430 Desturi wa Kuwa Mtulivu Mbele Ya Mungu

1 Ikiwa moyo wako umetulia mbele ya Mungu na unasonga karibu na Mungu haijalishi unachofanya, hii inathibitisha kuwa wewe ni mtu uliye mtulivu mbele ya Mungu. Unapozungumza na wengine, unapotembea, unaweza kusema, “Moyo wangu unasonga karibu na Mungu, na haulengi mambo ya nje, na naweza kutulia mbele ya Mungu.” Huyu ni mtu aliyetulia mbele ya Mungu. Usiingiliane na vitu vinavyoweza kuelekeza moyo wako kwa mambo ya nje, na usiingiliane na watu wanaoweza kuondoa moyo wako kwa Mungu. Achana na chochote kile kinachoweza kuvuta moyo wako usiwe karibu na Mungu, au kukaa mbali nacho. Njia hiyo ni ya manufaa zaidi kwa maisha yako.

2 Huu ndio wakati wa kazi kuu ya Roho Mtakatifu. Ni wakati ambao Mungu Mwenyewe anawakamilisha watu. Ikiwa kwa wakati huu huwezi kutulia mbele ya Mungu basi wewe si mtu unayerudi mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Ikiwa unafuatilia vitu badala ya Mungu hakuna uwezekano wa kukamilishwa na Mungu. Wale ambao leo wanaweza kusikia matamshi kama haya kutoka kwa Mungu na bado hawawezi kutulia mbele ya Mungu ni watu wasiopenda ukweli, watu wasiompenda Mungu. Ikiwa hutajitoa sasa utafanya hivyo lini? Kujitoa mwenyewe ni kuutuliza moyo wako mbele ya Mungu. Huku ni kujitoa kwa halisi. Yeyote anayetoa moyo wake kwa Mungu sasa kwa kweli bila shaka anaweza kukamlishwa na Mungu.

3 Hakuna chochote, haijalishi ni nini, kinaweza kukusumbua, ikiwa ni cha kukupogoa, au kukushughulikia, au ikiwa wewe hukutana na kuvunjwa moyo au kutofaulu, moyo wako unapaswa kila mara kutulia mbele ya Mungu. Haijalishi watu wanakutendea vipi, moyo wako unapaswa kutulia mbele ya Mungu. Haijalishi unakabiliwa na mazingira gani, iwe ni dhiki, taabu, au mateso, au ikiwa aina nyingi ya majaribio yanakukumba, moyo wako unapaswa kila mara kutulia mbele ya Mungu. Hii ni njia ya kukamilishwa. Kujitoa mwenyewe ni kuutuliza moyo wako mbele ya Mungu. Huku ni kujitoa kwa halisi. Yeyote anayetoa moyo wake kwa Mungu sasa kwa kweli bila shaka anaweza kukamlishwa na Mungu.

Umetoholewa kutoka katika “Kuhusu Kuutuliza Moyo Wako Mbele ya Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 429 Jinsi ya Kuutuliza Moyo Wako Mbele za Mungu

Inayofuata: 431 Matokeo ya Kutuliza Moyo Wako Mbele za Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp