Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kujua Kazi ya Mungu | Dondoo 159

31/08/2020

Ni lazima myafahamu maono ya kazi ya Mungu na mpate mwelekeo wa kazi Yake. Huku ni kuingia kwa njia nzuri. Punde mnapong’amua ukweli wa maono kwa usahihi, kuingia wako utakuwa salama; bila kujali kazi Yake hubadilika kiasi gani, utaendelea kuwa imara moyoni mwako, utakuwa wazi kuhusu maono, na utakuwa na lengo la kuingia na kazi yako. Kwa njia hiyo, tajriba na ufahamu ulio ndani yako utakua kwa kina na kutakaswa zaidi. Punde unapong’amua ukweli wote, hutapoteza kitu maishani na hutapotea. Kama hutazijua hatua hizi za kazi, utapata hasara kwa kila mojawapo. Huwezi kugeuka baada ya siku chache tu na hutaweza kuipata njia mwafaka hata katika majuma machache. Je, si hili linakurudisha nyuma? Kuna zaidi katika kuingia kwa njia nzuri dhahiri na vitendo ambavyo mnapaswa kuving’amua, na vilevile unapaswa kuelewa mambo kadha katika maono ya kazi Yake kama vile umuhimu wa kazi Yake ya ushindi, njia ya kufanywa mkamilifu katika siku za usoni, kinachofaa kupatikana kupitia uzoefu wa majaribu na masaibu, umuhimu wa hukumu na kuadibu, kanuni za kazi ya Roho Mtakatifu, na kanuni za ukamilifu na ushindi. Huu wote ndio ukweli wa maono. Hayo mengine ni hatua tatu za kazi ya Enzi ya Sheria, Enzi ya Neema na Enzi ya Ufalme pamoja na ushuhuda wa baadaye. Huu pia ni ukweli kuhusiana na maono, na ni wa msingi na muhimu sana pia. Kwa sasa, kuna mengi sana mnayopaswa kujihusisha nayo na kutenda, na kwa sasa yana safu nyingi na maelezo ya kina. Kama huna ufahamu wa ukweli huu, ni thibitisho kwamba bado hujaingia. Mara nyingi, ufahamu wa mwanadamu kuhusu ukweli huwa wa juujuu; mwanadamu hushindwa kuweka ukweli wa kimsingi katika vitendo na hajui jinsi ya kushughulikia hata maswala madogo. Kwa sababu ya tabia yake ya uasi, mwanadamu hushindwa kutenda ukweli, na ufahamu wake kuhusu kazi ya sasa ni wa juu juu na wa kuegemea upande mmoja. Kwa hivyo, si kazi rahisi kwa mwanadamu kufanywa mkamilifu. Uasi wako ni wa hali ya juu, na unashikilia sana hali yako ya zamani; umeshindwa kusimama katika upande wa ukweli, na umeshindwa kutenda hata ukweli ulio wazi. Wanadamu kama hao ndio ambao hawawezi kukombolewa na ni wale ambao hawajashindwa. Ikiwa kuingia kwako hakuna kina au malengo, kukua kwako kutakujia polepole. Ikiwa kuingia kwako hakuna uhalisi hata kidogo, basi kazi yako itakuwa bure. Ikiwa hujui kiini cha ukweli, hutabadilishwa. Ukuaji katika maisha ya mwanadamu na mabadiliko katika tabia zake hupatikana kwa kuwa ndani ya ukweli na, zaidi ya hili, kwa kuwa katika tajriba ya kina. Ukiwa na tajriba pana katika wakati wa kuingia kwako, na ukiwa na ufahamu halisi kuhusu kuingia, tabia yako itabadilika haraka. Hata kama kwa sasa hujapata nuru katika vitendo, unafaa angalau uwe na nuru ya maono ya kazi. La sivyo utashindwa kuingia, na hutaweza kufanya hivyo isipokuwa uufahamu ukweli. Ni baada ya kuangaziwa nuru na Roho Mtakatifu katika tajriba yako ndipo utakapopata ufahamu wa kina kuhusu ukweli na uingie kwa kina. Ni sharti uifahamu kazi ya Mungu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Tofauti Kati ya Huduma ya Mungu Mwenye Mwili na Wajibu wa Mwanadamu

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp