260 Kwa Ajili ya Uzima wa Mwanadamu, Mungu Anastahimili Mateso Yote

Hakuna yeyote amewahi kuchunguza siri zinazoongoza asili na kuendelea kwa maisha ya mwanadamu. Ni Mungu tu, ambaye Anaelewa yote haya, kwa kimya huvumilia mapigo na maumivu ambayo binadamu, ambaye amepokea kila kitu kutoka kwa Mungu lakini bila shukurani, humpa. Binadamu huchukulia kila kitu kinacholetwa na maisha kimzaha, na, vilevile, nini “jambo lisilo na shaka,” kwamba Mungu anasalitiwa na mwanadamu, anasahaulika na mwanadamu, na kutozwa kwa nguvu na mwanadamu. Je, inaweza kuwa kwamba mpango wa Mungu ni wa maana namna hii kweli? Je inaweza kuwa kwamba mwanadamu, kiumbe huyu hai ambaye alitoka katika mkono wa Mungu, ni wa maana namna hiyo kweli? Mpango wa Mungu hakika ni wa umuhimu kabisa; hata hivyo, kiumbe chenye uhai kilichoumbwa na mkono wa Mungu kipo kwa ajili ya mpango Wake. Kwa hivyo, Mungu hawezi kuuharibu mpango Wake kwa sababu ya chuki kwa jamii hii ya wanadamu. Ni kwa ajili ya mpango Wake na kwa ajili ya pumzi aliyotoa ndiyo maana Mungu hustahimili mateso yote, sio kwa ajili ya mwili wa mwanadamu ila ni kwa sababu ya uhai wa mwanadamu. Yeye hufanya hivyo ili kurudisha pumzi Aliyopuliza ndani mwa mwanadamu, wala sio nyama za mwili. Huu ndio mpango wake.

Umetoholewa kutoka katika “Mungu Ndiye Chanzo cha Uhai wa Mwanadamu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 259 Hakuna Anayeelewa Matamanio ya Mungu Yenye Bidii ya Kumwokoa Mwanadamu

Inayofuata: 261 Mungu Asikitikia Mustakabali wa Binadamu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp