Sura ya 34

Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu zote, mwenye kutimiliza yote na Mungu wa kweli mkamilifu! Habebi tu nyota saba, ana Roho saba, ana macho saba, anafungua mihuri saba na kufungua hati ya kukunja yenye maandishi, lakini zaidi ya hayo Yeye anaendesha mapigo saba na vitasa saba na kufungua radi saba; zamani za kale Yeye alipiga vinumbi saba! Vitu vyote vilivyoumbwa na kufanywa kuwa kamili na Yeye vinapaswa kumsifu, kumpa adhama na kutukuza kiti Chake cha enzi. Ee, Mwenyezi Mungu! Wewe ni kila kitu, Wewe umetimiza kila kitu, na kila kitu kinakamilika na Wewe, vyote vinang’aa, vyote vimekombolewa, vyote viko huru, vyote viko imara na vyenye nguvu! Hakuna chochote kilichofichwa wala kufungwa, na Wewe mafumbo yote yanafumbuliwa. Aidha, Wewe unahukumu halaiki za adui Zako, unaonyesha uadhama Wako, unaonyesha moto Wako unaoendelea vikali, unaonyesha ghadhabu Yako, na hata zaidi Unaonyesha utukufu Wako ambao haujawahi kuonekana awali, wa milele na usio na mwisho! Watu wote wanapaswa kuamka na wanapaswa kushangilia na kuimba bila kusita, wakihimidi mwenye Uweza, yule wa kweli, anayeishi, mkarimu, adhimu na Mungu wa kweli aliye kutoka milele hadi milele. Kiti Chake cha enzi kinapasa kutukuzwa kila wakati, jina Lake takatifu kusifiwa na kutukuzwa. Haya ni mapenzi Yangu—ya Mungu—ya milele na ni baraka zisizo na mwisho ambazo Yeye hutufichulia na kutukarimia! Je, ni nani kati yetu ambaye hairithi? Ili kurithi baraka za Mungu, mtu lazima alitukuze jina takatifu la Mungu na kuja kumwabudu kwa kuzunguka kiti Chake cha enzi. Wale wote ambao wanaenda mbele Yake wakiwa na nia nyingine na dhamira nyingine wanayeyushwa na moto Wake wenye ghadhabu. Leo ni siku ambayo adui Zake watahukumiwa, na pia wataangamia katika siku hii. Hata zaidi ni siku ambayo Mimi, Mwenyezi Mungu, nitafunuliwa na Nitapokea utukufu na heshima. Enyi, watu wote! Inukeni haraka ili mhimidi na kumkaribisha Mwenyezi Mungu ambaye milele na milele hutupa wema wenye upendo, wokovu, na kutupa baraka, huwafanya wana Wake kuwa wakamilifu na kufikia ufalme Wake kwa mafanikio! Hili ni tendo la ajabu la Mungu! Haya ni majaaliwa na mipango ya milele ya Mungu, kwamba Yeye Mwenyewe aje kutuokoa, kutufanya tuwe wakamilifu na kutuleta kwenye utukufu.

Wale wote ambao hawainuki na kuwa na ushuhuda ni wahenga wa vipofu, wafalme wa wasiojua na watakuwa daima wasiojua, wajinga wa milele na vipofu waliokufa daima. Kwa hivyo nafsi zetu zinapasa kuamka! Watu wote wanapaswa kuinuka! Mshangilie, msifu na kumhimidi Mfalme wa utukufu, Baba wa huruma, Mwana wa ukombozi bila kikomo, Roho saba zenye ukarimu, na Mwenyezi Mungu anayeleta moto adhimu wenye ghadhabu na hukumu yenye haki, anayejitosheleza, mkarimu, mwenye Uweza, na mkamilifu. Kiti Chake cha enzi kitatukuzwa milele! Watu wote wanafaa kuona kwamba hii ni hekima ya Mungu, ni njia Yake ya shani ya wokovu, na utimilifu wa mapenzi Yake yenye utukufu. Tusipoinuka na kuwa na ushuhuda, wakati muda utakapokwisha basi hakutakuwa na kurudi nyuma. Iwapo tunapokea baraka au balaa inaamuliwa katika hatua hii iliopo ya safari yetu, kulingana na tunayotenda, kufikiria au kuishi wakati huu. Basi mnapaswa kutenda yapi? Mshuhudieni na kumtukuza Mungu milele; mtukuzeni Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho—Mungu wa kweli, wa kipekee, na wa milele!

Kuanzia sasa kuendelea unapaswa kuona wazi kuwa wale wote wasiokuwa na ushuhuda kwa Mungu, wasiokuwa na ushuhuda kwa wale wa kipekee, waaminifu kwa Mungu, wale walio na tashwishi kumhusu, wote ni wagonjwa, wafu na wenye kumuasi Mungu! Maneno ya Mungu yamehakikishwa kutoka nyakati za kale: Wale wote ambao hawakusanyiki na Mimi wanatawanyika, na wale wasio upande Wangu wako dhidi Yangu; huu ni ukweli usioweza kubadilishwa uliochongwa jiweni! Wale wasiokuwa na ushuhuda kwa Mungu ni vikaragosi wa Shetani. Watu hawa huja kuwasumbua na kuwadanganya watoto wa Mungu, kukatiza usimamizi wa Mungu, na sharti wawekwe kwenye upanga! Yeyote anayewaonyesha nia nzuri anatafuta maangamizi yake mwenyewe. Unapaswa kusikiza na kuamini tamko la Roho wa Mungu, kutembea kwenye njia ya Roho wa Mungu na kuishi kwa maneno ya Roho wa Mungu, na hata zaidi kusifu kiti cha enzi cha Mwenyezi Mungu milele!

Mwenyezi Mungu ni Mungu wa Roho saba! Yule wa macho saba na nyota saba ndiye Yeye pia; Yeye hufungua mihuri saba, na hati nzima ya kukunja imekunjuliwa na Yeye! Amepiga baragumu saba, na vitasa saba na mapigo saba yako mikononi Mwake, yatakayofunguliwa kwa mapenzi Yake. Ee, ngurumo saba ambazo daima zimefungwa! Wakati wa kuzifungua umewadia! Yule atakayezifungua ngurumo saba tayari ameshaonekana mbele ya macho yetu!

Mwenyezi Mungu! Kila kitu kimekombolewa na kuwa huru na Wewe, hapana ugumu, na kila kitu kinakwenda vizuri! Hakuna kinachothubutu kukupinga au kukuzuia Wewe, vyote hukutii. Chochote kisichotii hufa!

Mwenyezi Mungu, Mungu mwenye macho saba! Vyote viko wazi vikamilifu, vyote ni ng’avu na wazi, vyote vimefunuliwa na kuwekwa wazi. Vyote ni dhahiri kabisa na Yeye, na si tu kuwa Mungu Mwenyewe yuko hivi, lakini pia wana Wake wako hivi vilevile. Hapana yeyote, hakuna kitu chochote, na hakuna hoja yoyote inayoweza kufichwa mbele Yake na wana Wake!

Nyota saba za Mwenyezi Mungu ni ng’avu bashashi! Kanisa limefanywa kuwa kamili na Yeye, Yeye huweka imara mitume wa kanisa Lake na kanisa lote liko ndani ya utoaji Wake. Yeye anafungua mihuri yote saba, na Yeye Mwenyewe analeta mpango wa usimamizi Wake na mapenzi Yake hadi tamati. Hati ndiyo kunga ya lugha ya kiroho ya usimamizi Wake na Amekifungua na kukifunua!

Watu wote wanapaswa kusikiliza baragumu Zake saba zinazopigwa kwa sauti. Kwake, vyote vinajulishwa, kamwe visifichike tena, na hakuna huzuni tena. Vyote vinafunuliwa, na vyote vinashinda!

Baragumu saba za Mwenyezi Mungu ziko wazi, baragumu adhimu na zenye ushindi! Pia ni baragumu zinazowahukumu adui Zake! Katikati ya ushindi Wake, baragumu Yake inatukuzwa! Yeye hutawala ulimwengu mzima!

Yeye amevitayarisha vitasa saba vya mapigo na vyote vinafunguliwa kwa nguvu kabisa kwa adui Zake kwa kiwango cha juu, na watateketea kwa miale ya moto Wake wenye ghadhabu. Mwenyezi Mungu huonyesha uwezo wa mamlaka Yake na adui Zake wote wanaangamia. Ngurumo saba za mwisho hazitafichwa tena mbele ya Mwenyezi Mungu, zote ziko wazi! Zote ziko wazi! Yeye huwaua adui Zake kwa ngurumo saba, Akiimarisha dunia, Akiifanya imtolee huduma, kamwe kutokuwa isiyofaa!

Mwenyezi Mungu mwenye haki! Tunakutukuza milele! Unastahili sifa zisizoisha, kuhimidiwa kusikoisha na kutukuzwa! Ngurumo Zako saba si tu za hukumu Yako, bali zaidi ni kwa ajili ya utukufu na mamlaka Yako, ili kukamilisha vitu vyote!

Watu wote wanasherehekea mbele ya kiti cha enzi, wakimtukuza na kumsifu Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho! Sauti zao zinautikisa ulimwengu mzima kama radi! Bila shaka vitu vyote vinakuwepo kwa ajili Yake, na kuinuka kwa ajili Yake. Je, ni nani anayethubutu kutoona utukufu, heshima, mamlaka, hekima, utakatifu, ushindi na ufunuo kuwa sio Zake? Huu ndio utimizaji wa mapenzi Yake na ndio ukamilishaji wa mwisho wa ujenzi wa usimamizi Wake!

Iliyotangulia: Sura ya 33

Inayofuata: Sura ya 35

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp