Ushuhuda wa Kweli | Kushikilia Wajibu Wangu

01/08/2020

Mhusika mkuu wa video hii anadhibitiwa na sumu za kishetani kama vile “Kujipatia sifa na kuleta heshima kwa mababu zake” na “Man struggles upwards; water flows downwards,” na hasa anavutiwa sana na sifa na hadhi. Akiwa anahusika katika upigaji picha wa sinema wa maonyesho ya kwaya, anafanya bidii katika mazoezi ya filamu hiyo, akiteseka na kulipa gharama, yote haya ili aweze kuwa katika mstari wa mbele na ajionyeshe mbele ya kamera. Akiwa na shauku juu ya nafasi yake kwa kuwa mpangilio unabadilishwa mara kwa mara, anaishi katika minyororo inayotesa ya fahari na hadhi. Mwishowe, kupitia ufunuo na hukumu ya maneno ya Mungu, anapata ufahamu kiasi juu ya hatari na athari za tabia yake mwenyewe ya kishetani na ufuatiliaji wake wa umaarufu, faida, na hadhi. Anaanza kujuta na anaacha ufuatiliaji wa sifa na hadhi. Badala yake, analenga kufanya wajibu wake vizuri na kwa uthabiti, na kuimba kwa njia ya kupendeza ili kumsifu na kumshuhudia Mungu. Kwa kufanya hivyo, anaonjeshwa amani na furaha ya kutia ukweli katika vitendo.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp