813 Maarifa ya Petro ya Yesu

1 Petro alimfuata Yesu kwa miaka kadhaa na aliona mambo mengi ndani ya Yesu ambayo watu hawana. Kila kitendo cha Yesu kilikuwa mfano kwake katika maisha yake, na mahubiri ya Yesu yaliwekwa hasa katika kumbukumbu ndani ya moyo wake. Alikuwa mwenye busara sana na wa kujitolea kwa Yesu, na kamwe hakuwa na malalamiko kumhusu Yesu. Hii ndiyo maana alikuwa mwandani mwaminifu wa Yesu popote Alipoenda. Petro alichunguza mafunzo ya Yesu, maneno Yake yasiyo makali, na kile Alichokula, Alichovaa, maisha Yake ya kila siku, na safari Zake. Alifuata mfano wa Yesu katika kila njia. Hakuwa wa kujidai, lakini alitupa vitu vyake yote vya awali vilivyopitwa na wakati akafuata mfano wa Yesu katika maneno na matendo.

2 Ni wakati huo ndipo alihisi kwamba mbingu na dunia na vitu vyote vilikuwa ndani ya mikono ya Mwenyezi, na kwa sababu hii hakuwa na chaguo lake mwenyewe, lakini alichukua kila kitu ambacho Yesu alikuwa ili kiwe mfano wake. Angeweza kuona kutoka kwa maisha yake kwamba Yesu hakuwa wa kujivuna katika kile Alichofanya, wala Hakujigamba kuhusu Mwenyewe, lakini badala yake, Aliwavuta watu na upendo. Katika hali mbalimbali Petro angeweza kuona kile ambacho Yesu alikuwa. Hiyo ndiyo maana kila kitu ndani ya Yesu kilikuwa chombo ambacho Petro alikifuata kama mfano. Katika uzoefu wake, alihisi kupendeza kwa Yesu zaidi na zaidi.

3 Alisema kitu kama hiki: “Nilimtafuta Mwenyezi katika ulimwengu na nikaona maajabu ya mbingu na dunia na vitu vyote, na hivyo nilikuwa na hisi kuu ya kupendeza kwa Mwenyezi. Lakini sikuwa kamwe na upendo halisi ndani ya moyo wangu, na sikuona kamwe kupendeza kwa Mwenyezi kwa macho yangu mwenyewe. Leo, katika macho ya Mwenyezi, nimetazamwa na fadhila na Yeye na hatimaye nimehisi kupendeza kwa Mungu, na hatimaye nimegundua kwamba kwa Mungu, siyo tu kuumba vitu vyote ambavyo vingewafanya wanadamu wampende Yeye. Katika maisha yangu ya kila siku nimepata kupendeza Kwake kusiko na kikomo; ni vipi ambavyo ingewezekana kuwekewa mipaka tu katika hali hii leo?”

Umetoholewa kutoka katika “Kuhusu Maisha ya Petro” ya Ufafanuzi wa Mafumbo ya Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 812 Petro Alilenga Kumjua Mungu kwa Vitendo

Inayofuata: 814 Una Ufahamu Kuhusu Misheni Yako?

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp