Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Tabia ya Mungu na Kile Anacho na Alicho | Dondoo 234

09/10/2020

Wamebarikiwa wale ambao wamelisoma neno Langu na kuamini kwamba litatimizwa—Sitakutendea vibaya, lakini Nitafanya yale unayoamini yatimizwe kwako. Hii ni baraka Yangu ikija kwako. Neno Langu linapiga siri zilizofichwa ndani ya kila mtu. Kila mtu ana majeraha ya mauti, na Mimi ni tabibu mzuri ambaye anayaponya—njoo tu katika uwepo Wangu. Kwa nini Nilisema kuwa katika siku zijazo hakutakuwa na huzuni tena na hakutakuwa na machozi tena? Ni kwa sababu ya hili. Ndani Yangu, kila kitu kinatimizwa, lakini ndani ya wanadamu, vitu vyote ni vipotovu na bure, na vyote ni vidanganyifu kwa wanadamu. Katika uwepo Wangu utapokea vitu vyote, na utaona na pia kufurahia baraka zote ambazo hungewahi kufikiria. Wale wasiokuja mbele Yangu bila shaka ni waasi, na hakika ndio wanaonipinga Mimi. Hakika Sitawaacha kwa urahisi; Nitamwadibu vikali mtu wa aina hii. Kumbuka hili! Wale wanaokuja mbele Yangu zaidi watapata zaidi, lakini haitakuwa zaidi ya neema. Baadaye, watapata baraka nyingi hata zaidi.

Tangu uumbaji wa ulimwengu Nimeanza kuamulia kabla na kuchagua kundi hili la watu, yaani, ninyi leo. Tabia yako, ubora wa tabia, sura, kimo, familia ambayo ulizaliwa kwayo, kazi yako na ndoa yako, nafsi yako yote, hata rangi ya nywele yako na ngozi yako, na wakati wa kuzaliwa kwako vyote vilipangwa na mikono Yangu. Hata mambo unayofanya na watu unaokutana nao kila siku hupangwa na mikono Yangu, sembuse ukweli kwamba kukuleta katika uwepo Wangu leo kwa kweli ni mpango Wangu. Usijitupe katika vurugu; unapaswa kuendelea kwa utulivu. Kile Ninachokuruhusu kufurahia leo ni mgawo ambao wewe unastahili, na Nilikipangia kabla katika uumbaji wa dunia. Wanadamu wote ni waliozidi sana—wao huwa vichwa ngumu sana au wasio na aibu kabisa. Hawawezi kufanya mambo kulingana na mpango Wangu na mpangilio. Usifanye hilo tena. Ndani Yangu vyote vinakombolewa; usijifunge mwenyewe, kwani utayapoteza maisha yako. Kumbuka hili!

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp