Katika ulimwengu wa kidini, ni ukweli na Mungu wanaoshikilia uwezo, au ni wapinga Kristo na Shetani wanaoshikilia uwezo?

24/09/2018

Aya za Biblia za Kurejelea:

“Lakini ole wenu nyinyi, waandishi na Mafarisayo, mlio wanafiki! Kwa maana mnafunga ufalme wa mbinguni wasiingie wanadamu: kwani ninyi hamwingii wenyewe, wala hamkubali wanaoingia ndani waingie” (Mathayo 23:13).

“Na Yesu akaingia katika hekalu la Mungu, naye akawaondoa wote waliokuwa wakiuza na kununua katika hekalu, naye akaziangusha meza za wabadilishaji wa fedha, na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa, Na akawaambia, imeandikwa, nyumba yangu itaitwa nyumba ya maombi; lakini mmeifanya pango la wezi” (Mathayo 21:12-13).

Maneno Husika ya Mungu:

Tazama tu viongozi wa kila madhehebu—wote ni wa kujigamba na kujidai, na wanafafanua Biblia nje ya muktadha na kulingana na ubunifu wao wenyewe. Wote wanategemea zawadi na maarifa kufanya kazi yao. Kama hawangekuwa na uwezo wa kuhubiri chochote, wale watu wangewafuata? Wao, hata hivyo, wanamiliki ufahamu fulani, na wanaweza kuhubiri kuhusu mafundisho fulani, au wanajua jinsi ya kuwashawishi wengine na jinsi ya kutumia ustadi kadhaa. Wanatumia haya kuwaleta watu mbele yao wenyewe na kuwadanganya. Kwa jina, watu hao humwamini Mungu, lakini katika uhalisi wanafuata viongozi wao. Wakikutana na mtu akihubiri njia ya kweli, baadhi yao husema, “Lazima tutafute ushauri kwa kiongozi wetu imani.” Imani yao lazima impitie mwanadamu; hilo si tatizo? Viongozi hao wamekuwa nini, basi? Hawajakuwa Mafarisayo, wachungaji waongo, wapinga Kristo, na vikwazo kwa kukubali kwa watu njia ya kweli?

kutoka katika “Ukimbizaji wa Ukweli Tu Ndiyo Imani ya Kweli katika Mungu” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Tumehubiri injili tena na tena kwa viongozi wengi katika jamii za dini, lakini bila kujali jinsi tunavyoshiriki ukweli na wao, wamekataa kuukubali. Kwa nini hivi? Ni kwa sababu majivuno yao yamekuwa tabia yao mbaya na Mungu hayuko tena mioyoni mwao! Watu wengine wanaweza kusema: “Watu walio chini ya uongozi wa baadhi ya wachungaji katika ulimwengu wa dini kweli wana msukumo mwingi. Inaonekana kwamba wana Mungu kati yao!” Haijalishi jinsi mahubiri ya wachungaji hao yanavyoweza kuwa makubwa, je, wanamjua Mungu? Kama kweli wangekuwa wanamcha Mungu mioyoni mwao, wangewafanya watu wawafuate na kuwatukuza? Je, wao wangewahodhi wengine? Je, wangethubutu kuwawekea vikwazo wengine wanaotafuta ukweli na kuchunguza njia ya kweli? Kama wanaamini kuwa kondoo wa Mungu kwa kweli ni wao na kwamba kondoo Wake wote wanapaswa wawasikilize, je, wao wenyewe hawatendi kama Mungu? Mtu wa aina hiyo ni mbaya hata zaidi kuliko Mafarisayo—yeye si mpinga Kristo? Kwa hiyo, asili yake ya majivuno inaweza kumdhibiti afanye mambo ambayo yanamsaliti Mungu.

kutoka katika “Asili yenye Majivuno ya Mwanadamu Ndiyo Chanzo cha Upinzani Wake kwa Mungu” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Wowote wasioelewa madhumuni ya kazi ya Mungu ni wale wanaompinga Mungu, na hata zaidi ya hayo ni wale waliofahamu madhumuni ya kazi ya Mungu lakini bado hawatafuti kumridhisha Mungu. Wale wanaosoma Biblia katika makanisa makubwa hukariri Biblia kila siku, lakini hakuna yeyote anayeelewa madhumuni ya kazi ya Mungu. Hakuna hata mmoja anayeweza kumwelewa Mungu; juu ya hayo, hakuna yeyote anayekubaliana na moyo wa Mungu. Wote hawana thamani, wanadamu waovu, kila mmoja akisimama juu kufundisha kuhusu Mungu. Ingawa wanalionyesha hadharani jina la Mungu, wanampinga kwa hiari. Ingawa wanajiita waumini wa Mungu, wao ni wale wanaokula mwili na kunywa damu ya mwanadamu. Wanadamu wote kama hao ni mashetani wanaoteketeza nafsi ya mwanadamu, pepo wakuu wanaowasumbua kimakusudi wanaojaribu kutembea katika njia iliyo sawa, na vizuizi vinavyozuia njia ya wanaomtafuta Mungu. Inagawa wao ni wenye “mwili imara,” wafuasi wao watajuaje kwamba wao ni wapinga Kristo wanaomwongoza mwanadamu katika upinzani kwa Mungu? Watajuaje kwamba hao ni mashetani hai wanaotafuta hasa nafsi za kuteketeza?

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Watu Wote Wasiomjua Mungu Ni Watu Wanaompinga Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp