Christian Testimony Video | Pingu za Umaarufu na Faida (Swahili Subtitles)

17/08/2020

Mhusika mkuu ni kiongozi wa kanisa, na hata ingawa ana shauku ya kujitumia kwa ajili ya Mungu, anadhibitiwa na tabia yake potovu ya kupigania umaarufu na faida. Yeye hujilinganisha na ndugu wengine kila mara anapofanya wajibu wake na hawajibikii kazi ya kanisa. Katika uchaguzi mmoja wa kanisa, hampigii kura ndugu ambaye ni bora kuliko yeye kimakusudi, kwa sababu tu ya wivu. Kupitia kuhukumiwa na kuadibiwa na maneno ya Mungu, anaona kwamba sifa na hadhi ni pingu tu za Shetani zisizoonekana ambazo humfunga mwanadamu, na kwamba kwa kufuatilia vitu hivyo, anachukua njia ya kumpinga Mungu. Anakuja kujichukia na kujutia matendo yake, na anaanza kuzingatia kufuatilia ukweli na anatekeleza wajibu wake vizuri. Na mwishowe, anaondokana na pingu za umaarufu na faida.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp