Christian Dance | Sifa kwa Maisha Mapya katika Ufalme

13/04/2019

Tumesikia sauti ya Mungu na kurudi nyumbani Kwake.

Mikutanoni tunakula na kunywa maneno ya Mungu, tunahudhuria karamu.

Sisi tunaaga huzuni na vifungo vyetu, tunaishi maisha mapya.

Maneno ya Mungu yako nasi kila siku, tunastarehe ndani yake.

Tunapofungua mioyo yetu katika ushirika wa kweli, mioyo yetu inaangazwa sana.

Tunatafakari, kufikiri maneno ya Mungu, Roho Mtakatifu anatuangazia.

Tunaondolewa vizuizi na ubaguzi wetu, tunaishi ndani ya upendo wa Mungu.

Tunaelewa ukweli na kuwekwa huru, mioyo yetu ni tamu kama asali.

Tunapendana, hakuna umbali kati yetu.

Tunaelewa moyo wa Mungu, sisi si hasi tena.

Tukiishi ndani ya maneno ya Mungu, tunaona uzuri Wake.

Tumechukua njia ya nuru maishani, haya yote ni mwongozo wa Mungu.

Tunaimba kwa sauti sifa zetu kwa Mungu, tunacheza na kucheza.

Tunasifu maisha yetu mapya katika ufalme, mioyo yetu kweli ni ya furaha.

Ni Mungu aliyetuokoa, tumekuwa watu wa Mungu.

Kuinuliwa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu ni furaha isiyo na kifani.

Maneno ya Mungu ni yenye thamani sana, yote ni ukweli kabisa.

Tunapokubali hukumu ya maneno ya Mungu, upotovu wetu unafunuliwa kabisa.

Kwa tabia fidhuli, tunakosa mantiki kweli.

Maneno ya Mungu hutupogoa na kutushughulikia, tumekuja kujijua wenyewe.

Tunajitafakaria, kujielewa, na kuwa na toba ya kweli.

Kupitia hukumu na kuadibu, upotovu wetu unatakaswa.

Tunatupa tabia zetu potovu, tunakuwa wanadamu wapya.

Tunaweza kutekeleza wajibu wetu vizuri kulipa upendo wa Mungu.

Kila mmoja wetu anafanya sehemu yake, tunajitolea kwa Mungu.

Tunasimama imara katika ushuhuda kutimiza mapenzi ya Mungu.

Kila mmoja anatoa mwanga wake mwenyewe, mwali wake mwenyewe, kumtangaza na kumshuhudia Mungu.

Upendo safi na aminifu kwa Mungu ni wenye furaha na mtamu.

Tunaimba kwa sauti sifa zetu kwa Mungu, tunacheza na kucheza.

Tunasifu maisha yetu mapya katika ufalme, mioyo yetu kweli ni ya furaha.

Ni Mungu aliyetuokoa, tumekuwa watu wa Mungu.

Kuinuliwa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu ni furaha isiyo na kifani.

Sisi huunga mioyo na mikono kushuhudia kwa Mungu.

Tunaeneza injili ya ufalme, tusiogope kamwe ugumu au uchovu.

Katika mateso na majaribu, tunamwomba na kumtegemea Mungu.

Njia ni yenye mabonde na milima, lakini Mungu hufungua njia.

Tunapoelewa ukweli wa maneno ya Mungu, mioyo yetu hupata nguvu.

Maneno ya Mungu yanatuhimiza, tunazidi kwenda mbele milele.

Sako kwa bako, mkono kwa mkono tunamshuhudia Mungu, tunajitoa Kwake mwili na akili.

Haijalishi ukubwa wa mateso yetu, tuko tayari sana.

Kwa mwongozo wa maneno ya Mungu, tunamshinda Shetani.

Tunampenda Mungu kweli, hatutajua kamwe.

Tumeliacha kabisa joka kuu jekundu, sisi ni askari washindi.

Tunashuhudia katika njia yetu ya upendo kwa Mungu, hatutarudi nyuma kamwe.

Tunaimba kwa sauti sifa zetu kwa Mungu, tunacheza na kucheza.

Tunasifu maisha yetu mapya katika ufalme, mioyo yetu kweli ni ya furaha.

Ni Mungu aliyetuokoa, tumekuwa watu wa Mungu.

Kuinuliwa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu ni furaha isiyo na kifani.

Tunaimba kwa sauti sifa zetu kwa Mungu, tunacheza na kucheza.

Tunasifu maisha yetu mapya katika ufalme, mioyo yetu kweli ni ya furaha.

Ni Mungu aliyetuokoa, tumekuwa watu wa Mungu.

Kuinuliwa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu ni furaha isiyo na kifani.

kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp