Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kujua Kazi ya Mungu | Dondoo 210

23/09/2020

Siku za mwisho zimefika na nchi nyingi ulimwenguni ziko katika machafuko. Vurugu ya kisiasa, njaa, ndwele, mafuriko, na ukame unaonekana kila mahali. Kuna maangamizi katika ulimwengu wa mwanadamu; Mbingu pia imetuma msiba hapa chini. Hizi ni ishara za siku za mwisho. Lakini kwa watu, unaonekana kama ulimwengu wa uchangamfu na fahari, ambao unaendelea kuwa hivyo zaidi na zaidi. Mioyo ya watu yote inavutiwa nao, na watu wengi wananaswa na hawawezi kujinasua kutoka kwa ulimwengu; idadi kubwa itadanganywa na wale wanaoshiriki katika hila na uchawi. Usipojitahidi kuendelea mbele, huna maadili, na hujajikita mizizi katika njia ya kweli, utapeperushwa na mawimbi yavumayo ya dhambi. China ni nchi iliyo nyuma zaidi kimaendeleo kuliko zote; ni nchi ambapo joka kuu jekundu hulala likiwa limejiviringisha, ina watu wengi zaidi wanaoabudu sanamu na kushiriki katika uchawi, ina hekalu nyingi zaidi, na ni mahali ambapo pepo wachafu huishi. Ulizaliwa kutoka kwayo, umeelimishwa nayo na ukaloweshwa katika ushawishi wake; umepotoshwa na kuteswa nayo, lakini baada ya kugutushwa unaachana nayo na unapatwa kabisa na Mungu. Huu ni utukufu wa Mungu, na hii ndiyo maana hatua hii ya kazi ina umuhimu mkubwa. Mungu amefanya kazi ya kiwango kikubwa hivi, amenena maneno mengi sana, na hatimaye Atawapata ninyi kabisa—hii ni sehemu moja ya kazi ya usimamizi ya Mungu, na ninyi ndio “mateka wa ushindi” wa vita vya Mungu na Shetani. Kadiri mnavyozidi kuelewa ukweli na kadiri maisha yenu ya kanisa yalivyo bora zaidi, ndivyo joka kuu jekundu linavyotishwa zaidi. Haya yote ni mambo ya ulimwengu wa kiroho—ni vita vya ulimwengu wa kiroho, na Mungu anapokuwa mshindi, Shetani ataaibishwa na kuanguka chini. Hatua hii ya kazi ya Mungu ina umuhimu wa ajabu. Mungu anafanya kazi kwa kiwango kikubwa sana na kukiokoa kabisa kikundi hiki cha watu ili uweze kuponyoka kutoka kwa ushawishi wa Shetani, uishi katika nchi takatifu, uishi katika nuru ya Mungu, na uwe na uongozi na mwongozo wa nuru. Kisha kuna maana katika maisha yako. Mnachokula na kuvaa ni tofauti na wasioamini; mnafurahia maneno ya Mungu na kuishi maisha yenye maana—na wao hufurahia nini? Wao hufurahia tu “urithi wa babu” zao na “fahari yao ya kitaifa.” Hawana hata chembe ndogo kabisa ya ubinadamu! Mavazi, maneno, na matendo yenu yote ni tofauti na yao. Hatimaye, mtatoroka kabisa kutoka katika uchafu, msitegwe tena katika majaribu ya Shetani, na mpate riziki ya Mungu ya kila siku. Mnapaswa kila mara kuwa waangalifu. Ingawa mnaishi mahali pachafu hamjawekwa mawaa na uchafu na mnaweza kuishi ubavuni mwa Mungu, mkipokea ulinzi Wake mkuu. Mungu amewachagua kutoka miongoni mwa wote walio katika nchi hii ya manjano. Je, ninyi sio watu waliobarikiwa zaidi? Wewe ni kiumbe aliyeumbwa—unapaswa bila shaka kumwabudu Mungu na kufuatilia maisha yenye maana. Usipomwabudu Mungu lakini unaishi ndani ya mwili wako mchafu, basi wewe si mnyama tu aliye ndani ya vazi la mwanadamu? Kwa kuwa wewe ni binadamu, unapaswa kujitumia kwa ajili ya Mungu na kuvumilia kila mateso! Unapaswa kukubali kwa furaha na kwa hakika mateso kidogo unayopitia leo na kuishi maisha yenye maana, kama Ayubu na Petro. Katika ulimwengu huu, mwanadamu huvaa mavazi ya ibilisi, hula chakula kutoka kwa ibilisi, na hufanya kazi na kutumika chini ya uelekezi wa Shetani, na kukanyagiwa kabisa ndani ya uchafu wake. Usipoelewa maana ya maisha au kupata njia ya kweli, basi kuna umuhimu gani katika kuishi kwa namna hii? Ninyi ni watu mnaofuatilia njia sahihi, wale mnaotafuta maendeleo. Ninyi ni watu ambao huinuka katika nchi ya joka kuu jekundu, wale ambao Mungu huwaita wenye haki. Je, hayo si maisha yenye maana zaidi?

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Utendaji (2)

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp