Christian Testimony Video | Tiba ya Wivu (Swahili Subtitles)

02/11/2020

Mhusika mkuu anapokuwa akishirikiana na mfanyakazi mwenzake wa kanisa, anaona kwamba mfanyakazi mwenza ana uwezo zaidi kumliko na anaheshimiwa na ndugu wengine. Kwa sababu ya kuishi katika hali ya wivu, anahusika katika njama ndogondogo na anashindania sifa na faida. Ingawa kuishi kwa njia hiyo kunasikitisha sana, hawezi kabisa kuondokana nayo na hilo linamwacha akifadhaika sana. Lakini kwa kupitia hukumu na kuadibu kwa maneno ya Mwenyezi Mungu, anapata ufahamu kiasi juu ya asili yake ya kishetani yenye kiburi, ubinafsi na inayostahili dharau. Maneno ya Mungu pia yanampa njia ya kutatua wivu wake na kuacha tabia zake potovu. Anapoukana mwili wake na kutenda ukweli kama Mungu anavyoataka, anapata utulivu na amani moyoni na anakuwa na uwezo wa kuishi kwa kudhihirisha mfano wa binadamu.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp