Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 530

12/09/2020

Leo, watu wengine wanatafuta kutumiwa na Mungu, lakini baada ya kushindwa hawawezi kutumika moja kwa moja. Kwa maneno yaliyonenwa leo, kama, wakati Mungu anapotumia watu, bado huwezi kuyakamilisha, basi hujafanywa mkamilifu. Kwa maneno mengine, kufika kwa mwisho wa wakati ambao mwanadamu anafanywa mkamilifu kutabaini iwapo mwanadamu atatupwa ama atatumiwa na Mungu. Wale walioshindwa ni mifano wa kutojihusisha na uhasi tu; ni sampuli na mifano, lakini si chochote ila ni ujazio wa wimbo. Ni wakati wanadamu wanapokuwa na uhai tu, tabia yake imebadilika, na amepata mabadiliko ndani na nje, ndipo atapokuwa amefanywa mkamilifu. Leo, ni nini utakacho, kushindwa ama kufanywa mkamilifu? Ni nini unachotamani kupata? Ni masharti mangapi ya kufanywa mkamilifu ambayo umeyatimiza? Ni yapi ambayo hujatimiza? Utajihami vipi, na utaweka mikakati ipi ili kuondoa upungufu wako? Utaingia vipi katika njia ya kufanywa mkamilifu? Utajiwasilisha vipi kikamilifu? Unataka kufanywa mkamilifu, je, unafuata utakatifu? Je, unafuata adabu na hukumu ili ulindwe na Mungu? Unatafuta kutakaswa, kwa hivyo una nia ya kukubali adabu na hukumu? Unataka kujua Mungu, lakini je, una maarifa ya adabu na hukumu Yake? Leo, kazi nyingi Anayofanya kwenu ni adabu na hukumu; ufahamu wako wa kazi hii ni upi, ambayo imetekelezwa juu yako? Je, adabu na hukumu ambayo umepitia imekutakasa? Imekubadilisha? Imekuwa na mabadiliko yoyote kwako? Umechoka na hii kazi ya leo—laana, hukumu na ufichuzi—ama unaona yakiwa ya manufaa kwako? Unapenda Mungu, lakini ni juu ya nini ndiyo unampenda? Je, unampenda Mungu kwa sababu umepokea neema kidogo, ama unapenda Mungu baada ya kupata amani na furaha? Ama unampenda Mungu baada ya kutakaswa na adabu na hukumu yake? Ni nini hasa kinachokufanya umpende Mungu? Ni masharti yapi ndiyo Petro alikamilisha ili afanywe mkamilifu? Baada ya kufanywa mkamilifu, ni njia gani muhimu ndiyo ilitumiwa kudhihirisha? Je, alimpenda Bwana Yesu kwa sababu alitamani kuwa na Yeye, ama kwa sababu hangemuona, ama ni kwa sababu alikuwa ameshutumiwa? Ama alimpenda Bwana Yesu zaidi kwa sababu alikubali mateso ya shida, na alikuwa amejua uchafu wake na kuasi, na alikuwa amepata kujua utakatifu wa Bwana? Je, mapenzi yake kwa Mungu yalikuwa safi kwa sababu ya adabu na hukumu ya Mungu, ama kwa sababu ya kitu kingine? Ni nini hasa? Unampenda Mungu kwa sababu ya neema ya Mungu, na kwa sababu leo amekupa baraka kidogo. Je, huu ni upendo wa ukweli? Unapaswa kumpenda Mungu vipi? Je, unapaswa kukubali adabu na hukumu Yake, na, baada ya kuona tabia Yake ya haki, uweze kumpenda kwa kweli, hivi kwamba umeshawishika kabisa, na kuwa na maarifa Yake? Kama Petro, unaweza kusema kwamba huwezi kumpenda Mungu vya kutosha? Je, unachofuata kishindwe baada ya adabu na hukumu, ama kutakaswa, kimelindwa na kushughulikiwa baada ya adabu na hukumu? Ni gani kati ya haya unayofuata? Je, maisha yako yana maana ama hayana maana wala dhamani? Unataka mwili ama ukweli? Unataka hukumu, ama faraja? Baada ya kupitia na kuiona kazi nyingi ya Mungu, na baada ya kuuona utakatifu na haki ya Mungu, unafaa kumfuata vipi? Unapaswa kutembea vipi katika njia hii? Utahitajika kuweka mapenzi ya Mungu katika matendo kivipi? Je, adabu na hukumu ya Mungu zimekuwa na athari yoyote kwako? Kama una maarifa ya adabu na hukumu ya Mungu itategemea jinsi unavyoishi kwa kudhihirisha, na kiwango gani unapenda Mungu! Kinywa chako kinasema unampenda Mungu, ilhali unachoishi kwa kudhihirisha ni tabia nzee, zilizo potovu; humchi Mungu, na zaidi ya yote huna dhamiri. Je, watu wa aina hii wanampenda Mungu? Je, watu wa aina hii ni waaminifu kwa Mungu? Je, wao ni wale wanaokubali adabu na hukumu ya Mungu? Unasema unampenda na kumwamini Mungu, ilhali huachi hisia zako. Katika kazi yako, kuingia kwako, maneno uzungumzayo, na katika maisha yako, hakuna udhihirisho wa mapenzi yako kwa Mungu, na hakuna heshima kwa Mungu. Je, huyu ni mtu ambaye amepata adabu na hukumu? Mtu kama huyu anaweza kuwa Petro? Wale walio kama Petro wana maarifa, lakini je, wanaishi kulingana nayo? Leo, ni hali gani inahitaji mwanadamu aishi kwa kudhihirisha maisha ya ukweli? Maombi ya Petro hayakuwa maneno matupu yaliyotoka mdomoni mwake? Hayakuwa maneno kutoka moyoni mwake? Petro aliomba tu, na hakuweka ukweli katika matendo? Kufuata kwako ni kwa niaba ya nani? Utajilinda aje na kutakaswa wakati wa adabu na hukumu ya Mungu? Je, adabu na hukumu ya Mungu haina faida yoyote kwa mwanadamu? Je, hukumu yote ni adhabu? Je, amani na furaha, baraka ya vitu vya dunia na faraja, ni muhimu kwa maisha ya mwanadamu? Mwanadamu akiishi katika mazingira mazuri ya raha, bila maisha ya hukumu, anaweza kutakaswa? Iwapo mwanadamu anataka kubadilika na kutakaswa, anafaa kukubali vipi kufanywa mkamilifu? Ni njia gani unayopaswa kuchagua leo?

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matukio Aliyopitia Petro: Ufahamu Wake wa Adabu na Hukumu

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp