513 Tafuta Ukweli Katika Kila Kitu

1 Idhini kutoka kwa Mungu ni jambo la kwanza unalopaswa kufikiria kuhusu na kulifanyia kazi; inapaswa kuwa kanuni na wigo la matendo yako. Sababu ikupasayo kuamua iwapo kile unachokitenda kinapatana na ukweli ni kwamba kikipatana na ukweli, basi hakika kinalingana na mapenzi ya Mungu. Si kwamba unapaswa kupima iwapo jambo ni sahihi au kosa, au kama linalingana na kile watu wote wanachopenda, au ikiwa kinapatana na tamaa zako mwenyewe; badala yake, unapaswa kuamua iwapo inalingana na ukweli, na iwapo inafaidi kazi na masalahi ya kanisa au la. Ukizingatia vitu hivi, basi utakuwa zaidi na zaidi sawa na mapenzi ya Mungu unapofanya vitu.

2 Kama huzingatii vipengele hivi, na utegemee tu mapenzi yako unapofanya vitu, basi una uhakikisho kuvifanya kimakosa, kwa sababu mapenzi ya mwanadamu sio ukweli na, bila shaka, hayalingani na Mungu. Ukitaka kupewa idhini na Mungu, basi ni lazima utende kulingana na ukweli badala ya kulingana na mapenzi yako mwenyewe. Bila kujali unachokifanya, jambo ni kubwa au dogo kiasi gani, na kama unalifanya ili kutimiza wajibu wako katika familia ya Mungu au kwa ajili ya sababu zako za faragha, lazima ufikirie kama kile unachofanya kinalingana na mapenzi ya Mungu, na vile vile kama ni kitu ambacho mtu ambaye ana ubinadamu anapaswa kufanya. Ukitafuta ukweli kwa namna hiyo katika kila kitu unachofanya, basi wewe ni mtu anayemwamini Mungu kwa kweli. Ukishughulikia kwa moyo wote kila jambo na kila ukweli kwa njia hii, basi utaweza kufanikisha mabadiliko katika tabia yako.

3 Watu wengine hufikiri kwamba wanapokuwa wakifanya kitu cha kibinafsi, wanaweza tu kupuuza ukweli, wakifanye watakavyo, na wakifanye kwa njia yoyote inayowafurahisha na kwa namna yoyote ile iliyo na faida kwao. Hawafikirii hata kidogo jinsi inavyoweza kuathiri familia ya Mungu, wala hawafikirii kama kile wanachofanya kinastahili umakini wa kitakatifu. Hatimaye, punde wanapomalizana na jambo hili, wanakuwa waovu ndani yao na kuhisi wasiwasi, ingawa hawajui ni kwa nini. Je, si hii ni adhabu inayowafaa? Ukifanya vitu ambavyo havijaidhinishwa na Mungu basi umemkosea Mungu. Ikiwa mtu hapendi ukweli, na mara nyingi nafanya vitu kulingana na mapenzi yake, basi atamkosea Mungu mara kwa mara. Watu kama hao kwa kawaida hawakubaliwi na Mungu katika yale wayatendayo, na wasipotubu, basi adhabu haitakuwa mbali sana nao.

Umetoholewa kutoka katika “Kutafuta Mapenzi ya Mungu ni Kwa Ajili ya Kutenda Ukweli” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo

Iliyotangulia: 512 Ni Msingi wa Maneno ya Mungu tu Unaotoa Njia ya Kutenda

Inayofuata: 514 Njia ya Kutafuta Ukweli

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp