Watu wengi katika ulimwengu wa kidini wanaamini kuwa wachungaji na wazee wa kanisa wamechaguliwa na kuwekwa na Bwana, na kwamba wote humtumikia Bwana katika makanisa ya kidini; tukiwafuata na kuwatii wachungaji na wazee wa kanisa, sisi kwa kweli tunamtii na kumfuata Bwana. Kwa mintarafu hasa ya maana ya kumtii mwanadamu na kumfuata mwanadamu, na kinachomaanishwa hasa maana na kumtii Mungu na kumfuata Mungu, watu wengi hawaelewi kipengele hiki cha ukweli, kwa hiyo tafadhali shiriki hili kwa ajili yetu.

09/06/2019

Jibu:

Katika dini, watu wengine hufikiri wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa wote wamechaguliwa na kuwekwa na Bwana. Kwa hivyo, watu wanapaswa kuwatii. Je, mtazamo kama huu una msingi wowote katika Biblia? Je, umethibitishwa na neno la Bwana? Je, una ushuhuda wa Roho Mtakatifu na uthibitisho wa Roho Mtakatifu? Ikiwa majibu yote ni la, si basi imani ya walio wengi kuwa wachungaji na wazee wa kanisa wote wameteuliwa na kuwekwa imara na Bwana hutukia katika dhana na mawazo ya watu? Tufikirie hayo. Katika Enzi ya Sheria, Musa alichaguliwa na kuwekwa na Mungu. Je, hili lina maana kuwa viongozi wote Wayahudi wakati wa Enzi ya Sheria walikuwa wameteuliwa na kutayarishwa na Mungu? Katika Enzi ya Neema, Mitume 12 wa Bwana Yesu wote walichaguliwa na kupakwa mafuta na Bwana Yesu Mwenyewe. Je, hili linamaanisha kuwa wachungaji wote na wazee wa kanisa katika Enzi ya Neema walichaguliwa binafsi na kuandaliwa na Bwana? Watu wengi hupenda kufuata sheria zilizowekwa na hawasogelei mambo kulingana na ukweli. Matokeo yake, wanaabudu na kuwafuata watu kwa upofu. Tatizo ni lipi hapa? Kwa nini watu hawawezi kutofautisha baina ya mambo haya? Kwa nini hawawezi kutafuta ukweli katika mambo haya?

Tunaweza kuona kutoka kwa kile kilichorekodiwa katika Biblia kuwa katika kila enzi ya kazi Yake, Mungu huchagua na kuwateua baadhi ya watu kuratibu kazi Yake. Na wale walioteuliwa na kutumiwa na Mungu Mwenyewe huthibitishwa na neno Lake. Hata kama hakuna neno la Mungu, angalau kunapaswa kuwa na uthibitisho wa kazi ya Roho Mtakatifu. Kama vile wakati wa Enzi ya Sheria, Mungu alimpaka mafuta Musa kuwaongoza Waisraeli. Hilo limethibitishwa na neno la Mungu. Kama tu vile Yehova Mungu alisema, “Kwa hivyo basi, tazama, nimefikiwa na kilio chao wana wa Israeli: na mimi pia nimeona ukandamizaji ambao Wamisri wanatumia kuwakandamiza. Kwa hivyo njoo sasa, nami nitakutuma kwake Farao, ili uwalete watu wangu, wana wa Israeli, kutoka Misri(Kutoka 3:9-10). Katika Enzi ya Neema, Bwana Yesu aliwapaka mafuta mitume 12 kuyachunga makanisa. Kama vile Bwana Yesu alivyompaka mafuta Petro: “Simoni, mwana wa Yona, Unanipenda Mimi? … Walishe kondoo wangu(Yohana 21:17). “Na nitakupa funguo za ufalme wa mbinguni: na chochote utakachofunga duniani kitafungwa mbinguni: na chochote utakachoweka huru duniani kitawekwa huru mbinguni(Mathayo 16:19). Tunaweza kuona watu walioteuliwa na kutumiwa na Mungu wanashuhudiwa na Mungu na wote wanathibitishwa na neno la Mungu, na uthibitisho wa kazi ya Roho Mtakatifu. Kazi yao yote huungwa mkono na Mungu. Kutii kazi zao na uongozi ni kumtii Mungu. Yeyote kati yetu ambaye humpinga mtu ambaye Mungu anampaka mafuta na kumtumia anampinga Mungu na atalaaniwa na kuadhibiwa na Mungu. Kama ilivyo katika Enzi ya Sheria, Kora, Dathani na watu wao walimpinga Musa. Nini kilichotokea mwishoni? Waliadhibiwa moja kwa moja na Mungu. Mungu aliifanya dunia ifunguke na kuwameza wote. Kila mtu anajua huu ni ukweli. Katika Enzi ya Neema, mitume waliopakwa mafuta na Bwana Yesu wote wana uthibitisho wa neno la Bwana. Lakini je, wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa wa leo wanapakwa mafuta na Bwana? Je, inathibitishwa na neno la Bwana? Wengi wao wanakuzwa na shule za teolojia na wana vyeti vya kuhitimu katika teolojia, ambayo walitegemea kuwa wachungaji, si kwa sababu Roho Mtakatifu binafsi aliwashuhudia na kuwatumia. Je, huo sio ukweli? Ni nani kati yetu aliyesikia au kuona Roho Mtakatifu akimshuhudia au kumpaka mafuta mchungaji yeyote? Haifanyiki kamwe! Ikiwa kweli wanapakwa mafuta na Bwana, hakika kuna ushahidi wa kweli wa Roho Mtakatifu na waumini wengi kama mashahidi. Kwa hivyo, wachungaji na wazee wa kanisa wa kidini wote hawapakwi mafuta na Bwana. Hii ni ya hakika! Nimesikia kwamba hata kuna baadhi ya wachungaji ambao hawaamini Bwana Yesu alitokana na utungaji mimba na Roho Mtakatifu. Hawafikiri “utungaji mimba na Roho Mtakatifu” una msingi wowote au kukubaliana na sayansi. Kuna hata uwezekano mdogo kuwa watu hawa wangekubali kwamba Kristo ni udhihirisho wa Mungu. Wachungaji kama hawa wangekuwapo wakati ambapo Bwana Yesu alifanya kazi, hakika wasingemkubali Bwana Yesu. Basi wangechukuliaje kuonekana kwa Mungu na kazi ya Mungu mwenye mwili katika siku za mwisho? Wote wangekuwa kama makuhani wakuu, waandishi, na Mafarisayo wa Kiyahudi, kumtukana kwa ukali na kumpinga Bwana Yesu. Basi wachungaji na wazee wa kanisa kama hawa wanamtii Mungu kwa kweli? Hata hawaamini katika Mungu mwenye mwili, na pia hawatambui ukweli ulioonyeshwa na Mungu mwenye mwili. Je, watu hawa si ni wapinga Kristo? Hivyo mtazamo kwamba “wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa wote wamepakwa mafuta na kutumiwa na Bwana” bado una utetezi? Tukisisitiza kuwa wachungaji hawa na wazee wa kanisa wamepakwa mafuta na kutumiwa na Mungu, basi si huku ni kumdharau na kumkufuru Mungu? Je, Mungu angewapaka mafuta na kuwatumia hawa wasioamini na wapinga Kristo kuwaongoza watu waliochaguliwa na Mungu? Je, mtazamo kama huu si ni wa upuuzi, wa uwongo sana? Je, si huku ni kugeuza ukweli na kuchanganya nyeusi na nyeupe?

Sasa sote tu wazi baada ya mawasiliano kiasi. Wote waliopakwa mafuta na kutumiwa na Mungu wanashuhudiwa binafsi na Mungu, na angalau wana uthibitisho na athari za kazi ya Roho Mtakatifu, na wanaweza kuwasaidia watu wa Mungu waliochaguliwa kupata ruzuku ya maisha na uchungaji wa kweli. Kwa sababu Mungu ni mwenye haki, mtakatifu, wote waliopakwa mafuta na kutumiwa na Mungu kwa hakika wanakubaliana na mapenzi ya Mungu. Hakika wao hawatakuwa Mafarisayo wanafiki, na aidha hawatakuwa wapinga Kristo wanaochukia ukweli, wanaompinga Mungu. Basi hebu tuwaangalie wachungaji na viongozi wa kidini wa leo. Wengi wao wanakuzwa kutoka katika shule za kiteolojia na wala sio kupakwa mafuta na kutumiwa na Mungu binafsi. Wanajifunza tu teolojia na Biblia. Kazi yao na mahubiri yanalenga tu kuzungumza juu ya maarifa ya Biblia, teolojia, au wahusika wa Biblia na hadithi, asili ya kihistoria, na kadhalika. Wanayotenda pia ni kuwafundisha tu watu kufanya matambiko ya kidini na kufuata kanuni. Hawazingatii kamwe kuwasilisha ukweli katika maneno ya Mungu, wala kuwaongoza watu kutenda na kujifunza maneno ya Mungu au kuzingatia amri za Mungu. Kamwe hawajadili jinsi ya kujijua wenyewe na uzoefu halisi katika uingiaji katika maisha, na aidha kamwe hawajadili maarifa ya kweli ya Mungu. Je, kazi kama hiyo na kuhubiri kunaweza kupata kazi ya Roho Mtakatifu? Je, huduma hiyo inaweza kutosheleza nia ya Mungu? Je, inaweza kutuongoza kutenda ukweli na kuingia kwenye njia sahihi ya kuamini katika Mungu? Kuelezea Biblia kwa njia hii, je, sio hawaendi kwenye njia yao wenyewe na kumpinga Mungu? Hasa wakati ambapo Mwenyezi Mungu anaonyesha ukweli na kufanya kazi Yake ya hukumu ya siku za mwisho, viongozi hawa wa dini wanajua wazi kwamba maneno ya Mwenyezi Mungu yote ni ukweli na yanaweza kuwatakasa na kuwaokoa watu, na bado hawayatafuti wala kuyakubali. Hata la kuchukiza zaidi ni kwamba hawaruhusu waumini kuyasoma maneno ya Mwenyezi Mungu au kusikiliza sauti ya Mungu. Kwa ajili ya kulinda hadhi zao na maisha yao, wao humkashifu na kumhukumu Mwenyezi Mungu kwa ghadhabu, hata kukubaliana na CCP, utawala wa Shetani, katika kuwakamata na kuwatesa wainjilisti. Je, matendo na mienendo ya hawa wachungaji na wazee wa kanisa yanatofautianaje na ya wale wa Mafarisayo ambao walimkataa Bwana Yesu siku hiyo ya awali? Je, sio kikwazo kwa sisi kukubali njia ya kweli? Je, hawa watu wanaochukia ukweli, watu wanaopinga Mungu Wanawezaje kupakwa mafuta na kutumiwa na Mungu? Je, Mungu angeweza kuwateua watu hawa wanaochukia ukweli ambao huyazuia mapenzi ya Mungu kuongoza watu waliochaguliwa na Mungu? Sivyo kabisa! Huo ni ukweli!

Baadhi ya watu wapumbavu katika miviringo ya kidini mara nyingi hutumia vibaya maneno kutoka katika Biblia ili kubuni amri. Wanadai kwamba Mafarisayo wanafiki na wachungaji wa kidini wote wanapakwa mafuta na kutumiwa na Mungu. Je, huku sio kumpinga na kumtukana Mungu kwa ukali? Watu wengi hawajui jinsi ya kutofautisha. Wanaamini katika Bwana lakini hawamtukuzi, badala yake wanapigania vipawa, hadhi na nguvu, na pia huwaamini na kuwaabudu wachungaji na wazee wa kanisa kwa upofu. Hawawezi kutofautisha kama mtu ana kazi ya Roho Mtakatifu na hali halisi ya ukweli. Wanafikiri tu kuwa almuradi mtu ana cheti cha mchungaji na vipawa na anaweza kuchambua Biblia, inamaanisha kuwa wanaidhinishwa na wamepakwa mafuta na Mungu, na kwamba wanafaa kutiiwa. Watu wengine hata ni wapumbavu zaidi na hufikiri kuwatii wachungaji na wazee wa kanisa ni kumtii Mungu, na kwamba kuwapinga wachungaji na wazee wa kanisa ni kumpinga Mungu. Tukienda kwa mujibu wa fikira kama hizi, makuhani wakuu wa Kiyahudi, waandishi na Mafarisayo ambao wote walijua Biblia na mara nyingi walielezea Biblia kwa wengine, lakini walimpinga na kumhukumu Bwana Yesu wakati Alipoonekana na kufanya kazi, na hata wakamsulubisha, je, walikuwa watu waliopakwa mafuta na kutumiwa na Mungu? Ikiwa mtu aliwafuata viongozi wa Kiyahudi katika kumpinga na kumhukumu Bwana Yesu, je, hiyo inamaanisha kwamba alikuwa wanamtii Mungu? Ungesema wale waliokataa viongozi wa Kiyahudi na wakamfuata Bwana Yesu walikuwa wanampinga Mungu? Hii inaonyesha kwamba mtazamo “Kuwatii wachungaji na wazee wa kanisa ni kuwatii Mungu, kuwapinga wachungaji na wazee wa kanisa ni kumpinga Mungu” kwa kweli ni upuuzi sana na udanganyifu! Sisi waumini wa Mungu tunapaswa kuwa wazi kwamba wachungaji na wazee wa kanisa wa kidini wakimpinga Mungu, na njia wanayopitia husaliti ukweli na kumpinga Mungu, basi tunapaswa kusimama upande wa Mungu, kuwafichua, na kuwakataa. Huo ni utiifu wa kweli wa Mungu. Huku ni kutelekeza giza kwa ajili ya nuru na kutosheleza dhamira ya Mungu. Kwa hivyo, linapofikia suala la jinsi ya kuwashughulikia na wachungaji na wazee wa kanisa, tunapaswa kufuata ukweli na kuelewa nia ya Mungu. Kama wachungaji na wazee wa kanisa ni watu wanaopenda ukweli na kufuatilia ukweli, basi hakika watakuwa na kazi ya Roho Mtakatifu na watakuwa na uwezo wa kutuongoza katika kutenda na kuyapitia maneno ya Mungu, kumcha Mungu na kuondoka na uovu. Kuheshimu na kuwafuata watu kama hao hukubaliana na nia za Mungu! Ikiwa hawapendi ukweli na hujali tu juu ya kueleza ujuzi wao wa Biblia na nadharia ya kiteolojia ya kujionyesha na kujijenga wenyewe, kutufanya tuwaabudu na kuwatii, na hawamtukuzi Mungu, kumshuhudia Mungu, wala kutuongoza kutenda na kuyapitia maneno ya Mungu, basi ni watu ambao wamehukumiwa na kulaaniwa na Mungu na tutakuwa tunampinga Mungu ikiwa bado tunaabudu, kufuata na kuwatii. Hii itakuwa kinyume kabisa na nia za Mungu.

Kimetoholewa kutoka katika Maswali na Majibu Bora zaidi Kuhusu Injili ya Ufalme

Kumtii Mungu na kumfuata Mungu ni nini hasa? Kuhusu kipengele hiki cha ukweli, hebu kwanza tusome fungu la maneno ya Mungu: “Kilicho na umuhimu mkuu katika kumfuata Mungu ni kwamba kila kitu kinapaswa kuwa kwa kadri ya maneno ya Mungu leo: Kama unafuatilia kuingia katika uzima au kutimiza mapenzi ya Mungu, kila kitu kinapaswa kulenga maneno ya Mungu leo. Kama kile ambacho unawasiliana kwa karibu na kufuatilia hakilengi maneno ya Mungu leo, basi wewe ni mgeni kwa maneno ya Mungu, na umeondolewa kabisa katika kazi ya Roho Mtakatifu. Kile ambacho Mungu hutaka ni watu ambao huzifuata nyayo Zake. Haijalishi vile ulichoelewa awali ni cha ajabu na safi, Mungu hakitaki, na kama huwezi kuweka kando vitu hivyo, basi vitakuwa kizuizi kikubwa mno kwa kuingia kwako katika siku za baadaye. Wale wote ambao wanaweza kufuata nuru ya sasa ya Roho Mtakatifu wamebarikiwa. Watu wa enzi zilizopita pia walifuata nyayo za Mungu, ilhali hawangeweza kufuata mpaka leo; hii ndiyo baraka ya watu wa siku za mwisho. Wale ambao wanaweza kufuata kazi ya sasa ya Roho Mtakatifu, na ambao wanaweza kuzifuata nyayo za Mungu, kiasi kwamba wamfuate Mungu popote Awaongozapo—hawa ni watu ambao wamebarikiwa na Mungu. Wale wasiofuata kazi ya sasa ya Roho Mtakatifu hawajaingia katika kazi ya maneno ya Mungu, na haijalishi wanafanya kazi kiasi gani, au mateso yao ni makubwa vipi, au wanakimbia hapa na pale kiasi gani, hakuna linalomaanisha chochote kwa Mungu kati ya hayo, na Yeye hatawasifu. … ‘Kuifuata kazi ya Roho Mtakatifu’ kuna maana ya kufahamu mapenzi ya Mungu leo, kuweza kutenda kwa mujibu wa masharti ya sasa ya Mungu, kuweza kutii na kumfuata Mungu wa leo, na kuingia kwa mujibu wa matamshi mapya zaidi ya Mungu. Huyu pekee ndiye mtu ambaye hufuata kazi ya Roho Mtakatifu na yuko ndani ya mkondo wa Roho Mtakatifu. Watu hao hawawezi tu kupokea sifa za Mungu na kumwona Mungu, lakini wanaweza pia kujua tabia ya Mungu kutoka kwa kazi ya karibuni zaidi ya Mungu, na wanaweza kujua dhana na ukaidi wa mwanadamu, na asili na kiini cha mwanadamu, kutoka kwa kazi Yake ya karibuni zaidi; pia, wanaweza kutimiza polepole mabadiliko katika tabia yao wakati wa huduma yao. Ni watu kama hawa pekee ndio wanaoweza kumpata Mungu, na ambao wamepata kwa halisi njia ya kweli(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Jua Kazi Mpya Zaidi ya Mungu na Ufuate Nyayo Zake). Kumfuata Mungu kimsingi kunamaanisha kufuata kazi ya sasa ya Mungu, kutii na kuyatenda maneno ya sasa ya Mungu, kuwa na uwezo wa kuzifuata amri za Mungu, kutafuta mapenzi ya Mungu katika masuala yote, kutenda kulingana na neno la Mungu, na kutii kabisa kazi na mwongozo wa Roho Mtakatifu. Hatimaye, kunamaanisha kuwa mtu anayetenda ukweli na kuyafuata mapenzi ya Mungu. Ni mtu wa aina hii pekee ndiye mfuasi wa Mungu, mtu anayepata wokovu wa Mungu. Kama katika imani yetu tunaitegemea na kuitukuza Biblia kwa nje, huku kwa kweli utendaji na kupitia kwetu ni kulingana na maneno na mafundisho ya binadamu katika Biblia badala ya kutii na kutenda neno la Mungu kutoka katika Biblia, na ikiwa hatuzielewi nia za Mungu na badala yake kushikilia tu taratibu na amri za dini, huku ni kumfuata mwanadamu. Tukifuata na kutenda maneno ya watu kutoka katika Biblia kana kwamba hayo yalikuwa maneno ya Mungu, lakini bado tumchukulie Bwana Yesu kuwa mkubwa wa jina tu, tukipuuza maneno Yake na kutofanya chochote kufuata amri Zake, basi hakika tutasukumwa mbali na kulaaniwa na Bwana Yesu, kama tu walivyofanyiwa Mafarisayo wanafiki. Kuna watu wengi walio na imani katika Bwana, lakini bado wanawaabudu bila kufikiria watu maarufu wa roho au wachungaji na wazee—wanawacha Mafarisayo wanafiki. Chochote kinachowakumba wanakimbia kwa wachungaji na wazee kutafuta mwongozo na kufanya vivyo hivyo inapofikia kuchunguza njia ya kweli. Kama matokeo, wanadanganywa na kupotoshwa na Mafarisayo wanafiki na viongozi wa dini na wanaingia katika njia ya kumpinga Mungu—haya ndiyo matokeo na miisho ya kumfuata mwanadamu badala ya Mungu. Njia ya pekee ya kumfuata Mungu kweli ni kuweka imani yetu kwa msingi wa kuifuata kazi ya Roho Mtakatifu pekee, kuyafuata maneno ya sasa ya Mungu, kuzifuata nyayo za kazi ya Roho Mtakatifu, na kufanya liwezekanalo kukamilisha wajibu wetu. Hasa wakati Mungu anafanya kazi Yake ya hukumu katika siku za mwisho, dunia ya dini imepoteza kazi ya Roho Mtakatifu na imekuwa yenye ukiwa. Wakati tunalazimishwa kuitafuta njia ya kweli, tunapaswa kuwa makini hata zaidi katika kuyatafuta maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa; lazima tuyatafute maneno na matamshi ya Mungu na kazi ya Roho Mtakatifu. Tusipotafuta maneno na kazi ya Roho Mtakatifu, tusipoweza kuisikia sauti ya Mungu, tusipoweza kupata lishe ya maneno ya sasa ya Mungu, basi badala yake tutaondolewa, kutupwa kando wakati wa kazi ya Mungu katika siku za mwisho, tukibiringika katika giza, tukilia na kusaga meno yetu. Watu wanaomfuata na kumtii Mungu kwa kweli hawatawahi kuachwa na Yeye kamwe. Wale wanaowaabudu wachungaji na wazee wa dini wanamtii mwanadamu na ni wafuasi wa mwanadamu. Watu hawa hatimaye watawekwa wazi na na kazi ya Mungu—wataondolewa na kutupwa kando.

Hata ingawa kutoka kwa vinywa vyetu tunapaza sauti kwamba tunamwamini Mungu na kwamba tunapaswa kumfuata Mungu tu na kumtii Yeye, hata hivyo, nini kinafanyika katika uhalisi si sawa. Tunaweza kuona hili dhahiri kutoka kwa njia ambayo wale wa imani ya Kiyahudi katika Enzi ya Neema walivyomtendea Bwana Yesu kinyume na jinsi Petro na Yohana na wengine walivyofanya. Bwana Yesu alitekeleza kazi Yake mpya, akatoa ukweli, na kuleta njia ya toba, lakini watu wengi wa Kiyahudi wakati huo waliyasikiza mafundisho ya makuhani wakuu na Mafarisayo tu. Hawakukubali kazi na maneno ya Bwana Yesu, na kwa kama matokeo waliupoteza wokovu wa Bwana Yesu. Kwa jina tu, walimwamini Mungu, lakini kwa kweli waliwaamini makuhani wakuu, waandishi na Mafarisayo. Hata hivyo, Petro, Yohana, Mathayo, Filipo na wale wengine waliona kwamba maneno na kazi ya Bwana Yesu yalikuwa na mamlaka na nguvu, na kwamba yalikuwa ukweli. Waliona kwamba maneno na kazi ya Bwana Yesu yalitoka kwa Mungu na hivyo walimfuata kwa karibu. Hawakupitia hata kidogo udhibiti wa Mafarisayo na walikuwa ndio wale waliomfuata na kumtii Mungu kweli. Katika siku za mwisho, njia ya pekee ya kumfuata na kumtii Mungu kweli ni kukubali na kutii kazi ya Mwenyezi Mungu ya hukumu, na huku kunakamilisha unabii unaopatikana katika Kitabu cha Ufunuo: “Hao ndio wale wanaomfuata Mwanakondoo popote aendapo(Ufunuo 14:4). Kwa sasa, viongozi katika dunia ya dini wanafanya wajibu wa Mafarisayo wa Kiyahudi, wakifanya kila juhudi kuyatukuza maneno ya mwanadamu katika Biblia, ilhali wanasaliti maneno ya Bwana Yesu. Cha upuuzi hata zaidi, wanaitumia Biblia kwa kutaja vifungu nje ya muktadha ili kuishutumu kazi ambayo Mungu anafanya katika siku za mwisho—wanafanya haya ili kuwadanganya, kuwafunga, na kuwadhibiti waumini. Kwa mfano, Bwana Yesu alisema wazi kwamba “Ila yeye atendaye mapenzi ya Baba yangu ambaye yuko mbinguni(Mathayo 7:21). pekee ndiye atakayeingia katika ufalme wa Mbinguni. Na bado miongoni mwa viongozi katika dunia ya dini, wanasema kwamba kila ambacho mwanadamu anahitaji kufanya katika imani yake ni kufanya kazi kwa bidii na kisha anaweza kuingia katika ufalme wa mbinguni, na kwamba ufalme wa mbinguni ni kitu ambacho kinaweza kutekwa kwa nguvu. Bwana Yesu alihitaji kutoka kwetu kwamba: “Muabudu Bwana Mungu wako(Mathayo 4:10), na bado wengine wanaodaiwa kuwa watu maarufu wa roho wanawaongoza waumini kutafuta jinsi ya kuwa Mungu au kutafuta kuwa mfalme na kutawala mataifa yote na watu wote, jambo ambalo ni la upuuzi kabisa. Viongozi katika dunia ya dini kwa jina tu humfanyia Bwana kazi na kuhubiri mahubiri, lakini kwa kweli wanaeneza mafundisho ya mwanadamu tu, wakikuza fikira zao wenyewe kama ukweli kwa ajili ya sisi kuufuata. Wao ni kama tu Mafarisayo wanafiki na wao ni vipofu wanaojaribu kuongoza njia. Wanampinga Kristo, wakijaribu kumpinga Yeye kwa usawa; wao ni wapinga Kristo wanaofanya kazi kutengeneza falme huru zilizotengana. Mara sisi waumini tunapoanza kuwafuata viongozi na watu maarufu wa dunia ya dini, tunaanza kuenenda katika njia yetu wenyewe na kupotoka kutoka kwa njia ya Bwana; huu ni mfano wenye uzito sana wa kumpinga na kumsaliti Mungu. Tusipotubu, hakika kutatupwa kando na kuondolewa na Mungu.

Kimetoholewa kutoka katika Maswali na Majibu Bora zaidi Kuhusu Injili ya Ufalme

Iliyotangulia: Kumfuata Mungu ni nini?

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Kumfuata Mungu ni nini?

Maneno Husika ya Mungu: Kilicho na umuhimu mkuu katika kumfuata Mungu ni kwamba kila kitu kinapaswa kuwa kwa kadri ya maneno ya Mungu leo:...

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp