Swahili Christian Movie "Kufungulia Moyo Minyororo" | Are We Really in Control of Our Own Fate?

10/08/2018

Chen Zhi alizaliwa katika familia iliyokuwa masikini. Shuleni, "Maarifa yanaweza kubadilisha majaliwa yako" na "Majaliwa ya mtu yako mikononi mwake" kama alivyofundishwa na shule ikawa wito wake. Aliamini kuwa almuradi angefanya kazi kwa bidii siku zote, angeweza kuwa bora kuliko wenzake, na kujipatia sifa na umaarufu. Baada ya kuhitimu kutoka chuo kikuu, Chen Zhi alipata kazi iliyolipa vizuri sana katika biashara ya nchi za nje. Hata hivyo, hakuridhika na hali aliyokuwa kwa wakati huo hata kidogo. Ili kutimiza njozi yake ya kuwa bora kuliko wengine, aliacha kazi yake na kuanzisha kampuni yake ya kuuza bidhaa. Lakini nyakati nzuri hazikudumu kwa muda mrefu. Kwa vile operesheni haikuendeshwa vizuri, wateja wakawa wachache, na biashara ya kampuni hiyo ikapungua. Hatimaye, kampuni haikuweza kuendelea kufanya kazi. Baada ya kampuni hiyo kufilisika, Chen Zhi hakuwa na nia ya kukubali kushindwa hata kidogo. Aliamini kwamba kwa kutegemea akili na uwezo wake, alimuradi angevumilia angeweza kurudi. Baadaye, Chen Zhi alianzisha tovuti ya mauzo ya mtandaoni na kuanzisha biashara kwenye Mtandao. Baada ya kujishughulisha kwa miaka kadhaa, hakufaulu bado. Chen Zhi akatumbukia katika lindi kuu la huzuni kubwa na kutojiweza ...

Mnamo mwaka wa 2016, familia ya Chen Zhi ilienda Marekani kuishi. Kwa msaada wa mkewe, alikubali kazi ya siku za mwisho za Mwenyezi Mungu. Kupitia kusoma maneno ya Mungu, Chen Zhi hatimaye alielewa kwamba Mungu anadhibiti majaliwa ya wanadamu, na kwamba mtu hawezi kabisa kubadili hatima yake mwenyewe kutegemea uwezo wake mwenyewe. Alijua pia chanzo cha dhiki ya mwanadamu maishani mwake, na jinsi Shetani amewapotosha wanadamu. Alijua kwamba ikiwa mtu ataishi maisha yenye maana, basi lazima aje mbele za Mungu, akubali hukumu na kuadibu kwa maneno ya Mungu ili kupata utakaso, na kuishi kwa kutegemea maneno ya Mungu, na ni hapo tu ndio atapata sifa ya Mungu . Chen Zhi alielewa ukweli fulani katika maneno ya Mwenyezi Mungu, akaanzisha mtazamo sahihi juu ya maisha, alimwaminia Mungu maisha yake yote, akatii udhibiti wa Mungu na mipangilio Yake, na hatimaye kujiondoa jozi katika nafsi yake ya "Majaliwa ya mtu yako mikononi mwake, "na kupata ufunguliwaji na uhuru. Kutoka wakati huo kuendelea alitembea kwenye njia angavu na sahihi ya maisha.

Baadhi ya taarifa katika video hii zinatoka kwa: www.stockfootage.com

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp