639 Umuhimu Mkubwa wa Mungu Kuwachagua Watu Hawa

1 Kama mtu binafsi katika mkondo huu, kila mtu anapaswa kujua lengo la mpango mzima wa usimamizi wa Mungu ni nini, ukweli ambao Mungu tayari ametimiza, kwa nini Amelichagua kundi hili la watu, malengo na umuhimu wa Yeye kuwachagua ni upi, na kile ambacho Anataka kufanikisha katika kundi hili. Mungu kuweza kuliinua kundi kama hilo la watu wasiofika katika nchi ya joka kubwa jekundu na kuweza kuendelea kufanya kazi hadi sasa, Akijaribu na kuwakamilisha kwa kila namna, Akizungumza maneno yasiyohesabika, Akitekeleza kazi kubwa na kutuma vitu vingi vya kuhudumu—kwa Mungu pekee kuweza kukamilisha kazi kubwa kama hiyo inaonyesha jinsi kazi Yake ilivyo muhimu. Kwa sasa, huna uwezo wa kuelewa hili kikamilifu.

2 Hivyo, ni sharti msiichukulie kazi ambayo Mungu amefanya ndani yenu kama jambo dogo; hili si jambo dogo. Hata kile ambacho Mungu amewafichulia leo kinawatosha kujaribu kutafakari na kujua. Mkielewa tu kwa kweli na kwa kina ndipo matukio yenu yatakuwa ya kina na maisha yenu yatakua. Leo, watu wanaelewa na kufanya kidogo sana; hawana uwezo wa kutimiza makusudi ya Mungu kikamilifu. Huu ni upungufu wa wanadamu na kushindwa kwao kutimiza wajibu wao, hivyo, hawawezi kutimiza matokeo yanayotarajiwa.

Umetoholewa kutoka katika “Sisitiza Uhalisi Zaidi” katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 638 Nini Kitafanyika Ukitoroka Hukumu ya Mungu?

Inayofuata: 640 Umefurahia Baraka Kuu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp