Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Hatua Tatu za Kazi | Dondoo 31

21/10/2020

Siku za mwisho ni wakati ambao vitu vyote vitaainishwa kulingana na aina zake kupitia kushinda. Kushinda ni kazi ya siku za mwisho; kwa maneno mengine, kuhukumu dhambi za kila mtu ni kazi ya siku za mwisho. La sivyo, watu wangeainishwa vipi? Kazi ya kuainisha inayofanywa miongoni mwenu ni mwanzo wa kazi ya aina hiyo ulimwenguni kote. Baada ya hii, wale wa kila nchi na watu wote watapitia kazi ya ushindi. Hii inamaanisha kuwa watu wote wataainishwa kimakundi na kufika mbele ya kiti cha hukumu kuhukumiwa. Hakuna mtu na hakuna kitu kitakachoepuka kupitia huku kuadibu na hukumu, na hakuna mtu au kitu kinaweza kukwepa uainishaji huu; kila mtu atawekwa katika jamii. Hii ni kwa sababu mwisho u karibu kwa vitu vyote na mbingu zote na dunia zimefikia hatima yake. Mwanadamu anawezaje kukwepa hatima ya maisha yake? Hivyo, mnaweza kuendelea na matendo yenu ya uasi kwa muda gani zaidi? Je, hamuoni kwamba siku zenu za mwisho ziko karibu sana? Ni vipi ambavyo wale wanaomcha Mungu na kutamani sana Aonekane watakosa kuona siku ya kuonekana kwa haki ya Mungu? Wanawezaje kukosa kupokea thawabu ya mwisho ya wema? Je, wewe ni yule atendaye mema, au yule atendaye maovu? Je, wewe ni yule akubaliye hukumu yenye haki na kisha kutii, au kisha hulaaniwa? Umekuwa ukiishi katika nuru mbele ya kiti cha hukumu, au katika giza jahanamu? Je, wewe mwenyewe si unayejua kwa dhahiri sana kama mwisho wako utakuwa wa thawabu au wa adhabu? Je, wewe si unayejua kwa dhahiri sana na kufahamu kwa kina sana kwamba Mungu ni mwenye haki? Kwa hiyo, kweli, mwenendo wako uko vipi na una moyo wako wa aina gani? Ninapoendelea kukushinda leo, unanihitaji Mimi kwa kweli kukueleza kinagaubaga kama mwenendo wako ni wa uovu au wa mema? Je, umeacha kiasi gani kwa ajili Yangu? Unaniabudu Mimi kwa kina gani? Wewe mwenyewe unajua kwa dhahiri sana ulivyo Kwangu—je, hiyo si kweli? Unapaswa kujua vizuri zaidi kuliko mtu yeyote jinsi utakavyokuwa hatimaye! Kweli Nakwambia, Niliwaumba tu wanadamu, na Nilikuumba wewe, lakini Sikuwakabidhi kwa Shetani; wala kuwafanya kwa makusudi muasi dhidi Yangu au kunipinga Mimi na kwa hivyo kuadhibiwa na Mimi. Hamjapata majanga haya kwa sababu mioyo yenu imekuwa migumu mno na mienendo yenu yenye kustahili dharau mno? Kwa hiyo si kweli kwamba mnaweza kuamua hatima yenu wenyewe? Je, si kweli kwamba mnajua ndani ya mioyo yenu, bora zaidi kuliko yeyote, vile mtaishia? Sababu ya Mimi kuwashinda watu ni kuwafichua, na pia kuhakikisha bora zaidi wokovu wako. Sio kukusababisha ufanye uovu au kwa makusudi kukusababisha uingie katika jahanamu ya uharibifu. Wakati utakapofika, mateso yako yote makuu, kulia kwako na kusaga meno—je, hayo yote hayatakuwa kwa ajili ya dhambi zako? Kwa hiyo, uzuri wako mwenyewe au uovu wako mwenyewe sio hukumu bora zaidi kukuhusu? Je, sio thibitisho bora zaidi ya kile ambacho mwisho wako utakuwa?

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

The Final Stage of Conquest Is Meant to Save People

I

The final stage of conquering is to save people, reveal their endings, disclose their degeneration through judgment, thus help them repent and rise up, pursue life and the right path of human life. The final stage of conquering is to wake the hearts of numb people, show their rebelliousness through judgment, through judgment. If they still can’t repent, cast off corruptions, and pursue the right path of human life, they will become ones who can’t be saved but will be swallowed by Satan. The significance of conquering is to save people and show their endings, good or bad, saved or cursed, all is revealed by the conquering work.

II

The last days are when all things are classified by kind through conquering. It is the last days’ work to conquer man, to judge their sins. It classifies the people in the entire universe. The people of all nations will be subject to the conquering work, coming before the judgment seat. The significance of conquering is to save people and show their endings, good or bad, saved or cursed, all is revealed by the conquering work.

III

All created beings will be classified by kind. All will be judged before the judgment seat. No person, no thing can escape this judgment. No person, no thing can skirt this classifying by kind. All will be sorted because the end is near for all things. All the heavens, all the earth will arrive at their conclusion. The significance of conquering is to save people and show their endings, good or bad, saved or cursed, all is revealed, all is revealed, all is revealed by the conquering work.

from Follow the Lamb and Sing New Songs

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp