81 Hukumu ya Siku za Mwisho Ndiyo Kazi ya Kukamilisha Enzi

1 Hata hivyo siku za mwisho ni tofauti kabisa na Enzi ya Neema na Enzi ya Sheria. Kazi ya siku za mwisho haifanyiki katika taifa la Israeli, lakini kati ya mataifa; ni ushindi mbele ya kiti Changu cha enzi cha watu kutoka mataifa yote na makabila yote nje ya Israeli, ili utukufu Wangu katika ulimwengu wote uweze kujaza ulimwengu na anga. Iko hivyo ili Niweze kupata utukufu mkuu, ili viumbe vyote duniani viweze kupitisha utukufu Wangu kwa mataifa yote, milele katika vizazi vyote, na viumbe vyote mbinguni na duniani viweze kuuona utukufu wote ambao Nimepata duniani.

2 Kazi inayofanyika katika siku za mwisho ni kazi ya ushindi. Sio uongozi wa maisha ya watu wote duniani, lakini hitimisho la maisha ya milenia ya mwanadamu yasiyoangamia, ya mateso katika dunia. Hii ni kwa sababu siku za mwisho ni hitimisho la nyakati nzima. Ni ukamilisho na tamatisho la mpango wa miaka elfu sita wa usimamizi wa Mungu, na kuhitimisha safari ya maisha ya mateso ya mwanadamu. Hazichukui binadamu wote hadi katika enzi mpya au kuruhusu maisha ya mwanadamu kuendelea. Hiyo haitakuwa na umuhimu wowote kwa ajili ya mpango Wangu wa usimamizi au kuwepo kwa mwanadamu.

3 Kazi Yangu inadumu kwa miaka elfu sita tu, na Mimi niliahidi kwamba udhibiti wa yule mwovu juu ya wanadamu wote utakuwa pia si zaidi ya miaka elfu sita. Na kwa hivyo, wakati umeisha. Katika siku za mwisho Nitamshinda Shetani, nami Nitaumiliki tena utukufu Wangu wote, na kurudisha nafsi zile zote zilizo Zangu duniani ili nyoyo hizi za dhiki ziweze kutoroka kutoka bahari ya mateso, na hivyo Nitakuwa nimetimiza kazi Yangu nzima duniani. Kutoka siku hii na kuendelea, kamwe Sitawahi kuwa mwili duniani, na kamwe Roho Wangu wa kudhibiti yote Hatafanya kazi tena duniani. Lakini Nitafanya jambo moja duniani: Nitamfanya tena mwanadamu, mwanadamu aliye mtakatifu, na aliye mji Wangu mwaminifu duniani.

Umetoholewa kutoka katika “Hakuna Aliye wa Mwili Anayeweza Kuepuka Siku ya Ghadhabu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 80 Matokeo ya Kukwepa Hukumu

Inayofuata: 82 Njia ya Pekee kwa Binadamu Kuingia katika Mapumziko

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp