967 Kiini cha Mungu ni kitakatifu

1 Hakuna udanganyifu ndani ya Mungu, hakuna uongo. Mungu ni mwaminifu na kila kitu Anachofanya ni halisi. Ni Yeye pekee ambaye watu wanaweza kutegemea na Mungu ambaye watu wanaweza kuaminia maisha yao na yote wanayo Kwake. Hii ni kwa sababu mwanadamu hawezi kuona chembe cha tabia potovu ya Shetani kwa Mungu. Yote ambayo Mungu hufanya na kufichua ni muhimu sana na ya msaada sana kwa mwanadamu, yanafanywa kumkimu mwanadamu kabisa, yamejaa uhai na yanampa mwanadamu njia ya kufuata na mwelekeo wa kuchukua. Kwa sababu Mungu hana upotovu wowote wa mwanadamu na hana chochote sawa na, au kinachofanana na tabia potovu ya mwanadamu ama kiini cha Shetani, kutoka mtazamo huu tunaweza kusema kwamba Mungu ni mtakatifu.

2 Mungu hafichui upotovu wowote, na ufunuo wa kiini Chake katika kazi Yake yote ni thibitisho tunalohitaji kwamba Mungu Mwenyewe ni mtakatifu. 1) Hakuna tabia potovu ndani ya Mungu; 2) kiini cha kazi ya Mungu kwa mwanadamu kinamruhusu mwanadamu kuona kiini cha Mungu mwenyewe na kiini hiki ni kizuri kabisa. Kwa kuwa vitu ambavyo kila namna ya kazi ya Mungu inamletea mwanadamu ni vitu vizuri. Na matokeo ya haya yote ni kwamba mwanadamu hadanganywi tena na Shetani, haendelei kudhuriwa na Shetani ama kudhibitiwa na yeye. Kwa maneno mengine, yanawaruhusu watu kujinusurisha kabisa kutoka upotovu wa Shetani, na hivyo kutembea polepole njia ya kumcha Mungu na kuepuka maovu.

Umetoholewa kutoka katika “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VI” katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 966 Mungu ni Mwenye Haki kwa Kila Mtu

Inayofuata: 968 Tabia ya Mungu ni Takatifu na Bila Dosari

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp