Filamu za Kikristo | Nani Atanyakuliwa Kwanza Wakati Bwana Atakaporudi? (Dondoo Teule)

27/08/2018

Wengi wa wale wanaomsadiki Bwana wanasadiki kwamba mradi tu wajitolee, wajitumie, na kutia bidii, bila shaka watakuwa miongoni mwa wale wa kwanza kunyakuliwa. Lakini je, kuna msingi wowote wa haya katika maneno ya Bwana? Bwana Yesu alisema, "But many that are first shall be last; and the last shall be first" (Mathayo 19:30). "Kondoo wangu huisikia sauti yangu" (Yohana 10:27). Ni wazi kwamba kama mtu anaweza kunyakuliwa au la kunaamuliwa na kama ataisikia sauti ya Bwana. Wale wanaoisikia kwanza sauti Yake na kukubali kuonekana Kwake na kazi ni wanawali wenye hekima, na watakuwa wa kwanza kunyakuliwa.

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Kauli Maalum: Uzalishaji huu wa video ulitengenezwa kama mradi usio wa faida na Kanisa la Mwenyezi Mungu. Wahusika wanaoonekana katika uzalishaji huu wanafanya kwa msingi wa kutotafuta faida, na hawajalipwa kwa njia yoyote. Video hii isisambazwe kwa mtu mwingine kwa minajili ya faida, na ni matumaini yetu kwamba kila mtu atashiriki kuigawa na kuisambaza hadharani. Wakati unapoisambaza, tafadhali sisitiza chanzo chake. Bila ridhaa ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, hakuna shirika, kundi la kijamii, au mtu binafsi anayeweza kubadilisha au kuhudhurisha visivyo maudhui ya video hii.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp