Kuona Uhalisi Wangu Kwa Dhahiri

14/01/2018

Xiaoxiao Jijini Xuzhou, Mkoani Jiangsu

Kwa sababu ya mahitaji ya kazi ya kanisa, nilihamishwa mpaka mahali pengine ili kutimiza wajibu wangu. Wakati huo, kazi ya injili mahali pale ilikuwa katika hali duni, na hali ya akina kaka na dada kwa kawaida haikuwa nzuri. Lakini kwa kuwa nilikuwa nimeguswa na Roho Mtakatifu, bado nilijitwisha kila kitu nilichoaminiwa nacho kwa matumaini kamili. Baada ya kukubali kuaminiwa, nilihisi uwajibikaji kamili, kupata nuru kamili, na hata nikafikiri kwamba nilikuwa na uamuzi kiasi fulani. Niliamini kuwa nilikuwa na uwezo na ningeweza kutekeleza kazi hii vizuri. Kwa kweli, wakati huo sikuwa na maarifa kabisa ya kazi ya Roho Mtakatifu au ya asili yangu mwenyewe. Nilikuwa naishi kabisa katika kujiridhisha na kujitamani.

Wakati uo huo nilipokuwa nimejawa na majivuno, nilikutana na ndugu katika familia ya wenyeji aliyekuwa msimamizi wa kazi hiyo. Aliniuliza kuhusu hali kuhusiana na kazi yangu, na nilijibu maswali yake moja baada ya lingine huku nikiwaza: Kwa hakika atatazama na kupendezwa na uwezo wa kazi yangu na umaizi wangu wa kipekee. Lakini sikuwahi kutarajia kwamba baada ya kusikiliza majibu yangu, hakutikisa kichwa kwa kufahamu tu, alisema kwamba kazi yangu ilikuwa na upungufu, kwamba wafanyakazi hawajahamasishwa vizuri, kwamba sijatimiza matokeo yoyote, na kadhalika. Kwa kutazama sura yake yenye kutoridhika na kusikiliza ukadiriaji wake wa kazi yangu, moyo wangu ulihisi baridi ghafla. Niliwaza: “Anasema kazi yangu ni pungufu? Kama sijatimiza matokeo yoyote, basi nitalazimika kufanya nini ndiyo ihesabike kama kutimiza matokeo? Inapasa kutosha kwamba sijachukia kazi hii iliyooza na nilikuwa radhi kuikabili, na bado anasema kwamba sijafanya kazi nzuri.” Nilikuwa muasi sana moyoni mwangu na kuhisi kukosewa kiasi kwamba machozi nusra yaanze kumwagika. Yale mambo ya ufidhuli, yasiyoridhika na ya uasi ndani mwangu yalijitokeza kwa ghafla: Ubora wangu wa tabia unaweza kutimiza kiasi hiki tu; nimefanya kila niwezalo hata hivyo, hivyo kama nina upungufu basi ni afadhali watafute mtu mwingine… Moyo wangu ulikuwa wenye wasiwasi sana na sikujua cha kufanya, nisijue kile cha kufikiri kuhusu hilo, na hivyo sikuweza kusikia hata neno moja alilosema baada ya hapo. Katika siku hizo chache, hali yangu ilibadilika kutoka kwa kujawa na majivuno mpaka kuwa yenye huzuni na kuvunjika moyo, kutoka kuwa mwenye furaha na mimi mwenyewe mpaka kuwa mwenye tumbo lililojaa masikitiko. Hisia ya kupoteza ilinikumba. … Kati ya kiza hicho, nilikumbuka maneno ya Mungu: “Petro alitafuta kuishi kwa kudhihirisha picha ya yule ambaye hupenda Mungu, kuwa mtu ambaye alimtii Mungu, kuwa mtu ambaye alikubali ushughulikaji na upogoaji …(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mafanikio au Kushindwa Kunategemea Njia Ambayo Mwanadamu Hutembea). Na mimi je? Kile alichofanya mtu ni kunikosoa tu kidogo, kusema kuwa kazi yangu haikuwa nzuri sana, na nikahisi kukasirika na kutaka kuiacha kazi yangu. Je, huyu ni mtu aliye tayari kukubali ushughulikiaji na upogoaji? Je, huku ni kutafuta kumpenda Mungu kama Petro? Je, si yale ambayo nimefichua ni yale ambayo Mungu huchukia? Kutotaka wengine kusema sikufanya vizuri vya kutosha na kutaka tu kupokea sifa za wengine na utambuzi wao—je, si huo ni ufuatiliaji wa msingi zaidi? Katika wakati huo, nilikuwa na mwali wa mwangaza moyoni mwangu, hivyo nilifungua Neno Laonekana katika Mwili na kuona kifungu kama hiki: “Ingekuwa bora kwenu kuweka juhudi zaidi kwa ukweli wa kuzijua nafsi zenu. Mbona hamjapata fadhili kwa Mungu? Kwa nini tabia zenu ni chukizo sana Kwake? Kwa nini maneno yenu yanachochea chuki Yake? Punde ambapo mmeonyesha uaminifu kidogo, nyinyi mnajisifu wenyewe, na mnadai malipo kwa ajili ya mchango mdogo; nyinyi huwadharau wengine wakati nyinyi mnaonyesha utiifu kidogo, na kumdharau Mungu baada ya kufanya kazi ndogo. … Ubinadamu kama wenu kweli ni wa kukera kuzungumziwa au kusikizwa. Kuna chochote kinachostahili sifa katika maneno na matendo yenu? … Je, hamuoni hili likiwa la kuchekesha? Mkijua vyema kwamba mnamwamini Mungu, hata hivyo ninyi hamwezi kulingana na Mungu. Kweli mnajua vyema kwamba hamstahili hata kidogo. Je, hamhisi kuwa hisia yenu imepunguka kiasi kwamba hamwezi tena kujizuia? Na hisia kama hii, mnastahili vipi kushirikiana na Mungu? Je, kufikia hapa nyinyi hamjionei hofu? Tabia yenu tayari imepunguka kiasi kwamba hamwezi kulingana na Mungu. Hali ikiwa hivi, je, imani yenu si ya kuchekesha? Imani yenu si ya kipuuzi? Ni jinsi gani utashughulikia maisha yako ya baadaye? Ni jinsi gani utachagua njia ya kutembelea?(Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Wale Ambao Hawalingani na Kristo Hakika Ni Wapinzani wa Mungu). Maneno ya Mungu yalichoma kiini changu kama upanga mkali, yakiniacha bila la kusema. Niliona haya sana na kujawa na aibu kubwa. Sababu zangu na mapambano yangu ya ndani yalitoweka kama moshi yasiwepo tena. Wakati huo, nilipitia nguvu na mamlaka ya neno la Mungu kwa kina ndani ya moyo wangu. Kupitia kwa ufunuo wa neno la Mungu, hatimaye nilipata kujijua mwenyewe: Katika kutimiza wajibu wangu sikujitahidi kila mara kupata ukamilifu kutimiza matokeo bora zaidi ili kumridhisha Mungu, lakini badala yake niliridhika na hali ilivyokuwa na kuhisi kufurahishwa na mimi mwenyewe sana. Nilishindwa tu kutambua kwamba hali yangu mwenyewe ingechukiwa na Mungu, na hata nilihisi vibaya nilipokosolewa na mtu. Kwa kweli nilikuwa mpumbavu na asiye na busara! Kila mara nilikuwa nikitafuta sifa kwa kufanya kazi kidogo, na mara tu ambapo haikupokelewa, nguvu yangu yote ingetoweka; Nilinuna kwa kuudhika bila sababu wakati juhudi zangu zilitiliwa shaka badala ya kuthaminiwa sana. Wakati huo, niliona uso wangu wa unafiki. Niliona kwamba utimizaji wa wajibu wangu ulikuja na madai na shughuli na ulikuwa umejaa uchafu. Haukuwa wa kumridhisha Mungu au kulipiza upendo Wake, lakini kwa ajili ya nia mbaya.

Zamani, nilipoona neno la Mungu likifichua hali ya chini ya ubinadamu wa mwanadamu, halikuwahi kung’aa katika moyo wangu na nilishuku kwamba neno la Mungu likikuwa linatia chumvi. Ilikuwa ni kupitia kwa Mungu kuliweka wazi ndiyo nilipata mwamko: Kuweza kutimiza wajibu wangu leo ni kupandishwa pakubwa wa Mungu na upendo Wake mkuu. Ilhali sikulitunza au kulithamini, na badala yake nilifuatilia mambo ambayo hayakuwa na thamani na maana—kusifiwa na watu, kutukuzwa na watu, kuonekana na watu, na kuwa na hadhi katika mioyo ya watu. Mambo haya yana maana gani? Mungu anasema mwanadamu haishi kwa kutegemea chakula tu, bali pia kwa maneno yaliyoonyeshwa kupitia kwa Kristo. Lakini maisha yangu yalitegemea nini? Niliishi kwa kutegemea mtazamo wa watu kwangu na jinsi walivyoniona, na mara nyingi nilikuwa na wasiwasi kuhusu faida za kibinafsi na hasara ambazo ningepata kwa ajili ya mambo kama hayo. Maneno machache ya utambuzi au sifa au maneno machache ya kuliwaza au kujali ungefanya nguvu yangu kuongezeka maradufu; maneno machache ya kukosoa au sura hasi ingenifanya nivunjike moyo na kupoteza nguvu na mwelekeo wa kufuatilia kwangu. Basi kwa nini mwishowe ninaamini kwa Mungu? Inaweza kuwa kwa sababu ya idhini ya watu tu? Kama maneno ya Mungu yalivyofichua, nilichojali kuhusu hakikuwa ukweli, si kanuni za kuwa binadamu, na sio kazi ya jitihada ya Mungu, bali kile ambacho mwili wangu hupenda, mambo ambayo hayana manufaa kabisa katika maisha yangu. Je, shauku ya mwingine kwangu inaweza kuthibitisha kwamba Mungu hunisifu? Kama siwezi kulingana na Mungu, basi si ufuatiliaji wangu bado ni bure? Shukrani kwa Mungu kwa kunipa nuru! Kutoka kwa ufunuo wangu mwenyewe kisha niliwaza juu ya nafsi ya Kristo, kuhusu jinsi Kristo alivyokuja kufanya kazi duniani kumwokoa binadamu. Lakini mtazamo wa mwanadamu kwa Mungu ni upi? Yeye ni mtakatifu na wa heshima, Mungu mtukufu Mwenyewe, lakini ni nani kwa kweli anayemthamini Mungu, ni nani anayemruhusu awe na nafasi moyoni mwake, na ni nani anayemtukuza Mungu? Mbali na uasi na upinzani, yote ambayo mwanadamu anawasilisha ni kukataa, na bado Kristo kamwe Hamlalamikii binadamu au kuwatendea watu kulingana na dhambi zao. Anastahimili magumu yote kwa ukimya, akitumia raslimali kwa ajili ya wanadamu, lakini kuna yeyote ambaye huonyesha sifa kutoka moyoni mwake kwa ajili ya unyenyekevu wa Kristo, wema Wake au ukarimu Wake? Kwa ulinganisho, niliona zaidi na zaidi ya mawazo yangu finyu, nilivyolalamika kuhusu mambo, jinsi nilivyotumaini kusifiwa na watu au kuthaminiwa nao, na tabia zingine za uchoyo, za kudharauliwa na za aibu. Hata na tabia ya kiwango cha chini vile, bado nilijiona nikiwa na thamani kama dhahabu. Ndiyo maana Mungu husema hisia ya binadamu imefika kiwango ambacho ni vigumu kwa binadamu kudhibiti. Maneno ya Mungu yameniridhisha kabisa. Wakati huu, aina ya hamu na upendo kwa Kristo—Bwana wa kila kitu—uliundika ghafla katika kina cha moyo wangu. Sikuweza kujizuia kuomba kwa Mungu: “Ee Mungu! Tabia Yako, kiini Chako na uzuri Wako hunifanya kila mara niwe na wivu. Nani anayeweza kulinganishwa na Wewe? Kile ambacho Umeonyesha na kufichua miongoni mwetu na kila kitu ambacho Umetuonyesha vyote ni udhihirisho wa uzuri Wako, uadilifu Wako, haki Yako na uadhama. Ee Mungu! Umeufungua moyo wangu na kunifanya nihisi haya, kunifanya niinamishe kichwa changu chini. Unajua kwa kina kuhusu majivuno yangu, ubatili wangu. Isingekuwa kwa ajili ya mipango Yako ya ajabu na mipangilio, isingekuwa kwa ajili ya ndugu Uliyemtuma kunishughulikia, ningelijisahau mimi ni nani kitambo sana. Kuiba utukufu Wako huku nikihisi mwenye majivuno—sikuona aibu kwa kweli! Ee Mungu! Kwa sababu ya ufunuo Wako na ulinzi, niliweza kuona nafsi yangu ya kweli kwa wazi na kugundua uzuri Wako. Ee Mungu! Sitaki tena kuwa hasi, na sitaki tena kuishi kwa ajili ya vitu vile vya chini. Tamanio langu la pekee ni kwamba, kupitia kwa kuadibu na hukumu Yako, mipigo na nidhamu Yako, nikujue Wewe, nikutafute, na zaidi ya hayo kupitia kwa ushughulikiaji Wako na upogoaji niweze kutimiza wajibu wangu ili niweze kukulipiza Wewe!”

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Mbona Ujihusishe na Hila Unapomtumikia Mungu

Ee Mungu! Asante kwa kufunua asili yangu ya kiburi na majivuno. Kuanzia siku hii na kuendelea, hakika nitachukulia hili kama onyo na kuweka juhudi zaidi katika kujua asili yangu. Nitafanya kazi hasa kulingana na mipangilio ya kazi. Kwa kweli nitakuwa mtu mwenye mantiki, anayezingatia kanuni, na aliye na moyo wa uchaji Kwako.

Ninapata njia ya kumjua Mungu

Xiaocao Mji wa Changzhi, Mkoa wa Shanxi Siku moja, niliona kifungu hiki kifuatacho cha neno la Mungu kwa maandishi “Namna Petro...

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp