kuonekana kwa Mungu | Dondoo 51

17/09/2020

Kuonekana kwa Mungu tayari kumetokea katika makanisa yote. Roho ndiye anayeongea, Yeye ni moto mkali, Yeye hubeba uadhama na Anahukumu; Yeye ni Mwana wa Adamu, aliyevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa mshipi kwenye matiti na ukanda wa dhahabu. Kichwa Chake na nywele Zake ni nyeupe kama sufu nyeupe, na macho Yake ni kama mwale wa moto; na miguu Yake iko kama shaba iliyosuguliwa sana, kana kwamba imesafishwa katika tanuru; na sauti Yake kama sauti ya maji mengi. Ana nyota saba katika mkono Wake wa kuume, upanga mkali wenye makali kuwili uko katika kinywa Chake na uso Wake ni kama jua liking’aa kwa nguvu zake!

Mwana wa Adamu Ameshuhudiwa, na Mungu Mwenyewe amefichuliwa waziwazi. Utukufu wa Mungu umekuja, uking’aa vikali kama jua lichomalo! Uso Wake mtukufu unawaka kwa mwanga ung’aao; ni macho ya nani yatathubutu kumtendea kwa upinzani? Upinzani husababisha kifo! Hakuna hata chembe ya rehema kwa kitu chochote unachofikiri katika moyo wako, neno lolote usemalo au chochote ufanyacho. Nyinyi nyote mtakuja kuelewa na kuja kuona ni nini ambacho mmekipata—hakuna chochote ila hukumu Yangu! Naweza kukistahimili wakati nyinyi hamuweki juhudi zenu katika kula na kunywa maneno yangu, lakini hudakiza kiholela na kuharibu ujenzi Wangu? Mimi sitamhurumia mtu wa aina hii! Mengine makubwa zaidi na utaangamizwa katika moto! Mwenyezi Mungu hudhihirika katika mwili wa kiroho, bila hata chembe ya mwili au damu ikiunganisha mwili mzima. Yeye huvuka mipaka ya ulimwengu dunia, kama Ameketi kwenye kiti kitukufu cha enzi katika mbingu ya tatu, Akisimamia mambo yote! Ulimwengu na vitu vyote vimo mikononi Mwangu. Kama Nikisema, itakuwa. Kama Nikiliamua, ndivyo litakavyokuwa. Shetani yu chini ya miguu Yangu, yu katika kuzimu! Sauti Yangu itakapotoka, mbingu na nchi zitapita na kuwa bure! Mambo yote yatafanywa upya na huu ni ukweli wa kweli sana usiobadilika. Nimeushinda ulimwengu, kuwashinda waovu wote. Naketi hapa nikizungumza nanyi; wale wote ambao wana masikio wanapaswa kusikiliza na wale wote wanaoishi wanapaswa kukubali.

Siku zitafika mwisho; mambo yote katika dunia yatakuwa bure, na mambo yote yatazaliwa upya. Kumbuka hili! Kumbuka hili! Hapawezi kuwa na utata! Mbingu na nchi zitapita lakini maneno Yangu hayatapita! Acha Niwasihi kwa mara nyingine tena: Msikimbie bure! Amkeni! Tubuni na wokovu umekaribia! Tayari Nimeonekana miongoni mwenu na sauti Yangu imetokea. Sauti yangu imetokea mbele yenu, uso kwa uso na nyinyi kila siku, safi na mpya kila siku. Unaniona Mimi na Ninakuona wewe, Ninasema na wewe mara kwa mara, uso kwa uso na wewe. Na, bado unanikataa Mimi, hunijui Mimi; Kondoo Wangu wasikia sauti Yangu na bado mnasita! Mnasita! Mioyo yenu imepumbaa, macho yenu yamepofushwa na Shetani na hamuwezi kuuona uso Wangu mtukufu—ni kusikitisha kulikoje! Kusikitisha kulikoje!

Roho saba mbele ya kiti Changu cha enzi watumwa kwa kila pembe ya dunia na Mimi Nitamtuma Mjumbe Wangu kuzungumza kwa makanisa. Mimi ni mwenye haki na mwaminifu, Mimi ni Mungu achunguzaye sehemu ya ndani kabisa ya moyo wa mtu. Roho anaongea na makanisa na ni maneno Yangu yanayotiririka kutoka ndani ya Mwanangu; wale wote ambao wana masikio wanapaswa kusikiliza! Wale wote ambao wanaishi wanapaswa kukubali! Yaleni tu na kuyanywa, na msitilie shaka. Wale wote ambao huyatii na kuyasikiza maneno Yangu watapokea baraka kuu! Wale wote wautafutao uso Wangu kwa kweli watapata mwanga mpya kwa hakika, nuru mpya na ufahamu mpya; wote watakuwa wasafi na wapya. Maneno Yangu yataonekana kwako wakati wowote na yatafungua macho ya roho yako ili uweze kuona siri zote za ulimwengu wa kiroho na kwamba ufalme uko miongoni mwa binadamu. Ingia katika hifadhi na neema yote na baraka zitakuwa juu yako, njaa na baa hazitaweza kukugusa, mbwa mwitu, nyoka, chui wakubwa na chui hawataweza kukudhuru. Utaenda na Mimi, utembee na Mimi, na uingie katika utukufu pamoja na Mimi!

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp