Swahili Christian Video | "Ni Vizuri Sana Kutupa Mbali Pingu za Hadhi" | Wokovu wa Mungu

10/06/2018

Baada ya Liang Zhi kumwamini Mungu, bila kukoma alitafuta kwa shauku, na kujitosa katika kutimiza wajibu wake. Baada ya miaka kadhaa, alichaguliwa kama kiongozi wa kanisa. Wakati alipokuwa akitekeleza wajibu wake kama kiongozi wa kanisa, aligundua kwamba baadhi ya ndugu walikuwa na uwezo zaidi kumliko, ambayo ilimfanya asiwe na furaha kwa kiasi kwamba alikuwa na wivu kwao. Ili kuokoa uso na kulinda hali yake, alishindana nao kwa siri ili kuona ni nani aliyekuwa bora, na alikimbilia umaarufu na hadhi. Umaarufu na hadhi vilionekana kama pingu zisizoonekana zilizomfunga sana, kumnyima uhuru, kumsababisha afanye mambo kinyume na ukweli na kupinga Mungu. Kwa sababu kutekeleza wajibu wake kulikuwa tu kwa ajili ya umaarufu na hadhi, na si kwa kufuatilia ukweli, matokeo yake ni kwamba alipoteza kazi ya Roho Mtakatifu. Hakuweza kufanya kazi ya vitendo, na aliondolewa kwenye kazi zake za uongozi na kubadilishwa. Aliteseka sana kama matokeo, na akaja mbele ya Mungu kutafakari juu yake mwenyewe. Baada ya kupitia hukumu na kuadibu kwa maneno ya Mungu, alikuja kutambua kwamba ufuatiliaji wa umaarufu na hadhi uliletwa kabisa na tabia yake ya kishetani ya kiburi na majivuno, na kuabudu mamlaka na ushawishi na hadhi. Alifahamu kuwa kiini cha kutafuta umaarufu na hadhi kilikuwa kufuata njia ya mpinga Kristo. Kama hangetubu na kurekebisha njia zake kote, matokeo ya mwisho yalikuwa kwamba alikusudiwa kuzama ndani ya utupu. Wakati huo huo aliona wazi kwamba imani katika Mungu ilihitaji kutembea kwenye njia ya ufuatiliaji wa ukweli na kutekeleza wajibu wake kwa kujitolea. Baada ya hapo, katika kutekeleza wajibu wake aliambatanisha umuhimu katika ufuatiliaji wa ukweli na kutenda ukweli. Kila wakati ambapo tabia potovu ya kukimbilia umaarufu na hadhi ilitokea, hapo basi alimwomba Mungu akitafuta ukweli na, akikubali hukumu na adabu ya maneno ya Mungu, kulingana na neno la Mungu alifanya mazoezi ya kuutelekeza mwili, na kuweka kwa mpangilio nia yake kutimiza wajibu wake mwenyewe. Bila kujali kama alikuwa na hadhi au la, aliweza kabisa kutekeleza majukumu yake. Pole pole alitupa mbali pingu za hadhi ambazo zilimfunga na hakufuatilia tena umaarufu na hadhi, baada ya kutembea kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu ya kutafuta ukweli na kupokea wokovu.

Baadhi ya taarifa katika video hii zinatoka kwa:

https://www.instagram.com/abenteuerschwarzwald/

https://www.facebook.com/abenteuerschwarzwald/?fref=ts

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp