285 Wimbo wa Kumpenda Mungu Bila Majuto

1

Njia ya ufalme ni yenye miamba ya milima na mabonde mengi.

Kutoka kifo hadi uzimani katikati ya mateso na machozi mengi.

Bila mwongozo na ulinzi wa Mungu, ni nani angeweza kufika leo?

Mungu alitawala na kupanga kuzaliwa kwetu katika siku za mwisho, na tuna bahati kumfuata Kristo.

Mungu hujinyenyekeza Mwenyewe kuwa Mwana wa Adamu, na Hupitia aibu kubwa sana.

Mungu ameteseka sana, nawezaje kuitwa mtu kama simpendi Mungu?

2

Haijalishi majaribu ni mengi au mateso ni mengi kiasi gani, maneno ya Mungu yanaonyesha njia.

Ingawa moyo wangu hulia kwa kusumbuka, najua kwamba Mungu anapendeka.

Haijalishi kiasi cha usafishaji ninachopitia, haijalishi mateso yangu yalivyo makubwa, sina majuto, sina malalamiko.

Upendo wa Mungu kwa mwanadamu hauna mipaka. Anafanya ukweli uwe maisha yao.

Maneno ya Mungu ni yenye thamani sana, tabia Yake ni nzuri sana.

Baada ya kuingia kwenye njia ya kumpenda Mungu, sitajuta kamwe kumfuata Yeye na kumshuhudia.

Ingawa naweza kuwa dhaifu na hasi, kupitia machozi moyo wangu bado unampenda Mungu.

Navumilia mateso na kutoa upendo wangu kwa Mungu, nisimsababishie huzuni tena kamwe.

Kupitia ugumu katika dhiki ni vizuri kama dhahabu inavyojaribiwa kwa moto; ningekosaje kuutoa moyo wangu?

Njia ya mbinguni ni ngumu na yenye miamba. Kutakuwa na machozi, lakini nitampenda Mungu kwa kina zaidi na sitakuwa na majuto.

3

Kwa kupitia hukumu na kuadibu kwa maneno ya Mungu, moyo wangu umeshindwa.

Ingawa nimepitia hukumu, majaribu na usafishaji, nimepata uzima.

Kazi yote ya Mungu mwenye mwili ni halisi, niulize nini zaidi?

Nikitafuta kumpenda Mungu na kupata ukweli, hakika naweza kumfuata Mungu mpaka mwisho.

Mungu hupitia maumivu mengi kwa ajili ya mwanadamu; na nitumie maisha yangu yote kulipiza fadhila Zake.

Nitakubali maisha ya usafishaji, na kutafuta tu moyo unaompenda Mungu. Mradi tu naweza kumjua Mungu, nitakuwa tayari kufa.

4

Kwa kuwa mtu mwaminifu na kutafuta kumpenda Mungu, naweza kulingana na Yeye.

Kwa kumpenda Mungu na kumcha kwa moyo wangu wote hakika nitapata sifa Zake.

Kwa kupitia maneno ya Mungu na kutenda ukweli, napata mwongozo na baraka Zake.

Kupitia mateso makubwa, kupitia majaribio na usafishaji, tabia yangu potovu hutakaswa.

Nitampenda Mungu na sitazungumza kuhusu thawabu, nami nitauweka moyo wangu katika kumridhisha Mungu.

Nikipata ukweli na uzima na niweze kumjua Mungu, basi maisha yangu hayataishiwa bure.

Moyo wangu una furaha sana ninapopitia kazi ya Mungu na kujua matendo ya Mungu.

Baada ya kuona kuonekana kwa Mungu katika siku za mwisho, nataka kumtumikia maisha yangu yote.

Natoa yote niliyo nayo kwa ajili ya maisha haya, na niko tayari kutoa maisha yangu kumfuata Mungu.

Natafuta tu kumpendeza Mungu na niko radhi kupitia kukataliwa. Kumpenda Mungu na kumtolea ushuhuda ni wa utukufu!

Iliyotangulia: 284 Kutembea kwenye Njia ya Kumpenda Mungu

Inayofuata: 286 Kuwa Jasiri Katika Njia ya Kumpenda Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp