Ngoma ya Kikristo | Mungu Ameleta Utukufu Wake Mashariki | Ukaribisheni Urejeaji wa Bwana Yesu

24/01/2018

Mungu aliipa Israeli utukufu Wake kisha Akauhamisha mbali na pale,

na kuwaleta Waisraeli na kuwaleta watu wote Mashariki.

Mungu amewaelekeza wote kwenye mwanga

ili waweze kuungana tena na kuwa pamoja na mwanga,

wasilazimike kuutafuta tena, kuutafuta mwanga.

Mungu atawaacha wote wanaotafuta kuuona mwanga tena

na utukufu Aliokuwa nao katika Israeli,

kuona kwamba Mungu tayari ameshuka chini juu ya wingu jeupe miongoni mwa watu,

na kuona mawingu mengi meupe, na kuona vishada vya matunda,

kumwona Yehova Mungu wa Israeli, Mungu wa Israeli,

kumwona Mkuu wa Wayahudi, kumwona Masihi Aliyengojewa,

na kuonekana kamili kwa Yeye aliyeteswa na wafalme katika enzi zote.

Mungu atafanya kazi ya ulimwengu mzima na kufanya kazi kubwa,

akifichua utukufu Wake wote na matendo Yake yote kwa mwanadamu

katika siku za mwisho.

Mungu ataonyesha uso Wake uliojaa utukufu

kwa wale ambao wamemngoja Yeye kwa miaka mingi,

kwa wale ambao wametamani kumuona Yeye akija juu ya wingu jeupe,

kwa Israeli ambayo imemngoja Aonekane kwa mara nyingine tena,

kwa watu wote wanaomtesa Mungu.

Ili wote wajue kwamba Mungu kwa muda mrefu uliopita Ameuchukua utukufu Wake

na kuuleta katika Mashariki.

Hauko katika Uyahudi, kwa maana siku za mwisho tayari zimewadia!

kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Kauli Maalum: Uzalishaji huu wa video ulitengenezwa kama mradi usio wa faida na Kanisa la Mwenyezi Mungu. Wahusika wanaoonekana katika uzalishaji huu wanafanya kwa msingi wa kutotafuta faida, na hawajalipwa kwa njia yoyote. Video hii isisambazwe kwa mtu mwingine kwa minajili ya faida, na ni matumaini yetu kwamba kila mtu atashiriki kuigawa na kuisambaza hadharani. Wakati unapoisambaza, tafadhali sisitiza chanzo chake. Bila ridhaa ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, hakuna shirika, kundi la kijamii, au mtu binafsi anayeweza kubadilisha au kuhudhurisha visivyo maudhui ya video hii.

Baadhi ya taarifa katika video hii zinatoka kwa:

Hawk Sound (http://www.orangefreesounds.com/hawk-sound/) by thecluegeek /CC BY 3.0 (https://creativecommons.org/licenses/by/3.0/)

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp