Mzunguko wa Uhai na Mauti wa Watu Mbalimbali Wenye Imani

10/09/2019

Tumemaliza kujadili mzunguko wa uhai na mauti wa kundi la kwanza, wasioamini. Hebu sasa tujadili ule wa kundi la pili, watu mbalimbali wenye imani. “Mzunguko wa uhai na mauti wa watu mbalimbali wenye imani” vilevile ni mada muhimu sana, na inafaa kwamba muwe na kiasi fulani cha uelewa wake. Kwanza, hebu tuseme ni imani gani “imani” kwa watu wa imani inaashiria: dini tano kuu za Uyahudi, Ukristo, Ukatoliki, Uisilamu, na Ubudha. Pamoja na wasioamini, watu ambao ni waumini katika hizi dini tano wanajumuisha idadi kubwa ya watu duniani. Miongoni mwa dini hizi tano, wale ambao wametengeneza ajira kutokana na imani yao ni wachache, lakini hizi dini zina waumini wengi. Waumini wake huenda sehemu tofauti wanapokufa. “Tofauti” na nani? Na wasioamini, watu wasiokuwa na imani, ambao tumemaliza kuzungumzia. Baada ya kufa, waumini wa hizi dini tano huenda mahali pengine, mahali tofauti na wasioamini. Lakini ni mchakato sawa. Ulimwengu wa kiroho pia utafanya uamuzi juu yao kutegemea yale yote waliyoyafanya kabla wafe, baadaye watatayarishwa ipasavyo. Lakini mbona hawa watu wanawekwa sehemu tofauti kutayarishwa? Kuna sababu muhimu ya hili. Na hii sababu ni gani? Nitawaambia kutumia mfano. Lakini kabla nifanye hivyo, mnaweza kuwa mkijiwazia: “Labda ni kwa sababu wana imani ndogo katika Mungu! Wao si wasioamini kabisa.” Hii ndiyo sababu mbona. Kuna sababu muhimu sana kwa wao kuwekwa mahali pengine.

Mzunguko wa Uhai na Mauti wa Watu Mbalimbali Wenye Imani

Chukua Ubudha: Hebu Niwaambie ukweli. Mfuasi wa Budha, kwanza kabisa, ni mtu aliyebadili dini kwenda Ubudha, na ni mtu ajuaye imani yake ni nini. Mfuasi wa Budha akinyoa nywele zake na kuwa mtawa wa kiume au mtawa wa kike, hii inamaanisha kuwa amejitenga na mambo ya kidunia na kuacha nyuma ghasia ya dunia ya mwanadamu. Kila siku anakariri maandiko ya sutra na kuimba majina ya Budha, na kula chakula bila nyama, anaishi maisha ya kujinyima anasa za kimwili, na kupitisha siku zake ndani ya mwangaza baridi, na hafifu wa taa ya mafuta ya siagi. Anaishi maisha yake yote kwa njia hii. Maisha yake ya kimwili yaishapo, anatengeneza muhtasari wa maisha yake, ila mioyoni mwake hajui atakapoenda baada ya kufa, atakutana na nani, na atakuwa na hatima ya aina gani—mioyoni mwake hana uhakika na haya mambo. Hajafanya chochote zaidi ya kuishi bila mwelekeo maisha yake yote akiambatana na imani, baadaye anaondoka duniani akiambatana na matamanio na maadili asiyoyafahamu. Hiyo ndiyo tamati ya maisha yake ya kimwili anapoiaga dunia ya walio hai, na baada ya hapo, anarudi katika sehemu yake asilia katika ulimwengu wa kiroho. Kama mtu hutu atapata mwili na kurudi duniani kuendelea na kujikuza kwake kunategemea mienendo na kujikuza kwake kabla ya kifo chake. Ikiwa hakufanya kitu kibaya wakati wa uhai wake, atapata mwili haraka na kurudishwa duniani, ambapo atakuwa mtawa wa kiume au mtawa wa kike tena. Kulingana na utaratibu wa mara ya kwanza, mwili wake unajikuza wenyewe, baada ya hapo anakufa na kurudi katika ulimwengu wa kiroho, ambapo anatathminiwa, na baada ya hapo—ikiwa hakuna shida—anaweza kurudi tena katika ulimwengu wa wanadamu, na kuweza kubadili dini hadi Ubudha tena na kuendelea kujikuza. Baada ya kupata mwili mara tatu hadi mara saba, atarudi tena katika ulimwengu wa kiroho, ambapo anakwenda kila mara ambapo maisha yake ya kimwili yanamalizika. Ikiwa viwango na mienendo yake mbalimbali katika ulimwengu wa wanadamu inaambata na sheria za mbinguni za ulimwengu wa kiroho, basi atabaki huko kutoka wakati huu kuendelea; hatapata mwili tena kama mwanadamu; wala hakutakuwa na tishio la yeye kuadhibiwa kwa kutenda maovu duniani. Hatawahi kupitia tena mchakato huu. Badala yake, kulingana na hali zake, atachukua nyadhifa katika milki ya kiroho. Hili ndilo wafuasi wa Budha wanaliita kufikia hali ya Ubudha.” Kufikia hali ya Ubudha hasa kunamaanisha kufanikiwa kama afisa wa ulimwengu wa kiroho, na baada ya hapo kutozaliwa tena katika mwili mpya ama kuwa katika hatari ya kuadhibiwa. Aidha, kunamaanisha kwamba hakuna kupata taabu tena ya kuwa mwanadamu baada ya kuzaliwa upya. Hivyo basi, bado kuna uwezekano wake kupata mwili tena kama mnyama? (La.) Hili linamaanisha kwamba anabaki kushika nafasi katika ulimwengu wa kiroho, na kamwe hatazaliwa upya. Huu ni mfano mmoja wa kufanikiwa kufikia hali ya Ubudha katika dini ya Ubudha. Na kuhusu wale ambao hawafanikiwi, baada ya wao kurudi katika ulimwengu wa kiroho, wanachunguzwa na kuthibitishwa na ofisa mhusika, ambaye anagundua kuwa ingawa wako hai, hawakujikuza kwa makini au kuwa makini katika kukariri maandiko ya sutra na kuimba majina ya Budha kama inavyotakiwa na dini ya Ubudha, na badala yake, walikuwa wametenda matendo mengi maovu na kujihusisha katika mienendo mingi mibaya. Basi katika ulimwengu wa kiroho hukumu inatolewa juu ya uovu wao, na baada ya hapo wana hakika ya kuadhibiwa. Hakuna vighairi katika hili. Basi, mtu kama huyu atafanikiwa lini? Katika maisha ambamo hakutenda maovu yoyote—wakati, baada ya kurudi katika ulimwengu wa kiroho, inaonekana hakufanya chochote kibaya kabla afariki. Basi anaendelea kuzaliwa upya, akiendelea kukariri maandiko ya sutra na kuimba majina ya Budha, akipitisha siku zake ndani ya mwangaza baridi na hafifu wa taa ya mafuta ya siagi, bila kuua chochote chenye uhai, bila kula nyama, na hafurahii ulimwengu wa mwanadamu, akiachana na vurugu zake kabisa, na kuepuka migogoro na wengine. Katika mchakato huu, hafanyi maovu, na kufuatia hayo anarudi katika ulimwengu wa kiroho, na baada ya matendo na mienendo yake yote kutathminiwa, anatumwa tena katika ulimwengu wa wanadamu, kwa mzunguko unaojirudia mara tatu au saba. Ikiwa hakuna kikwazo wakati huu, basi kupata kwake Ubudhaa hakutaathiriwa, na hakutacheleweshwa. Hii ni sifa ya mzunguko wa uhai na mauti wa watu wote wenye imani: Wanaweza “kufanikiwa” na kushikilia wadhifa katika ulimwengu wa kiroho; hili ndilo linawafanya kuwa tofauti na wasioamini. Kwanza kabisa, wanapokuwa hai duniani, matendo ya wale wanaoweza kushika wadhifa katika ulimwengu wa kiroho ni yapi? Ni sharti wasifanye kabisa ovu lolote: ni lazima wasifanye mauaji, uchomaji, ubakaji, au wizi; wakifanya hila, udanganyifu, au ujambazi, basi hawawezi kufanikiwa. Yaani, wakiwa na uhusiano au ushirikishaji wowote na uovu, hawataweza kuepukana na adhabu ya ulimwengu wa kiroho. Ulimwengu wa kiroho unafanya mipango inayofaa kwa wafuasi wa Budha wanaofikia hali ya Ubudha: wanaweza kuteuliwa kusimamia wale ambao wanaonekana kuamini katika Ubudha, na yule Mzee aliye Angani, na wafuasi wa Budha watapewa mamlaka, wanaweza tu kuteuliwa kuwasimamia wasioamini, vinginevyo wanaweza kuwa wasimamizi wadogo sana. Ugavi huo unalingana na asili ya hizi roho. Huu ni mfano wa Ubudha.

Miongoni mwa dini tano tulizozungumzia, Ukristo ni maalum kiasi fulani. Ni nini maalum kuhusu Ukristo? Hawa ni watu wanaomwamini Mungu wa kweli. Je, inawezekanaje wale wanaomwamini Mungu wa kweli waorodheshwe hapa? Kwa sababu Ukristo ni aina ya imani, basi, bila shaka, unahusiana tu na imani—ni aina ya sherehe, aina ya dini, na kitu tofauti na imani ya wale wanaomfuata Mungu kweli. Kilichonifanya kuuorodhesha miongoni mwa hizi dini tano ni kwa sababu Ukristo umeshushwa hadi kiwango sawa na Uyahudi, Ubudha, Uislamu. Wakristo wengi hawaamini kuna Mungu, au kwamba Anatawala juu ya vitu vyote, seuze kuamini katika uwepo Wake. Badala yake, wanatumia tu Maandiko Matakatifu kuzungumza kuhusu elimu ya dini, wakitumia elimu ya dini kuwafundisha watu kuwa wema, kuvumilia mateso, na kufanya vitu vizuri. Ukristo ni wa aina hiyo ya dini: Unazingatia tu nadharia za mafundisho ya kidini, hauna kabisa uhusiano wowote na kazi ya Mungu ya kusimamia na kuokoa wanadamu, ni dini ya wale wanaomfuata Mungu ambayo haitambuliwi na Mungu. Lakini pia Mungu ana kanuni kuhusu mtazamo Wake kwao. Hawatendei na kuwashughulikia wapendavyo bila mpango, njia sawa na wasioamini. Mtazamo Wake kwao ni sawa na Alio nao kwa wafuasi wa Budha: Ikiwa, angali hai, Mkristo anajiheshimu, anaweza kuzifuata kabisa Amri Kumi za Mungu na kuzingatia sheria na amri katika mahitaji yao kwa tabia zao wenyewe—na ikiwa wanaweza kufanya hivi katika maisha yao yote—basi pia watalazimika kuchukua muda sawa kupitia mzunguko wa uhai na mauti kabla hawajaweza kweli kupata huko kuitwako kuchukuliwa kuenda mbinguni. Baada ya kupata huku kunyakuliwa wanabaki katika ulimwengu wa kiroho, ambapo wanashika wadhifa na kuwa miongoni mwa wasimamizi. Vivyo hivyo, wakifanya maovu duniani, ikiwa ni watenda dhambi na kufanya dhambi nyingi, basi haiepukiki kwamba wataadhibiwa kwa ukali unaotofautiana. Katika Ubudha, kufanikiwa kunamaanisha kufika kwa Nchi Safi ya Furaha Kubwa Sana, lakini hii inaitwaje katika Ukristo? Inaitwa “kuingia mbinguni” na “kunyakuliwa.” Wale ambao kwa kweli “wananyakuliwa” pia wanapitia mzunguko wa uhai na mauti mara tatu hadi saba, halafu, wakiwa wamekufa, wanaingia katika ulimwengu wa kiroho, kana kwamba walikuwa usingizini. Ikiwa walikuwa wanafaa wanaweza kusalia kushika wadhifa, na tofauti na watu walio duniani, hawatapata mwili kwa njia rahisi, au kulingana na mazoea.

Miongoni mwa dini hizi zote, mwisho zinaozungumzia na ambao zinajitahidi kufikia ni sawa na kufanikiwa katika Ubudha; ni vile tu “kufanikiwa” huku kunatimizwa kwa njia tofauti. Wote ni wa aina moja. Kwa hili kundi la watu wa dini hizi ambao wanaweza kufuata kabisa maadili ya kidini katika tabia zao, Mungu huwapa hatima nzuri, sehemu nzuri ya kwenda, na kuwatendea inavyofaa. Haya yote ni sawa, ila si jinsi ambavyo watu wanadhani, sawa? Sasa, baada ya kusikia kuhusu yanayowatokea watu katika Ukristo, mnahisi vipi? Je, mnahisi kwamba shida zao si za haki? Mnawahurumia? (Kidogo.) Hakuna kitu kinachoweza kufanywa; watajilaumu wenyewe. Kwa nini Ninasema hivi? Kazi ya Mungu ni ya kweli; Yeye yu hai na kweli, na kazi Yake inawalenga wanadamu wote na kila mmoja. Kwa nini basi wasikubali hili? Ni kwa nini wanampinga kwa nguvu na kumtesa Mungu? Wana bahati hata kuwa na mwisho kama huu, basi mbona mnawaonea huruma? Kwa wao kutendewa namna hii kunaonyesha uvumilivu mkubwa. Kulingana na kiasi ambacho wanampinga Mungu, wanapaswa kuangamizwa—bali Mungu hafanyi hili, anaushughulikia Ukristo sawa tu na dini ya kawaida. Sasa kuna haja ya kutoa maelezo ya kina kuhusu dini nyinginezo? Maadili ya dini zote hizi ni kuwa watu wapitie shida zaidi, wasifanye maovu, watende mambo mema, wasiwaapize watu wengine, wasiwahukumu wengine, wajitenge na ugomvi, na wawe watu wazuri—mafundisho ya kidini mengi ni ya aina hii. Na kwa hiyo, kama hawa watu wa imani—hawa watu wa dini na madhehebu mbalimbali—wanaweza kufuata kabisa maadili ya kidini, basi hawatafanya makosa au dhambi nyingi wakati wangali duniani, na baada ya kupata mwili mara tatu hadi saba, basi kwa jumla watu hawa, watu ambao wanaweza kufuata kabisa maadili ya kidini, watabaki kushikilia wajibu katika ulimwengu wa kiroho. Na je, kuna watu wengi wa aina hii? (La, hakuna wengi.) Jibu lako linategemea nini? Si rahisi kutenda mazuri, au kufuata amri na sheria. Ubudha hauwaruhusu watu kula nyama—unaweza kufanya hilo? Ungepaswa kuvaa kanzu za kijivu na kukariri maandiko ya sutra na kuimba majina ya Budha katika hekalu la wafuasi wa Budha siku nzima, ungeweza kufanya hivyo? Haingekuwa rahisi. Ukristo una Amri Kumi za Mungu, amri na sheria, je, ni rahisi kufuata? Si rahisi! Chukua mfano wa kutowaapia wengine: Watu hawawezi kufuata hii amri. Kwa kushindwa kujizuia wenyewe, wanaapa—na baada ya kuapa hawawezi kurudisha kiapo, basi wanafanya nini? Usiku wanakiri dhambi zao. Wakati mwingine baada ya kuwaapia wengine, bado kuna chuki mioyoni mwao, na hata wanazidi zaidi na kupanga ni lini watawadhuru. Kwa jumla, kwa wale wanaoishi katika hii imani iliyokufa, si rahisi kukosa kufanya dhambi au kutenda maovu. Na kwa hiyo, katika kila dini, ni watu wachache sana tu ndio wanaweza kufanikiwa kweli. Unadhani kwamba kwa sababu watu wengi sana wanafuata hizi dini, wengi wataweza kubaki kuchukua nafasi katika milki ya kiroho. Lakini si wengi hivyo, ni wachache tu ndio wanaweza kulifikia hili. Kwa jumla ni hayo tu kwa mzunguko wa uhai na mauti wa watu wenye imani. Kinachowatofautisha ni kwamba wanaweza kufanikiwa, na hiki ndicho kinawatofautisha na wasioamini.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Ulimwengu wa kiroho ni nini?

Kwa ulimwengu yakinifu, watu wakikosa kuelewa vitu au jambo fulani, wanaweza kutafuta taarifa mwafaka, vinginevyo wanaweza kutumia njia...

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp