444 Una Uhusiano wa Kawaida na Mungu?

1 Ikiwa unataka kufuatilia kukamilishwa na Mungu na kuingia kwenye njia muwafaka ya maisha, basi lazima moyo wako uishi katika uwepo wa Mungu daima. Usiwe mwovu, usimfuate Shetani, usimpe Shetani fursa zozote za kutekeleza kazi yake, na usimruhusu Shetani akutumie. Lazima ujitolee kwa Mungu kabisa na umruhusu Mungu akutawale. Je, uko tayari kuwa mtumishi wa Shetani? Uko tayari kutumiwa vibaya na Shetani? Unamwamini Mungu na kumfuatilia ili uweze kukamilishwa na Yeye, au ili uweze kuwa foili[a] kwa ajili ya kazi Mungu? Ungependa maisha yenye kusudi ambayo unapatwa na Mungu, au maisha yasiyofaa na matupu?

2 Ungependa kutumiwa na Mungu, au kudhulumiwa na Shetani? Ungependa kuruhusu maneno na ukweli wa Mungu vikujaze, au uruhusu kujazwa na dhambi na Shetani? Zingatia mambo haya kwa uangalifu. Katika maisha yako ya kila siku, lazima uelewe ni maneno gani unayoyasema na ni mambo gani unayoyafanya ndiyo yanaweza kusababisha hitilafu katika uhusiano wako na Mungu, na kisha ujibadilishe ili uingie katika njia muwafaka. Wakati wote, yachunguze maneno yako, matendo yako, kila harakati yako, na mawazo na maoni yako yote. Pata ufahamu muwafaka kuhusu hali yako halisi na uingie katika njia ya kazi ya Roho Mtakatifu. Hii ndiyo njia ya pekee ya kuwa na uhusiano wa kawaida na Mungu.

3 Kwa kutathmini kama uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida, utaweza kurekebisha nia zako, kuelewa asili na kiini cha mwanadamu, na kujielewa kwa kweli, na kwa kufanya hivyo, utaweza kuingia katika matukio halisi, ujikane kwa njia halisi, na kutii kwa kusudi. Unapopitia mambo haya kuhusu ikiwa uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida au la, utapata fursa za kukamilishwa na Mungu na kuweza kufahamu hali nyingi za kazi ya Roho Mtakatifu. Pia utaweza kubaini hila nyingi za Shetani na kufahamu njama zake. Njia hii tu ndiyo inayosababisha kukamilishwa na Mungu.

Umetoholewa kutoka katika “Uhusiano Wako Na Mungu Ukoje?” katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 443 Zingatia Maneno ya Mungu kwa Ajili ya Uhusiano Ufaao na Wengine

Inayofuata: 445 Mfanano wa Wale Wanaotumiwa na Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp