Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 423

22/10/2020

Ukweli ambao mwanadamu anahitaji kuwa nao unapatikana katika neno la Mungu, na ni ukweli wenye manufaa na usaidizi zaidi kwa wanadamu. Ni dawa na ruzuku ambayo miili yenu inahitaji, kitu kinachomsaidia mwanadamu kurejesha tena ubinadamu wake wa kawaida. Ni ukweli ambao mwanadamu anapaswa kujitayarisha nao. Kadiri mnavyotenda neno la Mungu, ndivyo maisha yenu yatakavyositawi haraka zaidi, na ndivyo ukweli utakavyokuwa dhahiri zaidi. Mnapozidi kukua katika kimo, mtaona vitu vya dunia ya kiroho kwa dhahiri zaidi, na ndivyo mtakavyokuwa na nguvu zaidi kumshinda Shetani. Ukweli mwingi ambao hamwelewi utafanywa kuwa dhahiri mtakapotenda neno la Mungu. Watu wengi wanaridhishwa kuelewa tu maandiko ya neno la Mungu na hawalengi kujitayarisha kwa mafundisho badala ya kuzidisha uzoefu wao kwa vitendo, lakini, je, hiyo si njia ya Mafarisayo? Kwa hivyo msemo “Neno la Mungu ni uzima” unawezaje kuwa wa kweli kwao? Maisha ya mtu hayawezi kukua kwa kusoma neno la Mungu tu, bali ni wakati tu neno la Mungu linawekwa katika vitendo. Ikiwa unaamini kwamba kuelewa neno la Mungu ndicho kitu pekee kinachohitajika kuwa na uzima na kimo, basi ufahamu wako umepotoka. Kuelewa neno la Mungu kwa kweli hutokea unapoweka ukweli katika vitendo, na ni lazima uelewe kwamba “ni kwa kutenda ukweli tu ndipo unaweza kueleweka.” Leo, baada ya kusoma neno la Mungu, unaweza tu kusema kwamba unajua neno la Mungu, lakini huwezi kusema kwamba unalielewa. Wengine husema kwamba njia ya pekee ya kutenda ukweli ni kuuelewa kwanza, lakini hii ni sahihi kwa kiwango fulani tu, na hakika si sahihi kikamilifu. Kabla uwe na maarifa ya ukweli fulani, hujapitia ukweli huo. Kuhisi kwamba unaelewa kitu unachosikia katika mahubiri si kuelewa kwa kweli—huku ni kuwa na maneno halisi ya ukweli tu, na si sawa na kuelewa maana ya kweli ndani yake. Kuwa tu na maarifa ya juujuu ya ukweli hakumaanishi kwamba kweli unauelewa ama una maarifa yoyote kuuhusu; maana ya kweli ya ukweli hutokana na kuupitia. Kwa hiyo, ni wakati tu unapopitia ukweli ndiyo unaweza kuuelewa, na ni hapo tu ndiyo unaweza kufahamu sehemu zake zilizofichika. Kukuza uzoefu wako ndiyo njia ya pekee ya kuelewa vidokezo, na kuelewa asili ya ukweli. Kwa hiyo, unaweza kuenda popote ukiwa na ukweli, lakini iwapo hakuna ukweli ndani yako, basi usifikirie kujaribu kuwashawishi hata wanafamilia wako sembuse watu wa kidini. Bila ukweli wewe ni kama vipande vidogo sana vya theluji vinavyopepea, lakini ukiwa na ukweli unaweza kuwa na furaha na uhuru, na hakuna anayeweza kukushambulia. Bila kujali jinsi nadharia fulani ilivyo thabiti, haiwezi kuushinda ukweli. Kukiwa na ukweli, dunia yenyewe haiwezi kuyumba na milima na bahari kusogezwa, wakati ukosefu wa ukweli unaweza kusababisha nyuta zenye nguvu za mji kuangushwa na mabuu. Huu ni ukweli dhahiri.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Punde Unapoelewa Ukweli, Unapaswa Kuuweka Katika Vitendo

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp