Christian Testimony Video | Katikati ya Jaribu la Kifo (Swahili Subtitles)

21/10/2020

Mnamo 1991, Mwana wa Adamu mwenye mwili—Mwenyezi Mungu—alionyesha ukweli katika kanisa la nyumbani, akianzisha kazi ya hukumu akianza na nyumba ya Mungu. Watu wateule wa Mungu husoma manenoYake kila siku na kufurahia kazi ya Roho Mtakatifu. Wote wanaamini kuwa ni hitimisho la zamani kwamba watakuwa watu wa ufalme wa Mungu ambao hakika wataingia katika ufalme wa mbinguni wakati wa maisha yao. Kwa hivyo wanakimbia huku na kule kujitumia kwa shauku, na mhusika mkuu hajaachwa nyuma. Hata hivyo, wakiwa tu wamejawa na furaha ya kubarikiwa, Mwenyezi Mungu anaonyesha maneno akifunua jinsi Shetani amewapotosha wanadamu kwa kina, jinsi walivyojawa na tabia za kishetani kama vile kiburi, udanganyifu, ubinafsi na ulafi, na jinsi wanavyosema uwongo, kufanya dhambi, na kumpinga Mungu mara kwa mara. Maneno ya Mwenyezi Mungu yanasema kwamba ikiwa tabia za maisha ya watu hazitabadilika, watakabiliwa na kifo kwa hakika maafa makubwa yatakapokuja. Ndoto ya watu wateule wa Mungu ya kuingia katika ufalme wa mbinguni wakati wa maisha yao inavunjwa. Matumaini yao ya siku zijazo yanatoweka, mioyo yao imejaa uchungu, na hata wanafika kiwango cha kumlalamikia Mungu. Lakini baada ya kupitia hukumu na ufunuo wa maneno ya Mungu, wanakuwa na ufahamu kuhusu tamaa yao ya kupindukia ya baraka na kuingia katika ufalme wa mbinguni, na kuhusu fikira na mawazo yao. Wanaona kwamba tabia ya Mungu ni takatifu na yenye haki, na haitavumilia kosa lolote. Wanaona kwamba, kwa kuwa wamejawa na tabia za kishetani, hawastahili kuingia katika ufalme wa mbinguni. Wao kisha wanaweza kuachana na nia yao ya kupokea baraka, kutii utawala na mipango ya Mungu, na kuanza kulenga kufuatilia ukweli. Mwishowe, wanaona kwamba hukumu na majaribu ya Mungu ni kwa ajili ya kuwatakasa na kuwaokoa kabisa.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp