727 Viumbe Walioumbwa Wanapaswa Kumtii Muumba

1 Kuna kanuni ya msingi zaidi ya Bwana wa uumbaji anavyovishughulikia viumbe, ambayo pia ndiyo kanuni ya juu zaidi. Jinsi anavyoshughulikia viumbe walioumbwa hutegemea kabisa mpango Wake wa usimamizi na matakwa Yake; Hahitaji kushauriana na mtu yeyote yule, wala Hahitaji kukubaliana na mtu yeyoye yule. Chochote Alichotafuta kufanya, na jinsi Alivyokusudia kuwatendea watu, Anafanya hivyo, na haijalishi Afanyacho na jinsi anayowatendea watu, yote yanapatana na kanuni, kanuni ambazo kwazo Bwana wa uumbaji hufanya kazi. Kama kiumbe aliyeumbwa, kitu cha pekee cha kufanya ni kutii; hakupaswi kuwa na chaguo lingine.

2 Inaonyesha kwamba Bwana wa uumbaji atakuwa Bwana wa uumbaji kila wakati; Ana nguvu na sifa zinazostahili kupanga na kutawala kiumbe yeyote aliyeumbwa kama Anavyopenda, na Hahitaji sababu ya kufanya hivyo. Haya ni mamlaka Yake. Hakuna yeyote kati ya viumbe walioumbwa ambaye, kulingana na alivyo kiumbe aliyeumbwa, ana nguvu au anayestahili kutoa uamuzi juu ya jinsi Muumba anavyopaswa kutenda au juu ya ikiwa kile anachofanya ni chema au kibaya, wala hakuna kiumbe yeyote aliyeumbwa anayestahili kuchagua ikiwa anapaswa kutawaliwa, kupangiwa, au kutupwa na Bwana wa uumbaji. Vivyo hivyo, hakuna kiumbe yeyote aliyeumbwa anayestahili kuchagua jinsi anavyotawaliwa na kutupwa na Bwana wa uumbaji. Huo ndio ukweli wa juu zaidi.

3 Bila kujali Bwana wa uumbaji Amewafanyia nini viumbe Wake walioumbwa, na bila kujali ameifanyaje, wanadamu Aliowaumba wanapaswa kutenda tu jambo moja: Kutafuta, kutii, kujua na kukubali ukweli huu uliowekwa na Bwana wa uumbaji. Matokeo ya mwisho yatakuwa kwamba Bwana wa uumbaji atakuwa amekamilisha mpango Wake wa usimamizi na kumaliza kazi Yake, baada ya kusababisha mpango Wake wa usimamizi kusonga bila vizuizi vyovyote; wakati huo huo, kwa sababu viumbe walioumbwa wamekubali utawala na mipango ya Muumba, na kutii utawala na mipango Yake, watakuwa wamepata ukweli, wameelewa mapenzi ya Muumbaji, na kuja kujua tabia Yake.

Umetoholewa kutoka katika “Ni kwa Kutafuta Ukwelitu Ndiyo Mtu Anaweza Kujua Matendo ya Mungu” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo

Iliyotangulia: 726 Kiumbe Aliyeumbwa Anapaswa Kuwa Chini ya Mungu

Inayofuata: 728 Kweli Unaweza Kutii Utaratibu wa Mungu?

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp