Filamu za Injili “Hadithi Yangu, Hadithi Yetu” (Trela)

23/06/2023

Yang Yi, kiongozi wa kanisa, anakamatwa katika mojawapo ya kampeni za CCP za kuwakamata watu wengi na kuhukumiwa kifungo cha miaka kumi gerezani. Chini ya ufuatiliaji mkali na mahitaji ya kazi kama ya mtumwa ya walinzi wa magereza, anahisi mwenye huzuni na kuteswa, na anatamani ruzuku ya maneno ya Mungu. Siku moja, akina ndugu zake wanajihatarisha kumtembelea gerezani, na wanamletea kisiri nakala ya maneno ya Mungu. Yang Yi anaposoma maneno ya Mungu kwa hamu, anatiwa moyo sana, na anainuka kutoka katika maumivu na uhasi wake. Kadiri ukandamizaji na unyanyasaji wa CCP dhidi ya Wakristo unavyozidi kuwa mkali zaidi, ndugu zake zaidi wanafungwa pamoja naye. Yang Yi anaona kwamba baadhi yao ni wagonjwa na hasi kutokana na mateso wanayopitia, huku wengine wakilazimishwa na walinzi wa magereza kuandika “barua tatu” za kumkana Mungu, na kwa ajili ya hili, wanahisi majuto na kujilaumu. Baada ya kuona haya, Yang Yi anapata fursa za kuunga mkono na kuwasaidia akina ndugu zake, na anawapitishia maneno ya Mungu. Ndugu zake wanaposoma maneno ya Mungu, wanapata ruzuku ya kiroho, na wote wanahisi kwamba maneno ya Mungu ni yenye thamani sana, kwa hiyo wanaamua papo hapo kuandika vifungu vya maneno ya Mungu wanayokumbuka na kuyashiriki kati yao, jambo ambalo linawaruhusu akina ndugu wengi zaidi wasome maneno ya Mungu. Hata hivyo, kwa sababu ya uangalizi wa walinzi wa magereza na kuripoti kwa wapelelezi, ndugu za Yang Yi wanagunduliwa mfululizo kwamba wana maneno ya Mungu, na baada ya hapo wanawekwa chini ya usimamizi mkali sana na walinzi, wakikabiliwa na kuhojiwa na mateso. Kisha, msako mkubwa unafanywa katika kila eneo la gereza. Katikati ya hali hii ngumu, akina ndugu wanakabiliwa na jaribu kubwa la imani….

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp