Wimbo wa Injili | Mungu Atarudisha Maana ya Uumbaji Wake wa Mwanadamu

15/09/2020

Mungu aliumba binadamu na Akawaweka duniani,

ambao Amewaongoza mpaka siku ya leo.

Kisha Akaokoa binadamu

na kuhudumu kama sadaka ya dhambi kwa binadamu.

Mwishowe lazima bado ashinde binadamu,

aokoe binadamu kabisa na kuwarejesha kwa mfano wao wa awali.

Hii ndiyo kazi Amekuwa akifanya kutoka mwanzo hadi mwisho—

kurejesha mwanadamu kwa sura yake halisi na kwa mfano wake wa awali.

Ataanzisha ufalme Wake

na kurejesha mfano wa awali wa mwanadamu,

kurejesha mfano wa awali wa mwanadamu,

kumaanisha kwamba Atarejesha mamlaka Yake duniani

na kurejesha mamlaka Yake miongoni mwa viumbe vyote.

Mwanadamu alipoteza moyo wake wa kumcha Mungu baada ya kupotoshwa na Shetani

na kupoteza kazi ambayo kiumbe mmoja wa Mungu anapaswa kuwa nayo,

kuwa adui asiyemtii Mungu.

Mwanadamu alimilikiwa na Shetani

na kufuata amri za Shetani;

hivyo Mungu hakuwa na njia ya kufanya kazi miongoni mwa viumbe Wake,

na hakuweza zaidi kuwafanya viumbe Wake kumcha.

Mwanadamu aliumbwa na Mungu,

na anapaswa kumwabudu Mungu,

lakini mwanadamu kwa kweli alimpuuza Mungu na kumwabudu Shetani.

Shetani alikuwa sanamu katika moyo wa mwanadamu.

Hivyo Mungu alipoteza nafasi yake katika moyo wa mwanadamu,

kusema kwamba Alipoteza maana ya uumbaji Wake wa mwanadamu,

na ili kurejesha maana ya uumbaji Wake wa mwanadamu

lazima arejeshe mfano wa awali wa mwanadamu

na kumtoa mwanadamu tabia yake potovu.

Ili kumrejesha mwanadamu kutoka kwa Shetani,

lazima Amwokoe mwanadamu kutoka kwa dhambi.

Kwa njia hii tu ndiyo Anaweza kurejesha mfano wa awali wa mwanadamu polepole

na kurejesha kazi halisi ya mwanadamu,

na mwishowe kurejesha ufalme Wake.

Maangamizo ya mwisho ya wale wana wa uasi pia

yatafanywa ili kumruhusu mwanadamu kumwabudu Mungu vizuri zaidi

na kuishi duniani vizuri zaidi.

Ufalme Anaotaka kuanzisha ni ufalme Wake Mwenyewe.

Binadamu Anaotaka ni wale wanaomwabudu,

wale wanaomtii kabisa na wana utukufu Wake,

wana utukufu Wake.

kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp