874 Kila Kitu Ambacho Mungu Humfanyia Mwanadamu Ni Cha Kweli

1 Kila kitu ambacho Mungu hufanya ni cha vitendo, na hakuna Anachofanya ambacho ni kitupu. Mungu huja kati ya wanadamu, Akijinyenyekeza kuwa mtu wa kawaida. Haondoki baada ya kufanya tu kazi kidogo na kunena maneno machache; badala yake, kwa kweli Yeye huja kati ya wanadamu ili kupitia mateso ya ulimwengu. Analipa gharama ya uzoefu Wake mwenyewe wa kuteseka ili kulipia hatima ya wanadamu. Je, si hii ni kazi ya vitendo? Wazazi wanaweza kulipa gharama ya dhati kwa ajili ya watoto wao, na hii inawakilisha uaminifu wao. Kwa kufanya hivi, Mungu mwenye mwili bila shaka anakuwa mnyoofu na mwaminifu kabisa kwa wanadamu.

2 Kiini cha Mungu ni uaminifu; Yeye hufanya Anachosema, na chochote Afanyacho hutimizwa. Kila kitu Anachowafanyia wanadamu ni cha kweli. Yeye haneni tu maneno; Anaposema kuwa atalipa gharama, Yeye kwa kweli hulipa gharama. Anaposema kwamba Atapitia mateso ya wanadamu na kuteseka badala yao, kwa kweli Yeye huja kuishi kati yao, Akihisi na kupitia mateso haya Yeye binafsi. Baada ya hapo, vitu vyote ulimwenguni vitakiri kuwa kila kitu ambacho Mungu hufanya ni sahihi na chenye haki, kwamba vyote ambavyo Mungu hufanya ni halisi: Hiki ni kipande cha ushahidi chenye nguvu.

3 Wanadamu watakuwa na hatima nzuri katika siku zijazo, na wale wote watakaobaki watamsifu Mungu; watasifu sana kwamba matendo ya Mungu kweli yalifanywa kutokana na upendo Wake kwa wanadamu. Asili ya Mungu ya uzuri na wema inaweza kuonekana katika umuhimu wa kupata mwili Kwake. Lolote Afanyalo ni la kweli; lolote Asemalo ni la dhati na halisi. Vitu vyote Anavyokusudia kuvifanya hufanywa kwa vitendo, na Yeye huvilipia gharama halisi; Yeye haneni tu maneno. Kwa hiyo, Mungu ni Mungu mwenye haki; Mungu ni Mungu mwaminifu.

Umetoholewa kutoka katika “Kipengele cha Pili cha Umuhimu wa Kupata Mwili” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo

Iliyotangulia: 873 Jinsi Kazi ya Mungu Ilivyo Ngumu

Inayofuata: 875 Umuhimu wa Kupata Mwili kwa Mungu ili Ateseke kwa Niaba ya Mwanadamu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp