650 Lazima Utambue Maana ya Mateso Yako ya Sasa

1 Watu wengi sasa wanamwamini Mungu ila hawajaingia katika njia iliyo sawa. Bado wanahisi watupu na watepetevu, wakati mwingine hata kuhisi kana kwamba kuishi kote ni mateso, utupu wote—hata wanatamani kufa! Hivi ndivyo mtu alivyo kabla ya moyo wake kuwa na maono. Mtu wa aina hii hajapata ukweli na hamjui Mungu bado, hivyo bado hahisi furaha nyingi ya ndani. Ninyi, hasa, mmepitia mateso na kupata ugumu katika kurudi nyumbani; mnateseka, na pia mna fikra za kifo na kutokuwa na radhi kuishi. Haya ni mapungufu ya mwili. Baadhi ya watu hata hufikiri kuwa ikiwa wanamwamini Mungu basi wanapaswa kuhisi ridhaa ndani yao. Leo kumwamini Mungu kunaudhi.

2 Unajua tu kuwa ridhaa ya mwili ni nzuri kupita chochote kingine. Hujui kile ambacho Mungu anafanya leo. Mungu lazima aruhusu miili yenu iteseke ili kubadilisha tabia yenu. Hata ingawa miili yenu inateseka, mna neno la Mungu na mna baraka ya Mungu. Huwezi kufariki hata ukitaka: Je, unaweza kukubali bila malalamiko kutomjua Mungu na kutopata ukweli ukifa? Sasa, hasa, ni kuwa tu bado watu hawajapata ukweli, na hawana maisha. Sasa hasa ni kuwa tu bado watu hawajapata ukweli, na hawana maisha. Sasa watu wako katikati ya mchakato wa kutafuta wokovu, hivyo lazima wayapitie baadhi ya hayo wakati huu.

3 Leo kila mtu duniani kote hujaribiwa: Mungu bado anateseka—je, ni vyema kwamba msiteseke? Bila kusafishwa kupitia maafa makubwa hakuwezi kuwa na imani halisi, na ukweli na uzima havitapatikana. Kutokuwa na majaribio na usafishaji kusingesaidia. Unaona, Petro alijaribiwa kwa miaka saba mwishowe. Aliyapitia mamia ya majaribio katika miaka hiyo saba, na baada tu ya hiyo miaka mitatu na mitatu na moja zaidi ndipo alipopata uzima na mabadiliko ya tabia yake. Hivyo, unapopata ukweli kwa kweli na kuja kumjua Mungu unahisi kuwa maisha yanapaswa kuishi kwa ajili ya Mungu. Kutoishi kwa ajili ya Mungu ni jambo la kujutia sana. Ungeishi maisha yako kwa majuto machungu na toba iliyopita kiasi.

Umetoholewa kutoka katika “Jinsi ya Kujua Asili ya Mwanadamu” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo

Iliyotangulia: 649 Huwezi Kusikitisha Mapenzi ya Mungu

Inayofuata: 651 Kupitia Shida Kuna Umuhimu Mkubwa

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp