Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Tabia ya Mungu na Kile Anacho na Alicho | Dondoo 246

12/08/2020

Kila sentensi Niliyoizungumza inaendeleza tabia ya Mungu. Mngefanya vizuri zaidi endapo mngetafakari kuhusu maneno Yangu kwa umakini, na kwa kweli mtafaidi pakubwa kutoka katika maneno haya. Dutu ya Mungu ni ngumu sana kuelewa, lakini Ninaamini kwamba nyinyi nyote mnayo angalau baadhi ya maarifa kuhusu tabia ya Mungu. Ninatumai, basi, kwamba mtanionyesha Mimi na kufanya mengi zaidi ya yale ambayo hayakosei tabia ya Mungu. Kisha Nitatuliza moyo. Kwa mfano, mhifadhi Mungu katika moyo wako siku zote. Unapochukua hatua, timiza neno Lake. Tafuta fikira Zake katika kila kitu, na usifanye kile ambacho kitavunjia heshima na kumdhalilisha Mungu. Vilevile, usimweke Mungu nyuma ya akili zako ili ukajaze uwazi wa baadaye katika moyo wako. Ukifanya hivyo, basi utakuwa umekosea tabia ya Mungu. Kama kamwe hutamki matamshi ya kukufanya kukufuru au kulalamika dhidi ya Mungu na unaweza kufanya kikamilifu kila kitu ambacho amekuaminia wewe katika maisha yako yote, pamoja na kutii maneno yote ya Mungu, basi umeweza kuepuka kwa ufanisi kukosea amri za kiutawala. Kwa mfano, kama umewahi kusema “Kwa nini sifikirii kwamba Yeye ni Mungu?” “Nafikiri kwamba maneno haya si zaidi ya kutiwa nuru fulani na Roho Mtakatifu,” “Sifikirii kwamba kila kitu Mungu anachokifanya ni cha kweli,” “Ubinadamu wa Mungu hauna ukubwa zaidi kuliko wangu,” “Neno la Mungu haliaminiki tu,” au matamshi mengine kama hayo ya kuhukumu, basi Nakushawishi wewe kukiri dhambi zako na kutubu. Vinginevyo, hutawahi kuwa na fursa ya msamaha, kwani unakosea sio binadamu tu lakini Mungu Mwenyewe. Unaweza kuamini kwamba wewe unahukumu mtu tu, lakini Roho Mtakatifu wa Mungu hachukulii hivyo. Wewe kutoheshimu mwili Wake ni sawa na kumvunjia heshima Yeye mwenyewe. Kama hali ni hivi, basi si kweli kwamba umekosea tabia ya Mungu? Lazima mkumbuke kwamba kila kitu kinachofanywa na Roho wa Mungu ni kusaidia kazi Yake katika mwili na kufanya kazi kama hiyo vizuri. Ukiyapuuza haya, basi Nasema kwamba wewe ndiwe ambaye kamwe hutaweza kufaulu katika kumwamini Mungu. Kwani umechochea hasira ya Mungu, na kwa hivyo lazima Atumie adhabu inayofaa ili kukufunza adabu.

Kuzoea dutu ya Mungu si jambo dogo. Lazima uelewe tabia Yake. Katika njia hii, polepole utaanza kuzoea dutu ya Mungu Wakati umeingia katika maarifa haya, na hivyo basi kusonga mbele wakati uo huo katika hali kubwa zaidi na ya kupendeza zaidi. Hatimaye, utaaibika kutokana na nafsi yako ya kuchukiza, kiasi kwamba unaaibika kuuonyesha uso wako. Wakati huo, ndipo utakapokosea tabia ya Mungu kwa kiwango kidogo na kidogo; moyo wako utakuwa karibu zaidi na zaidi na ule wa Mungu, na polepole upendo wako Kwake utaweza kukua ndani ya moyo wako. Hii ni ishara ya mwanadamu kuingia katika hali nzuri. Lakini kufikia sasa bado hamjapata hili. Nyinyi hujichosha mkisafiri huku na kule kwa ajili ya hatima yenu, kwa hiyo ni nani angefikiria kujaribu na kuzoea zaidi dutu ya Mungu? Kama hali hii itaendelea, nyinyi mtaweza kuikosea bila kujua amri ya kiutawala kwani mnajua kidogo sana kuhusu tabia ya Mungu. Kwa hivyo, kile mfanyacho sasa hakiweki msingi kwa sababu ya makosa yenu dhidi ya tabia ya Mungu? Kwamba Ninawaomba muweze kuelewa tabia ya Mungu haipingani na kazi Yangu. Kwani mkienda kinyume cha amri za kiutawala mara nyingi, basi ni nani kati yenu anayeweza kutoroka adhabu? Je, kazi Yangu haingekuwa bure kabisa? Kwa hivyo, Ningali Naomba kwamba pamoja na kuchunguza matendo yenu binafsi, kwamba muwe makini zaidi na hatua mnazochukua. Hili ndilo ombi kubwa zaidi ambalo Nitawaomba, na Ninatumai kwamba nyote mtalitilia maanani kwa umakinifu na kuliona kuwa muhimu. Endapo siku itawahi kufika ambapo matendo yenu yatanichochea Mimi hadi kuwa katika hali iliyojaa hasira, basi matokeo yatakuwa yenu pekee kufikiria, na hakuna mwingine yeyote atakayevumilia adhabu hiyo kwa niaba yenu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp