Mungu Aliwekea Mipaka Ndege na Wanyama Mbalimbali, Samaki, Wadudu, na Mimea yote

08/09/2019

Kwa sababu ya mipaka hii ambayo Mungu ameichora, mandhari mbalimbali yamezalisha mazingira tofautitofauti kwa ajili ya binadamu kuendelea kuishi, na mazingira haya kwa ajili ya kuendelea kuishi yamekuwa na hali isiyokuwa na usumbufu kwa ajili ya aina tofautitofauti ya ndege na wanyama na vilevile kuleta nafasi kwa ajili ya kuendelea kuishi. Kutokana na hili, mipaka kwa mazingira kwa ajili ya kuendelea kuishi kwa viumbe hai mbalimbali imeendelezwa. Hii ndiyo hoja ya pili tutakayokwenda kuzungumzia baadaye. Kwanza kabisa ni aina gani ya mazingira ambamo ndege na wanyama na wadudu wanaishi? Je, wanaishi katika misitu na vijisitu? Haya ndiyo makazi yao. Kwa hivyo, kando na kuanzisha mipaka kwa ajili ya mazingira mbalimbali ya kijiografia, Mungu pia Aliweka mipaka kwa ajili ya ndege na wanyama, samaki, wadudu mbalimbali, na mimea yote. Pia alianzisha sheria. Kwa sababu ya tofauti za mazingira mbalimbali ya kijiografia na kwa sababu ya uwepo wa mazingira tofauti ya kijiografia, aina tofautitofauti za ndege na wanyama, samaki, wadudu, na mimea vina mazingira tofauti kwa ajili ya kuendelea kuishi. Ndege na wanyama na wadudu wanaishi miongoni mwa mimea, samaki wanaishi majini, na mimea inakua kwenye nchi kavu. Nchi kavu inajumuisha maeneo mbalimbali kama vile milima, tambarare, na vilima. Punde tu ndege na wanyama wanapokuwa na makazi yao yasiyobadilika, hawataweza kuzungukazunguka wakielekea njia yeyote . Makazi yao ni misitu na milima. Ikiwa, siku moja makazi yao yataharibiwa, mpangilio utakuwa machafuko. Mara tu mpangilio huo unapokuwa machafuko, madhara yake ni yapi? Wa kwanza kuumizwa ni akina nani? (Binadamu.) Ni binadamu. Ndani ya sheria na mipaka hii ambayo Mungu ameianzisha, je, mmewahi kuona tukio lolote la ajabu? Kwa mfano, tembo wakitembea jangwani kwa kawaida. Mmewahi kuona tukio hilo? Kama ingekuwa hivyo, lingekuwa ni tukio la ajabu sana, kwa sababu tembo wanaishi msituni, na ni mazingira kwa ajili ya kuendelea kuishi ambayo Mungu aliwaandalia. Wana mazingira yao wenyewe kwa ajili ya kuendelea kuishi na wana makazi yao yasiyobadilika, sasa kwa nini watangetange? Je, kuna mtu yeyote ambaye amewahi kuona simba au duma wakitembea ufuoni? Hapana, hamjawahi. Makazi ya simba na duma ni msituni na kwenye milima. Je, kuna mtu yeyote ambaye amewahi kumwona nyangumi au papa wa bahari akiogelea kupitia jangwani? Hakuna ambaye ameona hayo, siyo? Nyangumi na papa makazi yao ni baharini. Katika mazingira ya kuishi ya binadamu, je, kuna watu ambao wanaishi pamoja na dubu wa kahawia? Je, kuna watu ambao siku zote wamezungukwa na tausi au ndege wengineo, ndani au nje ya makazi yao? Je, kuna yeyote ambaye amewahi kuwaona tai au bata bukini wa mwituni wakicheza na tumbili? (Hakuna.) Haya yatakuwa ni matukio ya pekee sana. Sababu Ninazungumza juu ya vitu hivi ambavyo vinaonekana kuwa vya kipekee masikioni mwenu ni kuwafanya muelewe kwamba vitu vyote vilivyoumbwa na Mungu—haijalishi kama vimewekwa katika sehemu moja au iwapo vinapumua kupitia mapuani—vina sheria zao kwa ajili ya kuendelea kuishi. Zamani kabla Mungu hajaumba viumbe hai hivi Alikuwa ameviandalia makazi yao, mazingira yao kwa ajili ya kuendelea kuishi. Viumbe hai hivi vilikuwa na mazingira yao yasiyobadilika kwa ajili ya kuendelea kuishi, chakula chao, makazi yao yasiyobadilika, sehemu zao zisizobadilika zinazowafaa kwa ajili ya kuendelea kuishi, maeneo yenye halijoto inayowafaa kwa ajili ya kuendelea kuishi. Kwa njia hiyo wasingezungukazunguka au kuhafifisha hali ya mwanadamu kuendelea kuishi au kuathiri maisha yao. Hivi ndivyo Mungu anavyoongoza vitu vyote, akiwaandalia wanadamu mazingira mazuri kabisa kwa ajili ya kuendelea kuishi. Viumbe hai chini ya vitu vyote kila kimoja kina chakula chao kinachokimu maisha yao wenyewe ndani ya mazingira yao wenyewe kwa ajili ya kuendelea kuishi. Kwa chakula hicho, vinajifunga katika mazingira yao ya asili kwa ajili ya kuendelea kuishi. Katika aina hiyo ya mazingira bado vinaendelea kuishi, kuzaliana, na kuendelea kulingana na sheria za Mungu alizozianzisha kwa ajili yao. Kwa sababu ya aina hizi za sheria, kwa sababu ya majaaliwa ya Mungu, vitu vyote vinaishi kwa upatanifu na wanadamu, na wanadamu huishi pamoja na vitu vyote kwa kutegemeana.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IX

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp