Filamu za Injili | "Ivunje Laana" | Mungu ni Wokovu Wangu

23/02/2018

Fu Jinhua alikuwa mzee wa kanisa la nyumba nchini China. Kama Wakristo wengine wengi, alijitolea kwa Bwana kwa shauku kubwa, na alifanya kazi kwa bidii katika kazi yake kwa ajili Yake. Alikuwa hasa mwenye kujiamini, na alijiona kuwa mtu ambaye alimpenda Bwana kweli. Baada ya kumfuata Bwana kwa miaka mingi, aliamini kwa moyo wote kwamba Biblia ilikuwa imefunuliwa na Mungu, na kwamba maneno katika Biblia yote yalikuwa maneno ya Mungu. Kwa hivyo, akilini mwake, alilinganisha kuamini katika Bwana na kuamini katika Biblia. Alidhani kwamba wale walioachana na Biblia hawakuweza kuitwa wafuasi wa Bwana. Pia aliamini kwamba alihitaji tu kufuata Biblia ili kuchukuliwa kuenda katika ufalme wa mbinguni Bwana atakaposhuka na mawingu. Hivyo wakati ambapo kikundi cha watu kilianza kushuhudia kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho, Fu Jinhua aliamini katika dhana potovu za wachungaji na wazee wa kanisa wa kidini, na kamwe hakutafuta kuchunguza mambo zaidi. Siku moja, Fu Jinhua alimtembelea Dada He, mshiriki mwenza wa kanisa. Dada He alizungumza juu ya kiwewe chake mwenyewe: "Unabii wote juu ya kurudi kwa Bwana umetimia kimsingi, na Bwana anatakiwa kuwa amesharudi tayari. Hivyo kwa nini bado hatujamwona Bwana akishuka pamoja na mawingu?" Mfanyakazi mwenzake Fang Jianjie pia alisema: Miezi minne ya damu imeonekana, ambayo ina maana kwamba maafa makubwa yatatujia hivi karibuni. Kulingana na unabii kutoka katika vitabu vya manabii na Kitabu cha Ufunuo, Kanisa la Filadelfia litachukuliwa kwenda mbinguni kabla ya maafa makubwa, na Mungu atawastawisha watumishi na wajakazi Wake kwa Roho Wake ili kufanya kundi la washindi kabla ya maafa. Tusipochukuliwa kwenda mbinguni kabla ya majanga, huenda tutaangamia kati ya majanga haya makubwa. Lakini sasa, "Umeme wa Mashariki" limeshuhudia kwamba Bwana Yesu tayari amerejea, Ameonyesha ukweli, na kufanya kundi la washindi. Je, hili linatimiza unabii kutoka katika Biblia? Je, Umeme wa Mashariki ni onyesho la Bwana na kazi Yake? Baada ya kuwasikiliza wafanyakazi wenza, Fu Jinhua aliingia katika mawazo ya kina na akaanza kuyakadiria mambo haya …

Baadaye, Fu Jinhua na wafanyakazi wenza walikusanyika ili kutafuta majibu na kujadili juu ya jinsi ya kukaribisha kurudi kwa Bwana. Kwa kujifunza unabii wa Biblia, aligundua kwamba alikuwa ameshikilia tu unabii juu ya Bwana kushuka na mawingu, huku akipuuza kabisa unabii kuhusu jinsi Bwana angekuja kama mwivi na jinsi bikira wenye hekima wangemkaribisha bwana arusi. Wakati huo tu ndipo alitambua kwamba kurudi kwa Bwana katika siku za mwisho hakukuwa rahisi kama alivyofikiri kuwa, na kwamba kuna mafumbo yanayokuzunguka ambayo wanadamu hawawezi kuelewa. Aligundua kwamba ilikuwa ni makosa kwake kusikiza dhana potovu za wachungaji na viongozi wa kidini huku akikataa kutafuta na kuchunguza Umeme wa Mashariki kwa ajili yake mwenyewe. Na hivyo, Fu Jinhua aliamua kutafuta na kuchunguza kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho …

Baada ya kufanya ushirika na majadiliano na wahubiri kutoka katika Kanisa la Mwenyezi Mungu, Fu Jinhua hatimaye alielewa: Sisi waumini katika Mungu hatupaswi tu kushikilia Biblia na kumwekea Mungu mipaka kwa yaliyomo katika Biblia. Lazima tuweze kwenda zaidi ya Biblia. Lazima tujiweke huru kutoka kwa kufungwa na vikwazo vya wachungaji na viongozi wa ulimwengu wa dini. Tunapaswa kutafuta ukweli kwa kumcha Mungu na kuja kukubali na kutii kazi ya hukumu ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho. Wakati huo tu ndipo tunaweza kupata utakaso, wokovu, na kuingia katika ufalme wa mbinguni. Hatimaye, Fu Jinhua alijiweka huru kutokana na laana ambayo ilikuwa imemtia kwenye kifungo kwa miaka mingi, na hatimaye akakubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho. Kwa sababu ya hili, alichukuliwa kwenda mbinguni mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, na akahudhuria sikukuu ya harusi ya Mwana-Kondoo.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp