606 Mungu Hutumia Asili ya Mwanadamu Kumpima

1 Mwanadamu anapowapima wengine, ni kwa mujibu wa michango yao. Mungu anapompima mwanadamu, ni kwa mujibu wa asili yake. Miongoni mwa wale ambao hutafuta uzima, Paulo alikuwa mtu ambaye hakujua kiini chake mwenyewe. Hakuwa kwa njia yoyote mnyenyekevu ama mtiifu, wala kujua kiini chake, ambacho kilikinzana na Mungu. Na kwa hivyo, alikuwa mtu ambaye hakuwa amepitia matukio ya kina, na alikuwa mtu ambaye hakuweka ukweli katika vitendo. Petro alikuwa tofauti. Yeye alijua kutokamilika kwake, udhaifu, na tabia yake potovu kama kiumbe wa Mungu, na hivyo alikuwa na njia ya vitendo ambayo angebadilishia tabia yake; hakuwa mmoja wa wale ambao walikuwa tu na mafundisho ya kidini lakini hawakuwa na uhalisi.

2 Wale ambao hubadilika ni watu wapya ambao wameokolewa, ni wale ambao wana sifa zinazostahili katika kufuatilia ukweli. Watu ambao hawabadiliki ni wa wale ambao hawafai kwa sasa kiasili; ni wale ambao hawajaokolewa, yaani, ni wale ambao wamechukiwa na kukataliwa na Mungu. Hawatakumbukwa na Mungu bila kujali jinsi kazi zao ni kubwa. Kama bado hakuna ukweli kwa yale unayotafuta, na kama hata leo bado wewe ni mwenye kiburi na jeuri kama Paulo, na bado wewe ni mwepesi wa kusema maneno matupu na mwenye kujisifu kama yeye, basi bila shaka wewe ni aliyeharibika tabia na ambaye hushindwa. Kama wewe hutafuta jinsi sawa na Petro, kama unatafuta vitendo na mabadiliko ya kweli, na usiwe mwenye kiburi au mkaidi, bali utafute kutekeleza majukumu yako, basi utakuwa kiumbe wa Mungu ambaye anaweza kufikia ushindi.

Umetoholewa kutoka katika “Mafanikio au Kushindwa Kunategemea Njia Ambayo Mwanadamu Hutembea” katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 605 Kupatwa na Mungu Kunategemea Ufuatiliaji Wako Mwenyewe

Inayofuata: 607 Kiwango cha Chini Zaidi cha Kuwa Mtu Anayemtumikia Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp