Filamu za Kikristo | Mbona Dhiki Imewafika Mafarisayo Wanafiki? (Dondoo Teule)

12/04/2018

Imeandikwa katika Biblia kwamba Bwana Yesu aliwalaani Mafarisayo kwa dhiki saba. Siku hizi, njia inayotembelewa na wachungaji na wazee wa ulimwengu wa dini ni ile ya Mafarisayo na hali kadhalika wanapitia chuki ya Mungu na kukataliwa. Hivyo kwa nini Bwana Yesu aliwahukumu na kuwalaani Mafarisayo? Kimsingi ilikuwa kwa sababu walikuwa na kiini chenye unafiki ambacho kilimwasi Mungu, kwa sababu walitilia maanani kufanya matambiko ya dini na kufuata sheria tu, walieleza kanuni na mafundisho katika Biblia tu na hawakuweka maneno ya Mungu kwenye vitendo wala kufuata amri za Mungu kwa vyovyote, na hata waliacha amri za Mungu. Kila kitu walichofanya kilienda kinyume kabisa na mapenzi na mahitaji ya Mungu. Hiki kilikuwa kiini chenye unafiki cha Mafarisayo na ilikuwa sababu ya msingi ya Bwana Yesu kuwachukia na kuwalaani.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp