Filamu za Kikristo "Ni Nani Anayemsulubisha Mungu Tena"

03/08/2018

Go Shoucheng ni mchungaji katika kanisa la nyumbani huko China. Amemwamini Bwana kwa miaka mingi, na amekuwa akishughulikia kwa mahubiri yake kwa uthabiti, na amekuwa kila mahali akihuburu injili. Amekamatwa na kutiwa jelani kwa sababu ya kuhubiri injili, na kukaa miaka kumi na miwili gerezani. Baada ya kuondoka gerezani, Gu Shoucheng aliendelea kufanya kazi kanisani. Hata hivyo, wakati ambapo injili ya Mwenyezi Mungu ya ufalme ililijia kanisa alimo kuwa Gu Shoucheng, hatafuti wala kuichunguza hata kidogo, lakini kwa ukaidi anategemea dhana na mawazo yake mwenyewe kushutumu kazi ya Mungu katika siku za mwisho, na anafanya lote awezalo kueneza mawazo na uongo ili kukatiza na kuzuia waumini dhidi ya kukubali njia ya kweli. Ilikuwa hasa baada ya kusoma maneno ya Mwenyezi Mungu ambapo Gu Shoucheng aligundua kwamba kwa kweli yalikuwa na mamlaka na nguvu na kwamba yeyote aliyeyasikia angeridhika, na akawa na hofu kubwa kwamba yeyote katika kanisa aliyesoma maneno ya Mwenyezi Mungu angemwamini Yeye. Aliogopa kwamba wakati huo hadhi na riziki yake havingeendelezwa. Hivyo, alijadiliana hili na Mzee Wang Sen na wengine katika kanisa na kuamua kuwadanganya watu kwa uvumi uliotumiwa na Serikali ya Komunisti ya China kushambulia na kumshutumu Mwenyezi Mungu. Gu Shoucheng na Wang Sen wanafanya wawezalo kuzingia kanisa na kuzuia watu dhidi ya kukubali njia ya kweli, na hata wanashirikiana na utawala wa kishetani wa CCP kukamata na kutesa wale wanaomshuhudia Mwenyezi Mungu. Matendo yao yanakosea tabia ya Mungu vikali na wanapata laana Yake. Wang Sen akiwa njiani kukamata baadhi ya watu wanaoeneza injili ya ufalme, anapatwa na ajali ya gari na kufa papo hapo. Gu Shoucheng anaishi katika woga na hali ya kukata tamaa na anapatwa na hofu. Anajiambia mara kwa mara: "Je, shutuma yangu kwa Mwenyezi Mungu ni kumsulubisha Mungu tena?"

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp