Kwa nini Mungu Huchukua Jina la Mwenyezi Mungu Katika Enzi ya Ufalme?

10/11/2017

Watu wengi hawaelewi ni kwa nini, kwa kuwa Mwenyezi Mungu ni kurudi kwa Bwana Yesu katika siku za mwisho, Bwana Yesu anaitwa Mwenyezi Mungu wakati Anapokuja kufanya kazi ya hukumu katika siku za mwisho. Kwa nini haendelei kuitwa Bwana Yesu? Kwa kweli, Mungu ana jina jipya kila wakati Anapofanya hatua moja ya kazi Yake. Jina hili jipya linachukuliwa na Mungu Mwenyewe kama inavyofaa kazi hii–siyo kitu ambacho watu humuita Yeye kama wanavyotaka. Jina la Bwana Yesu aliyerejea wa siku za mwisho lilitabiriwa zamani katika Biblia. Katika Kitabu cha Ufunuo, ilisemwa pia kuwa “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika…. Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, na nitaliandika jina la Mungu wangu juu yake, na jina la mji wa Mungu wangu, ambao ni Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu: na nitaliandika juu yake jina langu jipya(Ufunuo 3: 7, 12). “Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, Akasema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi(Ufunuo 1: 8). “Na nikasikia sauti kama sauti ya makutano mengi, na kama sauti ya maji mengi, na kama sauti ya radi yenye nguvu, ikisema, Haleluya; kwa kuwa Bwana Mungu Mwenyezi humiliki(Ufu 19: 6). Jina la Mwenyezi Mungu wa Enzi ya Ufalme ni utimizaji kamili waunabii wa kitabu cha Ufunuo. Jina ambalo Mungu huchukua katika kila enzi lina umuhimi mkubwa na limeshikamana kwa undani na kazi ya Mungu wakati wa enzi hiyo. Mwenyezi Mungu alifichua mafumbo yanayohusiana na hili Aliposema,

Katika kila enzi, Mungu Anafanya kazi mpya na huitwa kwa jina jipya; Je, anawezaje kufanya kazi sawa katika enzi tofauti? Itakuwaje Yeye kugandamana na yale ya zamani? Jina la Yesu lilichukuliwa kuwa la kazi ya ukombozi, hivyo bado Yeye Anaweza kuitwa kwa jina moja wakati Atarudi katika siku za mwisho? Je, bado Yeye Atafanya kazi ya ukombozi? Ni kwa nini Yehova na Yesu ni kitu kimoja, ilhali wanaitwa kwa majina tofauti katika enzi hizi tofauti? Je, si kwa sababu enzi za kazi Yao ni tofauti? Jina moja linawezaje kumwakilisha Mungu kwa ukamilifu wake? Kwa njia hii, lazima Mungu aitwe kwa jina tofauti katika enzi tofauti, lazima Atumie jina kubadilisha enzi na kuwakilisha hiyo enzi, kwa kuwa hakuna jina moja linaweza kumwakilisha Mungu mwenyewe kikamilifu. Na kila jina linaweza tu kuwakilisha kipengele cha wakati cha tabia ya Mungu katika enzi fulani; yote linahitaji kufanya ni kuwakilisha kazi Yake. Kwa hivyo, Mungu Anaweza kuchagua jina lolote ambalo linafaa tabia yake kuwakilisha enzi nzima. Bila kujali iwapo ni enzi ya Yehova, au ni enzi ya Yesu, kila enzi inawakilishwa kwa jina(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maono ya Kazi ya Mungu (3)).

‘Yehova’ ni jina Nililolichukua wakati wa kazi Yangu kule Uyahudi, nalo linamaanisha Mungu wa Wayahudi (Wateule wa Mungu) Anayeweza kumhurumia mwanadamu, kumlaani mwanadamu, na kuyaongoza maisha ya mwanadamu. Linamaanisha Mungu anayemiliki nguvu kuu na Amejawa na hekima. ‘Yesu’ ni Imanueli, nalo linamaanisha sadaka ya dhambi iliyojawa na upendo, Amejawa na huruma, naye Anamkomboa mwanadamu. Alifanya kazi ya Enzi ya Neema, naye Anawakilisha Enzi ya Neema, na Anaweza tu kuwakilisha sehemu moja ya mpango wa usimamizi. Yaani, Yehova pekee ndiye Mungu wa watu wateule wa Uyahudi, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, Mungu wa Musa, na Mungu wa Wayahudi wote. Na hivyo, katika enzi ya sasa, Waisraeli wote, isipokuwa Wayahudi, wanamwabudu Yehova. Wanamtolea kafara kwa madhabahu, na kumtumikia wakiwa wamevalia mavazi ya kikuhani katika hekalu. Wanachotumainia ni kuonekana tena kwa Yehova. Yesu pekee ndiye Mkombozi wa wanadamu. Yeye ni sadaka ya dhambi ambayo ilimkomboa mwanadamu kutoka kwa dhambi. Yaani, jina la Yesu lilitoka katika Enzi ya Neema, nalo lilikuwepo kwa ajili ya kazi ya wokovu katika Enzi ya Neema. Jina la Yesu lilikuwepo ili kuwawezesha watu wa Enzi ya Neema kuzaliwa upya na kuokolewa, nalo ni jina mahsusi la wokovu wa binadamu wote. Kwa hiyo jina Yesu linawakilisha kazi ya ukombozi, nalo linaashiria Enzi ya Neema. Jina Yehova ni jina mahsusi la Wayahudi walioishi chini ya sheria. Katika kila enzi na kila hatua ya kazi, jina Langu haliko bila msingi, lakini lina umuhimu wakilishi: Kila jina linawakilisha enzi moja. ‘Yehova’ linawakilisha Enzi ya Sheria, nalo ni jina la heshima kwa Mungu aliyeabudiwa na Wayahudi. ‘Yesu’ linawakilisha Enzi ya Neema, nalo ni jina la Mungu wa wale wote waliokombolewa katika Enzi ya Neema. Iwapo mwanadamu bado anatamani kuwasili kwa Yesu Mwokozi katika siku za mwisho, na bado anamtarajia Afike katika mfano aliochukua kule Uyahudi, basi mpango wote wa usimamizi wa miaka elfu sita ungekoma katika Enzi ya Ukombozi, nao usingeweza kuendelea zaidi. Siku za mwisho, hata zaidi, zisingeweza kufika, nayo enzi isingekomeshwa. Hiyo ni kwa sababu Yesu Mwokozi ni kwa ajili ya ukombozi na wokovu wa wanadamu peke yake. Nililichukua jina la Yesu kwa sababu ya watenda dhambi wote katika Enzi ya Neema, nalo si jina ambalo kwalo Nitawaangamiza wanadamu wote. Ingawa Yehova, Yesu, na Masihi yote yanawakilisha Roho Wangu, majina haya yanaashiria tu enzi tofauti katika mpango Wangu wa usimamizi, nayo hayaniwakilishi katika ukamilifu Wangu. Majina wanayoniita watu duniani hayawezi kueleza kwa ufasaha tabia Yangu nzima na yote Niliyo. Ni majina tofauti tu ambayo Ninaitwa katika enzi tofauti. Na hivyo, enzi ya mwisho—enzi ya siku za mwisho—itakapofika, jina Langu litabadilika tena. Sitaitwa Yehova, au Yesu, wala Masihi, lakini nitaitwa Mwenyezi Mungu Mwenyewe mwenye nguvu, na chini ya jina hili Nitatamatisha enzi nzima. Nilijulikana kama Yehova wakati mmoja. Pia niliitwa Masihi, na wakati mmoja watu waliniita Yesu Mwokozi kwa sababu walinipenda na kuniheshimu. Lakini leo Mimi si yule Yehova au Yesu ambaye watu walimfahamu nyakati zilizopita—Mimi ni Mungu ambaye Amerejea katika siku za mwisho, Mungu ambaye Ataikamilisha enzi. Mimi ni Mungu Mwenyewe ambaye Anainuka kutoka mwisho wa dunia, Nimejawa na tabia Yangu nzima, na Nimejawa na mamlaka, heshima na utukufu(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mwokozi Amerudi Tayari Juu ya “Wingu Jeupe”).

Mwenyezi Mungu alisema kwa dhahiri kwamba kuna umuhimu mwakilishi kwa jina ambalo Mungu huchukua katika kila enzi: Kila moja huwakilisha kazi ya Mungu na tabia Anayoonyesha katika enzi hiyo. Wakati wa Enzi ya Sheria, Mungu alitumia jina la Yehova kutangaza sheria na amri Zake na kuyaongoza maisha ya wanadamu duniani; wakati wa Enzi ya Neema, Mungu alitumia jina la Yesu kufanya kazi ya ukombozi wa wanadamu; na wakati wa Enzi ya Ufalme, Mungu anaitwa Mwenyezi Mungu, Yeye hufanya kazi ya hukumu Akianza na nyumba ya Mungu kumtakasa, kumbadilisha, na kumwokoa mwanadamu. Mungu hubadilisha enzi akitumia jina Lake, na hutumia jina hili kuwakilisha kazi ya enzi. Wakati Yehova Mungu alifanya kazi ya Enzi ya Sheria, ni kwa kuomba tu kwa jina la Yehova na kutii sheria na amri Zake ndipo watu wangeweza kubarikiwa na kulindwa na Mungu. Kwa kuwasili kwa Enzi ya Neema, Mungu alitumia jina la Yesu kufanya kazi ya ukombozi, na watu hawakuwa na budi ila kumkubali Bwana Yesu kama Mwokozi, na kuombea toba kwa jina la Bwana, kusamehewa dhambi zao na kufurahia ukweli na neema iliyotolewa na Bwana Yesu. Ikiwa watu bado walishikilia jina la Bwana na kukataa kumkubali Bwana Yesu, basi walipoteza utunzaji na ulinzi wa Mungu, na walianguka katika giza, wakilaaniwa na kuadhibiwa na Mungu kama Mafarisayo Wayahudi. Pamoja na ujio wa siku za mwisho, Mungu hutumia jina la Mwenyezi Mungu kutekeleza kazi ya hukumu Akianza na nyumba ya Mungu. Ni kwa kukubali jina la Mwenyezi Mungu tu, kwenda sambamba na hatua za kazi ya Mungu, na kufanyiwa hukumu na kuadibiwa kwa Mwenyezi Mungu, ndipo watu wanaweza kuelewa na kupata ukweli, kujitenga na dhambi, kutakaswa, na kupokea wokovu wa Mungu. Wote wanaokataa kulikubali jina la Mwenyezi Mungu na kukataa kazi Yake ya hukumu ya siku za mwisho hawawezi kujitoa wenyewe kutoka kwa utumwa wa dhambi, na milele hawatakuwa na sifa kamili kuingia katika ufalme wa mbinguni.

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp