540 Tupilia Mbali Ushawishi wa Giza ili Upatwe na Mungu

1 Je, ushawishi wa giza ni nini? “Ushawishi wa giza” ni ushawishi wa Shetani kuwadanganya, kuwapotosha kuwafunga na kuwatawala watu; ushawishi wa shetani ni ushawishi ambao una hali ya kifo. Wale wote ambao wanaishi chini ya miliki ya shetani wamehukumiwa kuangamia. Unawezaje kuepuka ushawishi wa giza baada ya kupata imani katika Mungu? Baada ya kumwomba Mungu kwa dhati, unaelekeza moyo wako Kwake kikamilifu. Katika hatua hii, moyo wako unasongezwa na Roho wa Mungu, uko tayari kujitoa mwenyewe kikamilifu, na katika wakati huu, umeepuka ushawishi wa giza. Kama yote ambayo mtu anafanya yanampendeza Mungu na anapatana na matakwa Yake, basi yeye ni mtu ambaye anaishi ndani ya maneno ya Mungu, yeye ni mtu anayeishi chini ya utunzaji na ulinzi wa Mungu.

2 Kama watu hawawezi kutenda maneno ya Mungu, daima wakimpumbaza na kutenda katika namna ya uzembe na Yeye, na hawaamini katika uwepo Wake, watu kama hao wote wanaishi chini ya ushawishi wa giza. Watu ambao hawajapokea wokovu wa Mungu wote wamemilikiwa na Shetani, yaani, hao wote wanaishi chini ya ushawishi wa giza. Wale ambao hawamwamini Mungu wamemilikiwa na Shetani. Hata wale ambao wanaamini katika kuwepo kwa Mungu huenda si lazima wawe wanaishi katika nuru ya Mungu, kwa sababu wale ambao wanamwamini huenda si lazima wawe wanaishi ndani ya maneno ya Mungu, na huenda si lazima wawe watu ambao wanaweza kumtii Mungu.

3 Kama unataka kusifiwa na Mungu, lazima kwanza uepuke ushawishi wa giza wa Shetani, ufungue moyo wako kwa Mungu, na uuelekeze kwa Mungu kikamilifu. Je, mambo ambayo unafanya kwa sasa yanasifiwa na Mungu? Umeelekeza moyo wako kwa Mungu? Je, mambo ambayo umeyafanya ni yale ambayo Mungu ametaka kutoka kwako? Je, yanaingiana na ukweli? Lazima ujichunguze kila wakati, uzingatie kula na kunywa maneno ya Mungu, uweke moyo wako wazi mbele Yake, umpende kwa uwazi, na ujitumie kwa bidii kwa ajili ya Mungu. Watu kama hao hakika watapokea sifa ya Mungu.

Umetoholewa kutoka katika “Epuka Ushawishi wa Giza na Utapatwa na Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 539 Ushawishi wa Shetani Hauwezi Kutupiliwa Mbali Bila Kufuatilia Ukweli

Inayofuata: 541 Fuata Maneno ya Mungu ili Kutupilia Mbali Ushawishi Mbaya

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp