Utangulizi Mfupi Kuhusu Usuli wa Kuonekana kwa Kazi ya Kristo wa Siku za Mwisho Nchini China

09/06/2017

China ni nchi ambamo joka kubwa jekundu hukaa, na ni mahali ambapo pamempinga na kumshutumu Mungu zaidi sana katika historia. China ni kama ngome ya mapepo na gereza linalodhibitiwa na shetani, lisilopenyeka na lisiloingilika. Zaidi ya hayo, utawala wa joka kubwa jekundu husimama ukilinda katika ngazi zote na umeanzisha ulinzi katika kila kaya. Matokeo yake, hakuna mahali pagumu zaidi ya hapa kueneza injili ya Mungu na kufanya kazi ya Mungu. Wakati Chama cha Kikomunisti Cha China kiliposhika madaraka mwaka wa 1949, imani za kidini katika China bara zilizimwa kabisa na kupigwa marufuku. Mamilioni ya Wakristo walipitia mateso na fedheha hadharani, na kifungo. Makanisa yote yalifungwa kabisa na kufutiliwa mbali. Hata mikutano ya nyumbani ilipigwa marufuku. Iwapo mtu yeyote alibambwa akishiriki mkutano, angetiwa gerezani na hata angekatwa kichwa. Wakati huo, shughuli za kidini karibu zitoweke bila kupatikana. Ni idadi ndogo tu ya Wakristo iliendelea kuamini katika Mungu, lakini wangeweza tu kumwomba Mungu kimyakimya na kuimba nyimbo za sifa kwa Mungu katika mioyo yao, wakimwomba Mungu kufufua kanisa. Hatimaye, katika mwaka wa 1981, kanisa lilifufuka kwa dhati, na Roho Mtakatifu akaanza kazi kwa kiasi kikubwa katika China. Makanisa yakachipuka kama machipukizi ya mianzi baada ya mvua ya majira ya kuchipua, na watu zaidi na zaidi wakaanza kuamini katika Mungu. Katika mwaka wa 1983, wakati uamshaji wa kanisa ulifika kilele chake, Chama cha Kikomunisti Cha China kikaanza duru mpya ya ukandamizaji wa kikatili. Mamilioni ya watu walikamatwa, wakawekwa kizuizini, na kuelimishwa kwa njia ya kazi. Utawala wa joka kubwa jekundu uliwaruhusu waumini katika Mungu kujiunga tu na Kanisa la Nafsi Tatu la Kizalendo (Three-Self Patriotic Church) lililoanzishwa na serikali. Serikali ya Chama cha Kikomunisti Cha China (CCP) lilianzisha Kanisa la Nafsi Tatu la Kizalendo (Three-Self Patriotic Church) katika jaribio la kuzima kanisa la siri la nyumbani na kuwaleta wale waumini wa Bwana imara chini ya utawala wa serikali. Iliamini kwamba hii ilikuwa njia pekee ya kufikia lengo lake la kupiga marufuku imani na kugeuza China kuwa nchi isiyokuwa na Mungu. Lakini Roho Mtakatifu aliendelea kufanya kazi nyingi katika kanisa la nyumbani na katika wale ambao kweli waliamini katika Mungu, ambao serikali ya CCP ilishindwa kuwakomesha. Wakati huo, katika kanisa la nyumbani ambapo Roho Mtakatifu alifanya kazi, Kristo wa siku za mwisho kwa siri Alionekana Akifanya kazi, na kuanza kuonyesha ukweli na kufanya kazi ya hukumu Akianza na nyumba ya Mungu.

Katika mwanzo wa Februari 1991, mtu fulani katika kanisa alionekana kupokea nuru ya Roho Mtakatifu, na akaanza kunena, akiwashuhudia jina la Mungu na ujio wa Mungu. Maneno haya yalitumwa kwa makanisa, na baada ya kuyasoma, kila mtu alipatwa na msisimko sana, wote walifurahi mno, na kuamini kwamba hii hakika ilikuwa kupata nuru na maneno ya Roho Mtakatifu. Kuanzia hapo kuendelea, Kristo alianza kuongea. Wakati mwingine Kristo alinena kifungu kimoja kwa siku, wakati mwingine kimoja kila baada ya siku mbili, na matamshi yakawa zaidi na zaidi na mara kwa mara zaidi. Kila mtu aliyapitisha kwa mwenzake na kuhisi msisimko zaidi, mikutano ilijaa furaha, na kila mtu alikuwa amezama katika furaha. Kristo alipoonyesha maneno zaidi na zaidi, watu wote walisikiza kwa makini na kufurahia maneno ya Mungu, na mioyo yao ilinatwa kabisa na maneno ya Mungu. Na hivyo, wakati wa mabaraza, walianza rasmi kufurahia maneno ya sasa ya Roho Mtakatifu. Wakati huo, watu walikuwa bado hawajatambua kwamba Mungu alikuwa mwili tayari na huku kulikuwa ni kuonekana kwa Kristo. Wao walichukulia tu maonyesho ya Kristo kama nuru ya Roho Mtakatifu iliyopokewa na mtu wa kawaida, kwa sababu katika maonyesho ya Kristo, Yeye hakuwa Amethibitisha rasmi kupata mwili kwa Mungu. Hakuna yeyote aliyeelewa kupata mwili kulikuwa ni nini hasa, na walijua tu kuwa maneno haya yalikuwa nuru ya Roho Mtakatifu. Kwa hiyo, walikuwa bado wanamchukulia Kristo kama mtu wa kawaida. Ni wakati tu maneno ya Kristo yalipofikia upeo ambapo Mungu alianza kuthibitisha kwa Mungu kupata mwili, akielezea tofauti kati ya kushuka kwa Roho Mtakatifu kwa mtu na kazi ya Roho Mtakatifu ndani ya mtu na kufichua fumbo la utambuzi wa Roho katika mwili. Ni baada ya hayo tu ndipo watu walijua kwamba huyu mtu wa kawaida Aliyeishi kati yao na kuonyesha maneno ya kuchunga na kukimu makanisa alikuwa Mungu kupata mwili, Kristo, na Mungu ambaye Alionekana. Baada ya kutambua haya, wote walichukia jinsi walivyokuwa vipofu, wajinga, na wasiojua, na wakasujudu wenyewe mbele ya Kristo, wakilia na kutubu, kama mioyo yao imevunjwa na huzuni kubwa, mayowe yao yalisikika kila mahali. Wakati huo, mioyo ya watu ilikuwa imejawa na shaka za huzuni na furaha, ambazo hazingeelezeka. Walipomwona Kristo, walijua tu kusujudu juu ya ardhi; kama hawakufanya hivyo, hawakuwa na raha ndani ya mioyo yao. Wakati wakisujudu mbele ya Kristo, walikuwa na furaha na walihisi kuwa walikuwa kweli wamerudi mbele ya Mungu na walikuwa ndio waliokuwa miliki ya Mungu. Baada ya Kristo kuonekana, Alionyesha maneno zaidi na zaidi, hatua kwa hatua Akiingia katika njia sahihi ya kazi ya Mungu na kuashiria hukumu ikianza na nyumba ya Mungu. Maneno ya Mungu yaliwashinda watu kabisa. Kwa njia ya Kristo kutoa taarifa ya maana ya jina la Mungu, jina la Mwenyezi Mungu likawa na uwepo. Hivyo watu waliomba moja kwa moja kwa jina la Mwenyezi Mungu, na wakati wa mabaraza wao walifurahia maneno ya Mwenyezi Mungu. Hii ni kwa sababu maneno haya (yaani, maneno yote katika Neno Lonekana katika Mwili) ni kazi ya Mungu ya sasa, maneno ya Mungu katika enzi mpya, na haja ya watu ya sasa. Kwa kuwa kulikuwa na kazi mpya ya Mungu na maneno, kwa kawaida Biblia ikawa imepitwa na wakati, na kwa kawaida hakuna mtu aliyetilia maanani umuhimu wowote kwa misemo mbalimbali na nadharia za Enzi ya Neema. Wote walishindwa na maneno ya sasa ya Mungu, kama kwamba walikuwa wameona mbingu ikiwa wazi. Hii ni kwa sababu Mungu alifichua aina zote za mafumbo, macho ya watu yalifunguliwa, na waliona kwamba mingi ya misemo ambayo watu hapo awali walikuwa wameshikilia wakati wa Enzi ya Neema ilikuwa dhana, na ilikuwa na michepuko na mambo yenye makosa. Kwa sababu ya kuonekana kwa Mungu, watu walipitia njia sahihi wakiamini katika Mungu. Ni baada tu ya watu kushindwa na maneno ya Mungu ndipo waligundua kuwa huyu mtu wa kawaida na wa siku zote ambaye aliyaonyesha maneno ya Mungu alikuwa Kristo, na mwili wa Mungu kuwa mwili.

Kristo alizaliwa katika familia ya kawaida kaskazini mwa China. Kutoka utotoni, Alikuwa ameamini katika Mungu kwa moyo wake wote. Yeye alikua hatua kwa hatua kama mtu wa kawaida afanyavyo. Mwaka wa 1989, wakati ule ule Roho Mtakatifu alipokuwa akifanya kazi kwa kiasi kikubwa katika kanisa la nyumbani, Kristo aliacha masomo yake na akaingia rasmi katika kanisa la nyumbani. Wakati huo, Kristo alikuwa na ari katika moyo Wake na Alitamani kumtumikia Mungu na kufanya wajibu wake. Miaka miwili baadaye, Kristo alianza kuonyesha maneno, kuyaandika chini maneno katika moyo Wake na kuyatoa kwa makanisa. Baadaye, Kristo alipoonyesha ukweli zaidi na zaidi, watu walivutiwa na maneno ya Kristo, na wakawa na shauku ya kusoma yale Aliyokuwa Ameyaonyesha. Hasa, maneno Yake ambayo yalifichua na kuihukumu dutu ya asili ya wanadamu wapotovu, na tabia ya kishetani ya watu wapotovu, iliichoma mioyo ya watu kama upanga wenye makali kuwili. Hapo ndipo tu waliposhindwa kabisa na maneno ya Mungu, na wakapiga magoti mbele ya Mungu, hapo tu ndipo Kristo alipokubaliwa, kujulikana, na kutukuzwa na watu, na akawa Mungu wa vitendo Aliyeheshimiwa, kupendwa, na kuenziwa na watu wote. Kristo anamiliki mawili, ubinadamu wa kawaida na uungu kamili. Yeye anaweza kuonyesha ukweli wakati wowote na mahali popote, na kufichua dutu ya upotovu ya wanadamu. Maneno Yake na mtazamo vimejaa ukweli na hekima, kama tu Bwana Yesu. Kile Kristo huzungumzia na Alicho nacho hakifunzwi kutoka kwa vitabu, lakini kabisa hutoka kwa kiini cha Mungu anachomiliki. Kristo alizaliwa na Mungu. Katika maisha yake watu huona ubinadamu wake wa kawaida kabisa. Kutokana na kazi Yake na uvumilivu Wake na wanadamu, watu wanaweza kuona kiini Chake cha Mungu na tabia yake ambayo si vumilivu kwa kosa la mtu. Ingawa, kama Bwana Yesu, Kristo ana udhaifu wa binadamu, Yeye pia ana kiini cha kutii Roho wa Mungu. Yeye Amejawa na ukweli na hekima, Akivutia usadikisho kabisa katika watu kote katika mioyo na maneno yao. Kristo ni ukweli, njia, na uzima, kwa jina na katika hali halisi! Mungu amekuwa mwili kama mtu wa kimbaombao, na hufanya kazi kwa siri na kwa unyenyekevu kati ya wanadamu, Akiwashinda wanadamu na kuwashinda maadui kwa njia ya maonyesho ya ukweli. Ni muda mrefu tangu Aliposhinda kabisa, na kushuhudiwa na kutangazwa. Huu ni uenyezi, hekima, na utukufu wa Mungu. Kutokana na kuonekana kwa Kristo na kazi, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilikuja kuwa. Kisha ndugu wa kike na wa kiume katika Kanisa la Mwenyezi Mungu wakaanza kutoa ushahidi kwa kazi ya Mungu, na kuanza kazi ya kueneza injili ya ufalme wa Kristo. Huu ni utangulizi mfupi wa usuli wa Mungu kupata mwili na kuja kwake kisiri ili kufanya kazi. Kuyasema kwa ufupi, Kristo aliyepata mwili Amekuja katika nchi ambapo joka kubwa jekundu hukaa, na kuonyesha maneno ya hukumu na kuadibu, na kuwashinda na kuwaokoa wateule wa Mungu nchini China. Ambayo ni kusema, Mungu aliyepata mwili hupigana na Shetani katika pango la joka kubwa jekundu, na kutoa kila kitu ili kuwaamsha watu, na kusababisha watu kusikia na kutambua sauti ya Mungu, na hivyo kurudi mbele ya Mungu na kuokolewa na Mungu. Hiki ni kitu ambacho ni nadra sana, na cha maana ya kina isiyosadikika. Katika kuwa mwili huku Mungu hufanya kazi ili kumwokoa mwanadamu, ambayo ina maana kwamba Mungu amekuja kupanga kikomo cha safari ya wanadamu na kutamatisha enzi hii. Mungu amekuja Uchina Bara, nchi inayokaliwa na joka kubwa jekundu, na Amewasili kisiri kufanya kazi, Akiwashinda na kuwaokoa wanadamu wapotovu kwa kina na kulikamilisha kundi la watu kuwa washindi. Hili limeashiria hukumu ya kiti kikubwa cheupe cha enzi katika siku za mwisho, na limefungua njia ya kuonekana kwa Mungu kwa kila taifa na mahali pa dunia wakati wa hatua inayofuata.

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Ole Wao Wale Wamsulubishae Mungu Mara Nyingine Tena

Katika siku za mwisho, Mungu amepata mwili katika nchi ya China kufanya kazi, na Ameonyesha mamilioni ya maneno, Akishinda na kuokoa kundi la watu kwa neno Lake na kuikaribisha enzi mpya ya hukumu ikianza na nyumba ya Mungu. Leo, kuenea kwa kazi ya Mungu katika siku za mwisho kumefikia kilele chake katika China Bara. Wengi wa watu katika Kanisa Katoliki na madhehebu yote ya Kikristo na makundi ya kidini ambayo yanafuatilia ukweli wamerudi mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Mungu mwenye mwili Amekamilisha kazi ya "ujio wa siri wa Mwana wa Adamu" Aliyetabiriwa katika Biblia, na hivi karibuni Ataonekana kwa umma katika kila taifa na sehemu ulimwenguni. Watu wote katika kila taifa na sehemu walio na kiu cha kuonekana kwa Mungu watatarajia kuonekana kwa Mungu hadharani. Hakuna nguvu zinazoweza kuzuia au kuangamiza ufalme wa Mungu, na mtu yeyote ambaye anapinga Mungu ataadhibiwa na ghadhabu ya Mungu, kama vile inavyosemwa katika maneno ya Mungu: “Ufalme Wangu unaenea katika ulimwengu mzima, na kiti Changu cha enzi kimenyakua mioyo ya matrilioni ya watu. Kwa usaidizi wa malaika wa mbinguni, utimilifu Wangu mkuu utakamilika hivi karibuni. Halaiki zote za Wanangu na watu Wangu, wanangoja kwa hamu kurejea Kwangu, wakitarajia kuunganishwa Kwangu nao, tusije tukatengana tena. Itawezekanaje watu wote wa ufalme Wangu wasikimbie wakifurahiana kila mmoja kwa kuunganika pamoja na Mimi tena? Inawezekana huu uwe muungano usio na gharama? Mimi Ninaheshimiwa machoni pa kila mtu, Ninadhihirika katika maneno ya kila mtu. Nitakaporejea, Nitashinda nguvu zote za adui mara tena. Wakati umewadia! Ninataka kazi Yangu ianze, Ninataka kuwa kiongozi mkuu juu ya mwanadamu! Tazama, Ninarejea! Ninaondoka! Hili ndilo kila mmoja anatarajia, ndilo kila mmoja anatumainia. Nataka kila mmoja ashuhudie kufika kwa siku Yangu na aikaribishe siku Yangu kwa furaha tele!” "Wale wote ambao Nawapenda wataishi milele kwa hakika, na wale wote wanaosimama dhidi Yangu wataadhibiwa na Mimi milele kwa hakika. Kwani Mimi ni Mungu mwenye wivu, Sitawasamehe kwa urahisi wanadamu kwa kile watakachokuwa wametenda. Nitaiangalia dunia yote, na, Nikitokea Mashariki ya dunia na haki, adhama, gadhabu, na adhabu, Nitajionyesha binafsi kwa wanadamu wengi wa tabaka mbalimbali!"

Asili na Maendeleo ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu lilikuja kuwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu—Bwana Yesu aliyerudi—Kristo wa siku za mwisho, na pia chini ya hukumu Yake ya haki na kuadibu. Kanisa limejumuisha wale wote ambao wanaikubali kwa kweli kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho na wameshindwa na kuokolewa na neno la Mungu. Liliasisiwa kabisa na Mwenyezi Mungu mwenyewe, na linaongozwa na kuchungwa binafsi na Yeye, na kamwe halikuanzishwa na mtu yeyote. Huu ni ukweli unaokubaliwa na watu wote waliochaguliwa katika Kanisa la Mwenyezi Mungu.

Kueneza kwa Injili ya Ufalme wa Mwenyezi Mungu Nchini China

Mwaka wa 1995, kazi ya kushuhudia kwa injili ya ufalme ya Mwenyezi Mungu ilianza rasmi China Bara. Kwa njia ya shukrani kwa Mungu na kwa upendo ambao ulikuwa wa kweli, tulishuhudia kwa kuoenekana na kazi ya Mwenyezi Mungu kwa ndugu wa kiume na kike katika madhehebu mbalimbali na makundi ya kidini. Hatukutarajia hata kidogo kukumbwa na upinzani na kukashifiwa kulikokithiri kutoka kwa viongozi wao. Tungeweza tu kuja mbele ya Mwenyezi Mungu kusali kwa ari, tukimsihi Mungu kufanya kazi binafsi. Kutoka 1997 na kuendelea, tulimwona Roho Mtakatifu akifanya kazi kwa kiwango kikubwa. Kulikuwa na ongezeko la haraka la washirika wa makanisa katika maeneo mbalimbali. Wakati huo huo, ishara nyingi na maajabu vilitokea, na watu wengi katika madhehebu mbalimbali na makundi ya kidini yakarudi kwa Mwenyezi Mungu kwa sababu ya kupokea ufunuo au kuona hizi ishara na maajabu. Kama Roho Mtakatifu hangekuwa amefanya kazi, mtu angefanya nini? Hili lilitufanya kutambua: Ingawa tulielewa baadhi ya ukweli, hatungeweza kutoa ushuhuda kwa Mwenyezi Mungu kwa nguvu zetu za kibinadamu pekee. Baada ya watu hawa kutoka madhehebu mbalimbali na makundi ya kidini kumkubali Mwenyezi Mungu, wao hatua kwa hatua walipata uhakika wa Mwenyezi Mungu katika mioyo yao kupitia kula na kunywa na kufurahia neno la Mwenyezi Mungu, na baada ya muda fulani, kulifanyika ndani yao imani halisi na utii. Watu kutoka kila dhehebu na kundi la kidini kwa hivyo waliinuliwa mbele ya kiti cha enzi, na hawakutarajiwa tena "kukutana na Bwana angani" kama walivyokuwa wamefikiri.

Kutazama Kuonekana kwa Mungu katika Hukumu na Kuadibu Kwake

Kama wale mamia ya mamilioni ya wengine wanaomfuata Bwana Yesu Kristo, tunafuata sheria na amri za Biblia, kufurahia neema tele ya Bwana Yesu Kristo, na kukusanyika pamoja, kuomba, kusifu, na kuhudumu kwa jina la Bwana Yesu Kristo—na haya yote sisi hufanya chini ya utunzaji na ulinzi wa Bwana.

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp