231 Lazima Uichukulie Biblia kwa Usahihi

1 Biblia imekuwa sehemu ya historia ya binadamu kwa miaka mingi. Zaidi ya hayo, watu huichukulia kuwa Mungu, kufikia kiwango ambapo katika siku za mwisho, imechukua nafasi ya Mungu, jambo ambalo linamchukiza Mungu. Hivyo, muda uliporuhusu, Mungu alihisi kulazimishwa kubainisha maelezo ya ndani na vyanzo vya Biblia; Asingefanya hivi, Biblia ingeendelea kushikilia nafasi ya Mungu mioyoni mwa watu, na watu wangetumia maneno ya Biblia kupima na kushutumu matendo ya Mungu. Ukweli ambao Mungu angetaka kuwaambia watu hapa ni kwamba hakuna nadharia ama ukweli ambao unaweza kuchukua nafasi ya kazi na maneno ya Mungu ya leo, na kwamba hakuna kitu kinachoweza kuwa mbadala wa Mungu.

2 Ikiwa watu hawawezi kuepuka mtego wa Biblia, hawatawahi kuweza kuja mbele za Mungu. Ikiwa wanataka kuja mbele za Mungu, lazima kwanza waitakase mioyo yao na kuondoa chochote kinachoweza kuchukua nafasi Yake; kisha watamridhisha Mungu. Ingawa Mungu anaifafanua Biblia pekee hapa, usisahau kwamba kuna mambo mengi yenye makosa ambayo watu wanayaabudu kwa kweli kando na Biblia; mambo wasiyoyaabudu ni yale yanayotoka kwa Mungu kwa kweli pekee. Mungu anatumia tu Biblia kama mfano kuwakumbusha watu wasichukue njia mbaya, na wasivuke mipaka tena na kukanganyikiwa wanapomwamini Mungu na kukubali maneno Yake.

Umetoholewa kutoka katika Utangulizi wa Maneno ya Kristo Alipokuwa Akitembea Makanisani katika Neno Laonekana katika Mwili

Iliyotangulia: 230 Biblia Itawezaje Kuwaleta Watu Katika Enzi Mpya?

Inayofuata: 232 Mungu Amefanya Kazi Kubwa na Mpya Zaidi Kati ya Mataifa Katika Siku za Mwisho

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp