Wimbo wa Injili | Umuhimu wa Mungu Kumsimamia Binadamu

16/03/2020

Usimamizi wa Mungu ni kwa ajili

ya kupata kikundi cha watu ambao humwabudu Mungu na kujitoa kwake.

Hawa wanadamu wamepotoshwa na Shetani,

lakini hawamwoni Shetani kama baba yao:

hutambua uso usiopendeza wa Shetani,

na kuukataa, na kuja mbele Zake Mungu na kukubali hukumu na kuadibu Kwake.

Hujua kisichopendeza

na jinsi kinavyotofautiana na kile kilicho kitakatifu,

na hutambua ukubwa wa Mungu na uovu wa Shetani.

Wanadamu kama hawa hawatamfanyia Shetani kazi tena,

au kumwabudu Shetani, au kumsetiri Shetani.

Hii ni kwa sababu wao ni kikundi cha watu ambao wamemilikiwa na Mungu.

Huu ndio umuhimu wa Mungu kuwasimamia wanadamu.

Katika kazi ya usimamizi wa Mungu wa wakati huu,

wanadamu ndio chombo cha maovu ya Shetani,

na kwa wakati uo huo ni chombo cha ukombozi wa Mungu,

aidha ni sababu ya vita dhidi ya Mungu na Shetani.

Wakati sawia na wakati wa kutekeleza kazi Yake,

Mungu taratibu Humtoa mwanadamu kutoka mikononi mwa Shetani,

na hivyo mwanadamu anakuja karibu zaidi na Mungu …

na hivyo mwanadamu anakuja karibu zaidi na Mungu …

kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Kauli Maalum: Uzalishaji huu wa video ulitengenezwa kama mradi usio wa faida na Kanisa la Mwenyezi Mungu. Wahusika wanaoonekana katika uzalishaji huu wanafanya kwa msingi wa kutotafuta faida, na hawajalipwa kwa njia yoyote. Video hii isisambazwe kwa mtu mwingine kwa minajili ya faida, na ni matumaini yetu kwamba kila mtu atashiriki kuigawa na kuisambaza hadharani. Wakati unapoisambaza, tafadhali sisitiza chanzo chake. Bila ridhaa ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, hakuna shirika, kundi la kijamii, au mtu binafsi anayeweza kubadilisha au kuhudhurisha visivyo maudhui ya video hii.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp